< Книга пророка Исаии 13 >

1 Видение на Вавилона, еже виде Исаиа сын Амосов.
Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:
2 На горе польней воздвигните знамение, вознесите глас им, не бойтеся, поущайте рукою, отверзите, князи.
Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu, wapazieni sauti, wapungieni mkono waingie katika malango ya wenye heshima.
3 Аз повелеваю, освященни суть: и Аз веду их, исполини идут исполнити ярость Мою радующеся, вкупе и укаряюще.
Nimewaamuru watakatifu wangu; nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu: wale wanaoshangilia ushindi wangu.
4 Глас языков многих на горах, подобен языков многих, глас царей и языков собравшихся: Господь Саваоф заповеда языку оружеборцу
Sikilizeni kelele juu ya milima, kama ile ya umati mkubwa wa watu! Sikilizeni, makelele katikati ya falme, kama mataifa yanayokusanyika pamoja! Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.
5 приити от земли издалеча, от края основания небесе, Господь и оружеборцы Его, растлити всю вселенную.
Wanakuja kutoka nchi za mbali sana, kutoka miisho ya mbingu, Bwana na silaha za ghadhabu yake, kuangamiza nchi yote.
6 Рыдайте: близ бо день Господень, и сокрушение от Бога приидет:
Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu, itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.
7 сего ради всяка рука разслабеет, и всяка душа человеча убоится,
Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea, moyo wa kila mtu utayeyuka.
8 и смятутся послы, и болезни приимут я яко жены раждающия: и поскорбят друг ко другу, и ужаснутся, и лице свое яко пламень изменят.
Hofu itawakamata, uchungu na maumivu makali yatawashika, watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa. Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake, nyuso zao zikiwaka kama moto.
9 Се бо, день Господень грядет неизцельный, ярости и гнева, положити вселенную (всю) пусту и грешники погубити от нея.
Tazameni, siku ya Bwana inakuja, siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali, kuifanya nchi kuwa ukiwa na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.
10 Звезды бо небесныя и орион и все украшение небесное света своего не дадят, и помрачится солнце возсиявающее, и луна не даст света своего.
Nyota za mbinguni na makundi ya nyota havitatoa mwanga wake. Jua linalochomoza litatiwa giza na mwezi hautatoa nuru yake.
11 И заповем всей вселенней злая и нечестивым грехи их, и погублю укоризну беззаконных и укоризну гордых смирю:
Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake, waovu kwa ajili ya dhambi zao. Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi, na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.
12 и будут оставшии честнии паче, нежели злато нежженое, и человек честен будет паче, нежели камень, иже от Суфира.
Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi, watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.
13 Разярится бо небо, и земля потрясется от оснований своих, за ярость гнева Господа Саваофа в день, в оньже приидет ярость Его.
Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke, nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika siku ya hasira yake iwakayo.
14 И будут оставшии яко серна бежащая и яко овца заблудившая, и не будет собираяй, яко человеку в люди своя возвратитися, и человек во страну свою побегнет.
Kama swala awindwaye, kama kondoo wasio na mchungaji, kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.
15 Иже бо аще пленится, поразится, и иже собрани суть, мечем падут.
Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo, wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.
16 И чада их пред ними разбиют, и домы их пленят, и жены их поймут.
Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande mbele ya macho yao; nyumba zao zitatekwa na wake zao watatendwa jeuri.
17 Се, Аз возбуждаю на вы Мидов, иже сребра не вменяют, ниже злата требуют:
Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao, ambao hawajali fedha wala hawafurahii dhahabu.
18 стреляния юношеская сокрушат, и чад ваших не помилуют, ниже пощадят чад твоих очи их.
Mishale yao itawaangusha vijana, hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga wala hawataangalia watoto kwa huruma.
19 И будет Вавилон, иже нарицается славный от царя Халдейска, якоже разсыпа Бог Содому и Гоморру,
Babeli, johari ya falme, utukufu wa kiburi cha Wababeli, itaangushwa na Mungu kama Sodoma na Gomora.
20 не населится в вечное время, и не внидут в онь чрез многия роды, ниже пройдут его Аравляне, ниже пастуси почиют в нем.
Hautakaliwa na watu kamwe wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko, hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.
21 И почиют тамо зверие, и наполнятся домове шума, и почиют ту сирини, и беси тамо воспляшут,
Lakini viumbe wa jangwani watalala huko, mbweha watajaza nyumba zake, bundi wataishi humo nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.
22 и онокентавры тамо вселятся, и вогнездятся ежеве в домех их.
Fisi watalia ndani ya ngome zake, mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari. Wakati wake umewadia, na siku zake hazitaongezwa.

< Книга пророка Исаии 13 >