< Книга пророка Осии 1 >

1 Слово Господне, еже бысть ко Осии сыну Веириину, во днех Озии и Иоафама, и Ахаза и Иезекии царей Иудиных, и во дни Иеровоама сына Иоасова царя Израилева.
Neno la Bwana lililomjia Hosea mwana wa Beeri wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na wakati wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi, mfalme wa Israeli.
2 Начало словесе Господня ко Осии. И рече Господь ко Осии: иди, поими себе жену блужения, (и роди) чада блужения: понеже блудящи соблудит земля от Господа.
Wakati Bwana alipoanza kuzungumza kupitia Hosea, Bwana alimwambia, “Nenda ukajitwalie mwanamke wa uzinzi na watoto wa uzinzi, kwa sababu nchi ina hatia ya uzinzi wa kupindukia kwa kumwacha Bwana.”
3 И иде и поя Гомерь дщерь Девилаимлю: и зачат и роди ему сына.
Kwa hiyo alimwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba na kumzalia Hosea mwana.
4 И рече Господь к нему: прозови имя ему Иезраель: зане еще мало, и отмщу кровь Иезраелеву на дому Иудове и упокою царство дому Израилева:
Kisha Bwana akamwambia Hosea, “Mwite Yezreeli, kwa kuwa kitambo kidogo nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa ajili ya mauaji ya kule Yezreeli, nami nitaukomesha ufalme wa Israeli.
5 и будет в той день, сокрушу лук Израилев во удоле Иезраелеве.
Katika siku ile nitavunja upinde wa Israeli katika Bonde la Yezreeli.”
6 И зачат еще и роди дщерь. И рече ему (Господь): прозови имя ей Непомилована: зане не приложу ксему помиловати дому Израилева, но противляяся возсопротивлюся им:
Gomeri akachukua tena mimba akamzaa binti. Kisha Bwana akamwambia Hosea, “Mwite Lo-Ruhama, kwa maana sitaonyesha tena upendo kwa nyumba ya Israeli, kwamba nisije kabisa nikawasamehe.
7 сыны же Иудины помилую и спасу я о Где Бозе их: и не спасу их луком, ни мечем, ни бранию, ни коньми, ниже конниками.
Hata hivyo nitaonyesha upendo kwa nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa si kwa upinde, upanga au vita, wala kwa farasi na wapanda farasi, bali kwa njia ya Bwana Mungu wao.”
8 И отдои Непомилованную: и зачат паки и роди сына.
Baada ya Gomeri kumwachisha Lo-Ruhama kunyonya, Gomeri alipata mwana mwingine.
9 И рече (Господь): прозови имя ему Не Людие Мои: зане вы не людие Мои, и Аз несмь Бог ваш:
Kisha Bwana akasema, “Mwite Lo-Ami kwa maana ninyi si watu wangu, nami si Mungu wenu.
10 и будет число сынов Израилевых аки песок морский, иже не измерится, ни изочтется: и будет, на месте, на немже речеся им: не людие Мои вы: сии тамо прозовутся сынове Бога живаго.
“Hata hivyo Waisraeli watakuwa kama mchanga kando ya bahari, ambao hauwezi kupimika wala kuhesabiwa. Mahali pale walipoambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’
11 И соберутся сынове Иудины и сынове Израилевы вкупе, и поставят себе власть едину, и изыдут от земли, яко велик день Иезраелев.
Watu wa Yuda na watu wa Israeli wataunganishwa tena, nao watamchagua kiongozi mmoja nao watakwea watoke katika nchi, kwa kuwa siku ya Yezreeli itakuwa kuu sana.

< Книга пророка Осии 1 >