< Книга пророка Иезекииля 40 >
1 И бысть во двадесять пятое лето пленения нашего, перваго месяца, в десятый день месяца, в четвертоенадесять лето но пленении града, в той день бысть на мне рука Господня: и веде мя тамо,
Katika mwaka wa ishirini na tano wa kuhamishwa kwetu mwanzoni mwa mwaka siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya mji kuchukuliwa-katika siku hiyo hiyo, mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu na alinichukua huko.
2 в видении Божии веде мя на землю Израилеву и постави мя на горе высоце зело, на нейже яко сограждение града прямо (полудне),
Katika maono ya Mungu akanileta hata nchi ya Israeli. Akanileta kupumzika juu ya kila mlima mrefu sana; upande wa kusini kulikuwa na monekano kana kwamba majengo ya mji.
3 и введе мя тамо: и се, муж, и зрак его бяше, яко видение меди блещащияся, и в руце его бяше вервь зиждущих и трость мерителная. Той же стояше у врат
Kisha akanileta huko. Tazama, kulikuwa na mtu! Mwonekano wake ulikuwa kama mwonekano wa shaba. Alikuwa na uzi wa kitani na mwanzi wa kupimia mkononi mwake, na alisimama katika lango la mji.
4 и рече ко мне: видел ли еси, сыне человечь? Виждь очима твоима и ушима твоима слыши, и учини в сердцы твоем вся, елика аз показую тебе, зане того ради вшел еси семо, да покажу тебе, и покажеши ты вся, елика видиши, дому Израилеву.
Huyo mtu akanambia, “Mwanadamu, tazama kwa macho yako na sikiliza kwa masikio yako, na elekeza moyo wako juu ya yote ninayokufunulia, kwa kuwa ulinileta hapa ili niweze kukufunulia haya wewe. Toa taarifa ya kila kitu utakachokiona kwa nyumba ya Israeli.
5 И се, ограда внеуду окрест храма, и в руце мужа мера тростяна шести лакот в лакоть шестодланный, и измери предстение ширину равно трости, и высоту его равно трости.
Kulikuwa ukuta uliokuwa umezunguka eneo la hekalu. Urefu wa kipimo cha mwanzi katika mkono wa mtu ulikuwa dhiraa sita urefu, kila urefu wa dhiraa ulikuwa dhiraa moja na kipimo cha kiganja cha mkono urefu. Aliupima ukuta; ulikuwa kipimo cha mwanzi mmoja na ufito mmoja urefu.
6 И вниде во врата зрящая на восток седмию степеньми, и измери фее, шесть о сию страну, шесть же об ону, и елам дверный равно трости.
Kisha akaenda hata kwenye lango la hekalu lililokuwa limeelekea mashariki. Akapanda ngazi na kuipima kizingiti cha lango-mwanzi mmoja upana.
7 И фее равно трости в долготу и равно трости в широту, и аилам среде феилаф шести лакот. И фее второе равно трости в широту и равно трости в долготу, елам же пяти лакот.
Vyumba vya ulinzi vilikuwa kila mwanzi mmoja urefu na mwanzi mmoja upana; kulikuwa na dhiraa tano katika kila vyumba viwili, na kizingiti cha lango la hekalu karibu na tawa la hekalu kilikuwa mwanzi mmoja urefu.
8 И фее третие равно трости в долготу и равно трости в широту,
Akapima tawa la lango; ulikuwa mwanzi mmoja urefu.
9 елам же вратный, иже близ елама двернаго осми лакот, аилев же двою лактей: и елам дверный внутрьуду.
Akapima tawa la lango. Ilikuwa mwanzi mmoja kwenda chini. Mihimili ilikuwa dhiraa mbili upana. Hili lilikuwa tawa la lango kuelekea hekalu.
10 И фее дверныя прямо фее, три о сию страну и три об ону, мера же едина трием: и мера едина аилам сюду и сюду.
Kulikuwa na vyumba vitatu vya ulinzi pande zote za lango la mashariki, na yote yalikuwa na kipimo kile kile, na kuta zilizokuwa zimezigawanya zilikuwa na kipimo kile kile.
11 И размери широту входа вратнаго десяти лактей, широту же вратную тринадесяти лактей,
Kisha yule mtu akapima upana wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi; na akapima urefu wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi na tatu.
12 и лакоть един сводимь прямо фееим лактя единаго и лактя единаго, предел сюду и сюду, и фее шести лактей о сию страну и шести лактей об ону страну.
Akaupima ukuta uliokuwa mpaka mbele ya vyumba-dhiraa moja urefu. Vyumba vilipimwa dhiraa sita kila upande.
13 И размери врата от стены фее до стены фее, широта двадесяти и пяти лактей: сия врата ко вратом,
Kisha akapima lango la njia kutoka kwenye paa ya chumba kimoja kuelekea chumba kingine-dhiraa ishirini na tano, kutoka lango la kuingia chumba cha kwanza kuelekea kile cha pili.
14 и непокровенное елама врат шестидесяти лактей, (двадесяти пяти) и фее двора окрест,
Kisha akapima ukuta uliokuwa umeenda kati ya vyumba vya ulinzi-dhiraa sitini urefu; alipima kwa mbali na tawa la lango.
15 и непокровенное врат отвне в непокровенное (врат) елама врат внутрьуду пятьдесят лактей.
Lango la kuingia kutoka lango la mbele kuelekea lango jingine la tawa la mwisho lilikuwa dhiraa hamsini.
16 И оконца сокровена фееим и в аилам внутрь врат двора окрест: такожде и елам оконца внутрьуду окрест, и на аилам финики сюду и сюду (изваяны).
Kulikuwa na madirisha yaliyokuwa yamefungwa kuelekea vyumba na kuelekea nguzo zake kati ya malango kuzunguka kote; na vivyo hivyo kwa mabaraza. Kulikuwa na madirisha pande zote za ndani, na kila mhimili ulikuwa umepambwa kwa mitende.
17 И введе мя во двор внутренний, и се, преграждения и междустолпия окрест двора, преграждений же тридесять в междустолпиих,
Kisha huyo mtu akanileta hata ua wa nje mwa hekalu. Tazama, kulikuwa na vyumba, na kulikuwa na kibamba katika ua, pamoja na vyumba thelathini baada ya kibamba.
18 и притворы противу задней стране врат, по долготе врат междустолпие нижнее.
Kibamba kilienda juu hata upande wa malango, na upana wake ulikuwa sawsawa na urefu wa malango. Hiki kilikuwa kibamba cha chini.
19 И размери широту двора от непокровенаго врат внешних внутрь ко непокровеному врат зрящих вне, лактей сто зрящих на восток: и введе мя на север,
Kisha huyo mtu akapima umbali kutoka mebele ya lango la chini hata mbele ya lango la ndani; ilikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki, na sawasawa na upande wa kaskazini.
20 и се, врата зрящая на север двору внешнему, и размери я, долготу их и широту.
Kisha akapima urefu na upana wa lango lililokuwa upande wa kaskazini mwa ua wa nje.
21 И фее три о сию страну, три же об ону, и аилев, и еламы, и финики их: и бысть по мере врат зрящих на восток, пятидесяти лактей долгота их, а широта их двудесяти и пяти лактей:
Kulikuwa na vyumba vitatu pande zote za lango, na lango na matawa yake yalipimwa sawa na lango kubwa-dhiraa hamsini upana wote na dhiraa ishirini na tano upana.
22 и оконца их, и еламы, и финики их, якоже врата зрящая на восток: и седмию восходами восхождаху на ня, и еламы внутрьуду.
Madirisha yake, tawa, vyumba, na mitende yake vilikabiliana na lango ambalo linaloelekea mashariki. Ngazi saba kuupandia juu hata kwenye tawa lake.
23 И врата двору внутреннему зрящая ко вратом северным, якоже врата зрящая на восток: и размери двор от врат до врат лактей сто.
Kulikuwa na lango kwenye ua wa ndani mbele kuelekea mashariki; huyo mtu alipima kutoka lango moja hadi lango jingine-dhiraa mia moja umbali.
24 И веде мя к югу, и се, врата зрящая на юг, и размери я, и фее, и аилева, и еламы, по темжде мерам.
Kisha huyo mtu akanileta hata kwenye lango la kuingia la kusini, na kuta zake na tawa vilipimwa sawa kama malango mengine ya nje.
25 И оконца их и еламы окрест якоже и оконца елаг, пятидесяти лактей долгота их, а широта двудесяти и пяти лактей,
Kulikuwa na madirisha yaliyofungwa katika lango la njia na tawa lake kama lile lango. Lango la kusini na tawa lake vilipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
26 и седмь восходов им, и еламы внутрьуду, и финики их, един о сию страну, а другий об ону над аилев.
Kulikuwa na ngazi saba hadi kwenye lango na matawa yake, na kulikuwa na mitende iliyochongoka juu ya kuta pande zote.
27 И врата прямо вратом двора внутренняго на юг: и размери двор от врат до врат на юг, сто лактей в широту.
Kulikuwa na lango la ua wa ndani upande wa kusini, na yule mtu akapima kutoka hilo lango hata lango la kuingia upande wa kusini-dhiraa mia moja umbali.
28 И введе мя во двор внутренний врат, яже на юг, и размери врата, яже на юг, по темжде мерам:
Kishi huyo mtu akanileta hata ua wa ndani karibu na lango lake la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo vile vile kama malango mengine.
29 и фее, и аилев, и еламы по темжде мерам.
Vyumba vyake, kuta, na matao vilipimwa sawa kama malango mengine; kulikuwa na madirisha kuzunguka matao yote. Lango la ndani na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
30 И оконца их и еламы окрест, пятидесяти лактей долгота их, а широта двудесяти и пяти лактей.
Pia kulikuwa na matao pande zote za kuta za ndani; haya yalikuwa dhiraa ishirini na tano urefu na dhiraa tano upana.
31 Еламы же во двор внешний, и финики аилев, и осмь восходов.
Hili tawa lilielekea ua wa nje pamoja na mitende iliyochongwa juu ya kuta zake na ngazi nane kuupandia.
32 И введе мя во врата зрящая на восток, и размери я по темжде мерам, и фее и аилев и еламы по темжде мерам.
Kisha yule mtu akanileta hata kwenye ua wa ndani karibu na njia ya kaskazini na kulipima lango, ambalo lilikuwa na vipimo sawa kama malango mengine.
33 И оконца им, и еламы и окрест, пятидесяти лактей долгота их, а широта их двудесяти и пяти лактей.
Vyumba vyake, kuta, na matawa yalikuwa na kipima sawa kama cha malango, na kulikuwa na madirisha pande zote. Laango la ndani na matawa yake yalikuwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
34 И еламы во двор внутренний, и финики на аилев сюду и сюду, и осмь восходов им.
Matawa yake yalielekea nje ya ua; ilikuwa na mitende pande zote za hiyo na ngazi nane za kuupandia.
35 И введе мя во врата яже на север, и размери по темжде мерам,
Kisha huyo mtu akanileta hata lango la kaskazini na kulipima; likapimwa vivyo hivyo kama malango mengine.
36 и фее и аилев и еламы, и оконца им окрест, пятидесяти лактей долгота их, а широта двудесяти и пяти лактей,
Vyumba vyake, kuta, na ukumbi vilipimwa sawa na malango mengine, na kulikuwa na madirisha pande zote. Njia ya lango na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na upana dhiraa ishirini na tano.
37 и еламы во внешний двор, и финики аилеву сюду и сюду, и осмь восходов им.
Tatawa lake lilielekea ua wa nje; ilikuwa na mitende pande zote za huo na ngazi nane kuupandia.
38 И преграды их, и двери их, и еламы их пред враты их вторыми сток, тамо измывают всесожжения.
Kulikuwa na chumba pamoja na mlango karibu na kila lango la ndani. Hapa ndipo ambako walipooshea sadaka za kutekezwa.
39 Во еламе же врат, две трапезы о сию страну, две же об ону, еже закалати на них всесожжения, яже за грехи и яже за неведение.
Kulikuwa na meza mbili kila upande wa kila ukumbi, ambako sadaka ya kuteketezwa ilipochinjiwa, na pia sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
40 И созади стока всесожжений дверий зрящих на север две трапезы на восток противу задней стране (дверий) вторых, и противу елама врат две трапезы на восток.
Karibu na ukuta wa ua, kuelekea juu kwenye lango kuelekea kaskazini, kulikuwa na meza mbili. Pia kwa upande mwingine kulikuwa na meza mbili kwenye lango la ukumbi.
41 Четыри о сию страну, четыри же об ону противу задней стране врат, на тех закалают заколения: прямо осми трапез заколений:
Kulikuwa na meza nne pande zote karibu na lango; wakachinja wanyama juu ya meza nane.
42 четыри же трапезы всесожжений каменны истесаны, в широту лактя единаго и пол, в долготу двух лактей и пол, а в высоту лакоть един: на тыя возлагают орудия, имиже закалают тамо всесожжения и заколения.
Kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, dhiraa moja na nusu urefu, dhiraa moja na nusu upana, na kimo dhiraa moja. Juu yake waliweka vyombo pamoja ambavyo walivichinjia sadaka za kuteketezwa kwa ajili ya sadaka.
43 И имеют ограждение мало истесано на длань внутрьуду окрест, верху же трапезы покров, еже покрыватися им от дождя и зноя.
Kulabu mbili ujazo wa kiganja urefu uliokuwa umeunganishwa katika ua pande zote, na nyama ya matoleo ilikuwa imewekwa juu ya meza.
44 И введе мя во двор внутреннейший, и се, две преграды во внутреннейшем дворе, едина противу задней стране врат зрящих на север, вводящая на юг, а другая противу задней стране врат сущих на юг, зрящих же к северу.
Karibu na lango la ndani, katika ua wa ndani, kulikuwa na vyumba vya waimbaji. Moja ya hivi vyumba kilikuwa upande wa kaskazini, na kingine kusini.
45 И рече ко мне: преграда сия, яже зрит на юг, жерцем есть, иже стрегут стражбу храма:
Kisha yule mtu akanambia, “Hiki chumba kinachoelekea kusini ni kwa ajili ya makuhani walio zamu katika hekalu.
46 а преграда, яже зрит к северу, жерцем есть стрегущым стражу требника: тии суть сынове Садуковы, приступающии от Левиа ко Господеви, еже служити Ему.
Chumba kilichoelekea kaskazini kilikuwa kwa ajili ya makuhani waliokuwa zamu kwenye madhabahu. Hawa ni wana wa Sadoki ambaye huja humkaribia Yahwe kumtumikia; ambao ni miongoni mwa wana wa Lawi.”
47 И размери двор ста лактей в долготу и в широту ста лактей, на четыри страны его, и требник прямо храму.
Kisha akaupima ule ua-dhiraa mia moja urefu na dhiraa mia moja upana mraba, pamoja na madhabahu mbele ya nyumba.
48 И введе мя во елам храма: и размери аил елама пяти лактей широту о сию страну, пяти же лактей об ону, широта же дверная четырехнадесяти лактей, и бока дверная елама три лакти о сию страну, три же об ону.
Kisha yule mtu akanileta hata kwenye varanda ya nyumba na kupima mwimo wa milango yake-ilikuwa dhiraa tano unene upande huu. Njia ya kuingilia yenyewe ilikuwa dhiraa kumi na nne, na kuta pande zote za huo zilikuwa dhraa tatu upana.
49 Долгота же елама двадесять лактей, а широта дванадесять лактей: и десятию степеньми восхождаху к нему, и столпи бяху у аилама, един о сию страну, а другий об ону.
Urefu wa ukumbi ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa kumi na moja. Kulikuwa na ngazi zilizokuwa zimepanda juu na nguzo zilizokuwa zimesimama pande zote za huo.