< Книга пророка Исаии 5 >
1 Воспою ныне Возлюбленному песнь Возлюбленнаго моего винограду моему: виноград бысть Возлюбленному в розе, на месте тучне:
Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye, kuhusu shamba lake la mizabibu: Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima chenye rutuba.
2 и ограждением оградих и окопах, и насадих лозу избранну, и создах столп посреде его, и предточилие ископах в нем, и ждах, да сотворит гроздие, и сотвори терние.
Alililima na kuondoa mawe na akaliotesha mizabibu bora sana. Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake, na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia. Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri, lakini lilizaa matunda mabaya tu.
3 И ныне, живущии во Иерусалиме и человече Иудин, судите между Мною и виноградом Моим.
“Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda, hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.
4 Что сотворю еще винограду Моему, и не сотворих ему? Занеже ждах, да сотворит гроздие, сотвори же терние.
Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika kwa shamba langu la mizabibu kuliko yale niliyofanya? Nilipotazamia kupata zabibu nzuri, kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?
5 Ныне убо возвещу вам, что Аз сотворю винограду Моему: отиму ограждение его, и будет в разграбление: и разорю стену его, и будет в попрание.
Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea shamba langu la mizabibu: Nitaondoa uzio wake, nalo litaharibiwa, nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa.
6 И оставлю виноград Мой, и ктому не обрежется, ниже покопается, и взыдет на нем, якоже на лядине, терние: и облаком заповем, еже не одождити на него дождя.
Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu, halitakatiwa matawi wala kulimwa, nayo michongoma na miiba itamea huko, nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”
7 Виноград бо Господа Саваофа, дом Израилев есть, и человек Иудин новый сад возлюбленный: ждах, да сотворит суд, сотвори же беззаконие, и не правду, но вопль.
Shamba la mzabibu la Bwana Mwenye Nguvu Zote ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni bustani yake ya kumpendeza. Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu, alitazamia uadilifu, lakini akasikia vilio vya taabu.
8 Горе совокупляющым дом к дому и село к селу приближающым, да ближнему отимут что: еда вселитеся едини на земли?
Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba na kuunganisha mashamba baada ya mashamba hadi hakuna nafasi iliyobaki, nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.
9 Услышашася бо во ушесех Господа Саваофа сия: аще бо будут домове мнози, в запустение будут велицыи и добрии, и не будут живущии в них:
Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema nikisikia: “Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa, nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.
10 идеже бо возорют десять супруг волов, сотворит корчаг един, и сеяй артавас шесть сотворит меры три.
Shamba la mizabibu la eka kumi litatoa bathi moja ya divai, na homeri ya mbegu zilizopandwa itatoa efa moja tu ya nafaka.”
11 Горе востающым заутра и сикер гонящым, ждущым вечера: вино бо сожжет я:
Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema wakikimbilia kunywa vileo, wale wakawiao sana mpaka usiku, mpaka wamewaka kwa mvinyo.
12 со гусльми бо и певницами, и тимпаны и свирельми вино пиют, на дела же Господня не взирают и дел руку Его не помышляют.
Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao, matari, filimbi na mvinyo, lakini hawayajali matendo ya Bwana, wala hawana heshima kwa ajili ya kazi ya mikono yake.
13 Убо пленени быша людие мои, за еже не ведети им Господа, и множество бысть мертвых глада ради и жажди водныя.
Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ufahamu, watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa na watu wao wengi watakauka kwa kiu.
14 И разшири ад душу свою и разверзе уста своя, еже не престати: и снидут славнии и велицыи и богатии и губителие их и веселяйся в нем: (Sheol )
Kwa hiyo kaburi limeongeza hamu yake na kupanua mdomo wake bila kikomo, ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu, pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote. (Sheol )
15 и смирится человек, и обезчестится муж, и очи высокоглядающии смирятся.
Hivyo mwanadamu atashushwa, na binadamu kunyenyekezwa, macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.
16 И вознесется Господь Саваоф в суде, и Бог Святый прославится в правде:
Lakini Bwana Mwenye Nguvu Zote atatukuzwa kwa ajili ya haki yake, naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa haki yake.
17 и упасутся расхищеннии яко юнцы, и пустыни плененных агнцы поядят.
Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe, wana-kondoo watajilisha katika magofu ya matajiri.
18 Горе привлачающым грехи яко ужем долгим, и яко ига юнична ременем беззакония своя,
Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,
19 глаголющым: скоро да приближатся, яже сотворит, да видим, и да приидет совет Святаго Израилева, да разумеем.
kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka, aharakishe kazi yake ili tupate kuiona. Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike, tena udhihirike ili tupate kuujua.”
20 Горе глаголющым лукавое доброе, и доброе лукавое, полагающым тму свет, и свет тму, полагающым горькое сладкое, и сладкое горькое.
Ole wao wanaoita ubaya ni wema, na wema ni ubaya, wawekao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza, wawekao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu.
21 Горе, иже мудри в себе самих и пред собою разумни.
Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.
22 Горе крепким вашым, вино пиющым, и вельможам растворяющым сикер,
Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo, nao walio hodari katika kuchanganya vileo,
23 оправдающым нечестива даров ради, и еже есть праведное праведнаго вземлющым от него.
wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo, lakini huwanyima haki wasio na hatia.
24 Сего ради якоже сгорит трость от углия огненнаго и сожжется от пламене разгоревшагося, корень их яко персть будет, и цвет их яко прах взыдет: не восхотеша бо закона Господа Саваофа, но слово Святаго Израилева раздражиша.
Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi, na kama vile majani makavu yazamavyo katika miali ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza na maua yao yatakavyopeperushwa kama mavumbi; kwa kuwa wameikataa sheria ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na kulisukumia mbali neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.
25 И возярися гневом Господь Саваоф на люди Своя, и наложи руку Свою на них, и порази их: и раздражишася горы, и быша трупи их яко гной посреде пути. И во всех сих не отвратися ярость Его, но еще рука Его высока.
Kwa hiyo hasira ya Bwana inawaka dhidi ya watu wake, mkono wake umeinuliwa na anawapiga. Milima inatetemeka, maiti ni kama takataka kwenye barabara. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
26 Воздвигнет убо знамение во языцех сущих далече и позвиждет им от конец земли, и се, скоро легце грядут:
Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali, anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia. Tazama wamekuja, kwa kasi na kwa haraka!
27 не взалчут, ни утрудятся, ни воздремлют, ни поспят, ни распояшут поясов своих от чресл своих, ниже расторгнутся ремени сапогов их:
Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.
28 ихже стрелы остры суть, и луцы их напряжени: копыта коней их яко тверд камень вменишася, колеса колесниц их яко буря.
Mishale yao ni mikali, pinde zao zote zimevutwa, kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume, magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.
29 Ярятся яко львове, и предсташа яко львичища: и имет, и возопиет яко зверь, и извержет, и не будет отемлющаго их.
Ngurumo yao ni kama ile ya simba, wananguruma kama wana simba, wanakoroma wanapokamata mawindo yao, na kuondoka nayo pasipo yeyote wa kuokoa.
30 И возопиет их ради в той день, яко шум моря волнующася: и воззрят на землю, и се, тма жестока в недоумении их.
Katika siku ile watanguruma juu yake kama ngurumo za bahari. Kama mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki; hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.