< Книга пророка Исаии 23 >

1 Плачитеся, корабли Кархидонстии, яко погибе, и ктому не идут от земли Китиейския, отведеся пленен.
Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
2 Кому подобни быша живущии во острове, купцы Финичестии, преходящии море?
Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
3 В воде мнозе семя купеческо, аки жатве вносимей купцы язычестии.
Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
4 Усрамися, Сидоне, рече море. Крепость же морская рече: не болех, ни породих, ни вскормих юнош, ниже вознесох девиц.
Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
5 Егда же слышано будет во Египте, приимет я болезнь о Тире.
Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
6 Идите в Кархидон, плачитеся, живущии во острове сем.
Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
7 Не сие ли бе величание вам исперва, прежде неже предану быти ему?
Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
8 Кто сия совеща на Тира? Еда хуждший есть, или не крепкий есть? Купцы его славнии князи земли.
Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
9 Господь Саваоф совеща разсыпати всякую гордыню славных и обезчестити всякое славное на земли.
Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
10 Делай землю твою, ибо корабли ктому не приидут от Кархидона.
Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
11 И рука Твоя ктому не укрепеет по морю, разгневляющая царей. Господь Саваоф заповеда о Ханаане, еже погубити крепость его.
Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
12 И рекут: ктому не приложите укаряти и обидети дщерь Сидоню: и аще отидеши ко Китииом, ниже тамо будет тебе покой:
Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
13 и в землю Халдейску, но и та опустела от Ассириан, яко стена ея падеся.
Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
14 Плачитеся, корабли Кархидонстии, яко погибе твердыня ваша.
Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
15 И будет в той день, оставлен будет Тир седмьдесят лет, якоже время (единаго) царя, яко время человеческо: и по седмидесятих летех будет Тир яко песнь блудницы.
Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
16 Возми гусли, обыди град, блудница забвеная, добре погуди, много воспой, да память твоя будет.
“Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
17 И будет по седмидесятих летех, присещение сотворит Бог Тиру, и паки возставится на прежднее и будет торжище всем царствам вселенныя на лицы земли.
Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
18 И будет его купля и мзда свято Господеви, не им собрано будет, но живущым пред Господем, вся купля его, ясти и пити и наполнитися, и в сытость, на память пред Господем.
Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.

< Книга пророка Исаии 23 >