< Бытие 4 >
1 Адам же позна Еву жену свою, и заченши роди Каина и рече: стяжах человека Богом.
Adamu akakutana kimwili na mkewe Eva, naye akapata mimba, akamzaa Kaini. Eva akasema, “Kwa msaada wa Bwana nimemzaa mwanaume.”
2 И приложи родити брата его, Авеля. И бысть Авель пастырь овец, Каин же бе делаяй землю.
Baadaye akamzaa Abeli ndugu yake. Basi Abeli akawa mfugaji, na Kaini akawa mkulima.
3 И бысть по днех, принесе Каин от плодов земли жертву Богу:
Baada ya muda Kaini akaleta baadhi ya mazao ya shamba kama sadaka kwa Bwana.
4 и Авель принесе и той от первородных овец своих и от туков их. И призре Бог на Авеля и на дары его:
Lakini Abeli akaleta fungu nono kutoka baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake. Bwana akamkubali Abeli pamoja na sadaka yake,
5 на Каина же и на жертвы его не внят. И опечалися Каин зело, и испаде лице его.
lakini Mungu hakumkubali Kaini pamoja na sadaka yake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana, uso wake ukawa na huzuni.
6 И рече Господь Бог Каину: вскую прискорбен был еси? И вскую испаде лице твое?
Kisha Bwana akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika? Kwa nini uso wako una huzuni?
7 Еда аще право принесл еси, право же не разделил еси, не согрешил ли еси? Умолкни: к тебе обращение его, и ты тем обладаеши.
Ukifanya lililo sawa, je, hutakubalika? Lakini usipofanya lililo sawa, dhambi inakuvizia mlangoni mwako, inakutamani wewe, lakini inakupasa uishinde.”
8 И рече Каин ко Авелю брату своему: пойдем на поле. И бысть внегда быти им на поли, воста Каин на Авеля брата своего и уби его.
Basi Kaini akamwambia ndugu yake Abeli, “Twende shambani.” Walipokuwa shambani, Kaini akamshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.
9 И рече Господь Бог ко Каину: где есть Авель брат твой? И рече: не вем: еда страж брату моему есмь аз?
Kisha Bwana akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Abeli yuko wapi?” Akamjibu, “Sijui, je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
10 И рече Господь: что сотворил еси сие? Глас крове брата твоего вопиет ко Мне от земли:
Bwana akasema, “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kutoka ardhini.
11 и ныне проклят ты на земли, яже разверзе уста своя прияти кровь брата твоего от руки твоея:
Sasa umelaaniwa na umehamishwa kutoka ardhi, ambayo imefungua kinywa chake na kupokea damu ya ndugu yako kutoka mkononi mwako.
12 егда делаеши землю, и не приложит силы своея дати тебе: стеня и трясыйся будеши на земли.
Utakapoilima ardhi, haitakupa tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga duniani asiye na utulivu.”
13 И рече Каин ко Господу Богу: вящшая вина моя, еже оставитися ми:
Kaini akamwambia Bwana, “Adhabu yangu ni zaidi ya niwezavyo kustahimili.
14 аще изгониши мя днесь от лица земли, и от лица Твоего скрыюся, и буду стеня и трясыйся на земли, и будет, всяк обретаяй мя убиет мя.
Leo unanifukuza kutoka nchi, nami nitafichwa mbali na uwepo wako. Nitakuwa mtu wa kutangatanga asiyetulia duniani na yeyote anionaye ataniua.”
15 И рече ему Господь Бог: не тако: всяк убивый Каина седмижды отмстится. И положи Господь Бог знамение на Каине, еже не убити его всякому обретающему его.
Lakini Bwana akamwambia, “La sivyo, ikiwa mtu yeyote atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba zaidi.” Kisha Bwana akamwekea Kaini alama ili mtu yeyote ambaye angemwona asimuue.
16 И изыде Каин от лица Божия и вселися в землю Наид, прямо Едему.
Kwa hiyo Kaini akaondoka mbele za Bwana akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, iliyoko mashariki ya Edeni.
17 И позна Каин жену свою, и заченши роди Еноха. И бе зиждяй град, и именова град во имя сына своего Енох.
Kaini akakutana kimwili na mkewe, naye akapata mimba na akamzaa Enoki. Wakati huo Kaini alikuwa anajenga mji, akauita Enoki jina la mtoto wake.
18 Родися же Еноху Гаидад: и Гаидад роди Малелеила: и Малелеил роди Мафусала: Мафусал же роди Ламеха.
Enoki akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli, Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, na Methushaeli akamzaa Lameki.
19 И взя себе Ламех две жены: имя единей Ада и имя вторей Селла.
Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada, na mwingine Sila.
20 И роди Ада Иовила: сей бяше отец живущих в селениих скотопитателей.
Ada akamzaa Yabali ambaye ni baba wa wale walioishi katika mahema na kufuga wanyama.
21 И имя брату его Иувал: сей бяше показавый певницу и гусли.
Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi.
22 Селла же и тая роди Фовела: сей бяше млатобиец, ковачь меди и железа: сестра же Фовелова Ноема.
Pia Sila alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Tubali-Kaini ambaye alifua vifaa vya aina mbalimbali vya shaba na chuma. Naama alikuwa dada wa Tubali-Kaini.
23 Рече же Ламех своим женам: Ада и Селла, услышите глас мой, жены Ламеховы, внушите моя словеса: яко мужа убих в язву мне и юношу в струп мне:
Lameki akawaambia wake zake, “Ada na Sila nisikilizeni mimi; wake wa Lameki sikieni maneno yangu. Nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana mdogo kwa kuniumiza.
24 яко седмицею отмстися от Каина, от Ламеха же седмьдесят седмицею.
Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba, basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”
25 Позна же Адам Еву жену свою: и заченши роди сына, и именова имя ему Сиф, глаголющи: воскреси бо ми Бог семя другое, вместо Авеля, егоже уби Каин.
Adamu akakutana kimwili na mke wake tena, akamzaa mwana, akamwita Sethi, akisema, “Mungu amenijalia mwana mwingine badala ya Abeli, kwa kuwa Kaini alimuua.”
26 И Сифу бысть сын: именова же имя ему Енос: сей упова призывати имя Господа Бога.
Naye Sethi akamzaa mwana, akamwita Enoshi. Wakati huo watu wakaanza kuliitia jina la Bwana.