< Бытие 8 >
1 И помяну Бог Ноа, и вся звери, и вся скоты, и вся птицы, и вся гады пресмыкающыяся, елика беху с ним в ковчезе: и наведе Бог дух на землю, и преста вода.
Mungu akamtazama Nuhu, wanyama wote wa mwitu, na wanyama wote wa kufugwa ambao walikuwa pamoja naye kwenye safina. Mungu akafanya upepo uvume juu ya nchi, na maji yakaanza kuzama chini.
2 И заключишася источницы бездны и хляби небесныя: и удержася дождь от небесе.
Chemichemi za vilindi pamoja na madirisha ya mbingu vikafungwa, na mvua ikakoma kunyesha.
3 И вспять пойде вода идущая от земли: и умаляшеся вода по сте пятидесятих днех.
Maji ya gharika yakaanza kuzama kidogo kidogo katika nchi. na mwisho wa siku miamoja na hamsini maji yakawa yamezama chini.
4 И седе ковчег в месяц седмый, в двадесять седмый день месяца, на горах Араратских.
safina ikatulia katika mwezi wa saba, siku ya kumi na saba ya mwezi, juu ya milima ya Ararati.
5 Вода же уходящи умаляшеся даже до десятаго месяца: и в десятый месяц, в первый день месяца явишася верси гор.
Maji yakaendelea kuzama chini hadi mwezi wa kumi. Siku ya kwanza ya mwezi, vilele vya milima vikaonekana.
6 И бысть до четыредесятих днех отверзе Ное оконце ковчега, еже сотвори,
Ikatokea kwamba baada ya siku arobaini Nuhu alifungua dirisha la safina ambayo aliitengeneza.
7 и посла врана (видети, аще уступила вода от лица земли): и изшед не возвратися, дондеже изсяче вода от земли.
Akatuma kunguru na akaruka hadi maji yalipo kauka katika nchi.
8 И посла голубицу по нем видети, аще уступила вода от лица земли:
Kisha akatuma njiwa kuona kama maji yamezama chini kutoka kwenye uso wa nchi,
9 и не обретши голубица покоя ногама своима, возвратися к нему в ковчег, яко вода бяше по всему лицу всея земли: и простер руку свою, прият ю и внесе ю к себе в ковчег.
lakini njiwa hakuona sehemu ya kutua unyayo wake, na akarudi kwake ndani ya safina, kwa kuwa maji yalikuwa bado yamefunika nchi yote. Akanyoosha mkono wake, akamchukua na kumuweka ndani ya safina pamoja naye.
10 И премедлив еще седмь дний, паки посла голубицу из ковчега.
Akasubiri siku saba zingine akatuma tena njiwa kutoka kwenye safina.
11 И возвратися к нему голубица к вечеру, и имеяше сучец масличен с листвием во устех своих: и позна Ное, яко уступи вода от лица земли.
Njiwa akarudi kwake jioni. Tazama! katika mdomo wake kulikuwa na jani bichi la mzeituni lililochumwa. Kwa hiyo Nuhu akatambua kuwa maji yamekwisha zama chini ya nchi.
12 И премедлив еще седмь дний других, паки посла голубицу, и не приложи возвратитися к нему потом.
Akasubiri siku saba zingine na akamtuma njiwa tena. Njiwa hakurudi kwake tena.
13 И бысть в первое и шестьсотное лето жития Ноева, в первый день перваго месяца, изсяче вода от лица земли: и откры Ное покров ковчега, егоже сотвори, и виде, яко изсяче вода от лица земли.
Ikawa kwamba katika mwaka wa mia sita na moja, katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, maji yalikuwa yamekauka katika nchi. Nuhu akaondoa kifuniko cha safina, akatazama nje, na akaona kwamba, Tazama, uso wa nchi ulikuwa umekauka.
14 В месяц же вторый, в двадесять седмый день месяца изсше земля.
Katika mwezi wa pili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, nchi ilikuwa imekauka.
15 И рече Господь Бог Ноеви, глаголя:
Mungu akamwambia Nuhu,
16 изыди из ковчега ты и жена твоя, и сынове твои и жены сынов твоих с тобою:
“Toka nje ya safina, wewe, mke wako, wanao wa kiume, na wake wa wanao pamoja nawe.
17 и вся звери, елицы суть с тобою, и всяку плоть от птиц даже до скотов, и всяк гад движущийся по земли изведи с собою: и раститеся и множитеся на земли.
Wachukuwe utoke nje pamoja nao kila kiumbe hai chenye mwili ambacho kiko nawe - ndege, wanyama wa kufugwa, na kila kitambaacho ambacho hutambaa juu ya nchi - ili kwamba viweze kukua na kuwa na idadi kubwa zaidi ya viumbe hai katika nchi yote, kwa kuzaliana na kuongezeka juu ya nchi.”
18 И изыде Ное и жена его, и сынове его и жены сынов его с ним,
Kwa hiyo Nuhu akatoka nje pamoja na watoto wake wa kiume, mke wake, na wake wa wa wanawe pamoja naye.
19 и вси зверие, и вси скоти, и вся птицы и вси гади движущиися по роду своему на земли изыдоша из ковчега.
Kila kiumbe hai, kila kitambaacho, na kila ndege, na kila kiendacho juu ya nchi, kwa kabila zao, wakaiacha safina.
20 И созда Ное жертвенник Господеви: и взя от всех скотов чистых и от всех птиц чистых и вознесе во всесожжение на жертвенник.
Nuhu akajenga madhabahu kwa Yahwe. Akachukua baadhi ya wanyama walio safi na baadhi ya ndege walio safi, na kutoa sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
21 И обоня Господь воню благоухания. И рече Господь Бог размыслив: не приложу ктому прокляти землю за дела человеческая, зане прилежит помышление человеку прилежно на злая от юности его: не приложу убо ктому поразити всякую плоть живущую, якоже сотворих:
Yahwe akanusa harufu nzuri ya kuridhisha na akasema moyoni mwake, “Sita laani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, ingawa nia za mioyo yao ni mbaya tokea utoto. Wala sita haribu kilakitu chenye uhai, kama nilivyo fanya.
22 во вся дни земли сеятва и жатва, зима и зной, лето и весна, день и нощь не престанут.
Wakati nchi isaliapo, majira ya kupanda mbegu na mavuno, baridi na joto, kiangazi na majira ya baridi, mchana na usiku havitakoma.”