< Книга пророка Исаии 26 >
1 В той день воспоют песнь сию в земли Иудейстей, глаголюще: се, град крепок, и спасение нам положит стену и ограждение.
Katika siku ile, wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda: Tuna mji ulio na nguvu, Mungu huufanya wokovu kuwa kuta zake na maboma yake.
2 Отверзите врата, да внидут людие хранящии правду и хранящии истину,
Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia, taifa lile lidumishalo imani.
3 приемлющии истину и хранящии мир.
Utamlinda katika amani kamilifu yeye ambaye moyo wake ni thabiti kwa sababu anakutumaini wewe.
4 Яко на тя надеянием надеяшася, Господи, во век, Боже великий, вечный,
Mtumaini Bwana milele, kwa kuwa Bwana, Bwana, ni Mwamba wa milele.
5 иже смирив низвел еси живущыя в высоких: грады крепкия разориши и обнизиши я даже до земли.
Huwashusha wale wajikwezao, huushusha chini mji wenye kiburi, huushusha hadi ardhini na kuutupa chini mavumbini.
6 И поперут я ноги кротких и смиренных.
Miguu huukanyaga chini, miguu ya hao walioonewa, hatua za hao maskini.
7 Путь благочестивых прав бысть, и приуготован путь благочестивых.
Mapito ya wenye haki yamenyooka. Ewe uliye Mwenye Haki, waisawazisha njia ya mtu mnyofu.
8 Путь бо Господень суд: уповахом на имя Твое и память, еяже желает душа наша.
Naam, Bwana, tukienenda katika sheria zako, twakungojea wewe, jina lako na sifa zako ndizo shauku za mioyo yetu.
9 От нощи утренюет дух мой к Тебе, Боже, зане свет повеления Твоя на земли: правде научитеся, живущии на земли.
Nafsi yangu yakutamani wakati wa usiku, wakati wa asubuhi roho yangu yakuonea shauku. Wakati hukumu zako zinapokuja juu ya dunia, watu wa ulimwengu hujifunza haki.
10 Преста бо нечестивый: всяк, иже не научится правде на земли, истины не сотворит: да возмется нечестивый, да не видит славы Господни.
Ingawa neema yaonyeshwa kwa waovu, hawajifunzi haki, hata katika nchi ya unyofu huendelea kutenda mabaya wala hawazingatii utukufu wa Bwana.
11 Господи, высока Твоя мышца, и не ведеша, разумевше же постыдятся: ревность приимет люди ненаказанныя, и ныне огнь супостаты пояст.
Ee Bwana, mkono wako umeinuliwa juu, lakini hawauoni. Wao na waone wivu wako kwa ajili ya watu wako tena waaibishwe, moto uliowekwa akiba kwa ajili ya adui zako na uwateketeze.
12 Господи Боже наш, мир даждь нам, вся бо воздал еси нам.
Bwana, unaamuru amani kwa ajili yetu, yale yote tuliyoweza kuyakamilisha ni wewe uliyetenda kwa ajili yetu.
13 Господи Боже наш, стяжи ны: Господи, разве Тебе иного не вемы: имя Твое именуем.
Ee Bwana, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametutawala, lakini jina lako pekee ndilo tunaloliheshimu.
14 Мертвии же живота не имут видети, ниже врачеве воскресят: сего ради навел еси и погубил еси, и взял еси всяк мужеск пол их.
Wao sasa wamekufa, wala hawako tena hai, roho za waliokufa hazitarudi tena. Uliwaadhibu na kuwaangamiza, umefuta kumbukumbu lao lote.
15 Приложи им зла, Господи, приложи зла славным земли.
Umeliongeza hilo taifa, Ee Bwana, umeliongeza hilo taifa. Umejipatia utukufu kwa ajili yako mwenyewe, umepanua mipaka yote ya nchi.
16 Господи, в скорби помянухом Тя, в скорби мале наказание Твое нам.
Bwana, walikujia katika taabu yao, wewe ulipowarudi, waliweza kuomba kwa kunongʼona tu.
17 И яко болящая приближается родити и в болезни своей воскрича, тако быхом возлюбленному Твоему.
Kama mwanamke mwenye mimba aliyekaribia kuzaa anavyogaagaa na kulia kwa ajili ya maumivu yake, ndivyo tulivyokuwa mbele zako, Ee Bwana.
18 Страха ради Твоего, Господи, во чреве прияхом и поболехом, и родихом дух спасения Твоего, егоже сотворихом на земли: не падемся, но падутся вси живущии на земли.
Tulikuwa na mimba, tuligaagaa kwa maumivu, lakini tulizaa upepo. Hatukuleta wokovu duniani, hatujazaa watu katika ulimwengu huu.
19 Воскреснут мертвии и востанут иже во гробех, и возрадуются иже на земли: роса бо, яже от Тебе, изцеление им есть, земля же нечестивых падет.
Lakini wafu wenu wataishi, nayo miili yao itafufuka. Ninyi mnaokaa katika mavumbi, amkeni mkapige kelele kwa furaha. Umande wenu ni kama umande wa asubuhi, dunia itawazaa wafu wake.
20 Идите, людие мои, внидите во храмину вашу, затворите двери своя, укрыйтеся мало елико елико, дондеже мимоидет гнев Господень.
Nendeni, watu wangu, ingieni vyumbani mwenu na mfunge milango nyuma yenu, jificheni kwa kitambo kidogo mpaka ghadhabu yake ipite.
21 Се бо, Господь от святаго (места) наводит гнев на живущыя на земли: и открыет земля кровь свою и не покрыет избиеных.
Tazama, Bwana anakuja kutoka makao yake ili kuwaadhibu watu wa dunia kwa ajili ya dhambi zao. Dunia itadhihirisha umwagaji damu juu yake, wala haitaendelea kuwaficha watu wake waliouawa.