< Книга Екклезиаста 2 >
1 Рекох аз в сердцы моем: прииди убо, да тя искушу в веселии, и виждь во блазе: и се, такожде сие суетство.
Nikafikiri moyoni mwangu, “Haya basi, nitakujaribu kwa anasa nione ni lipi lililo jema.” Lakini hilo nalo likaonekana ni ubatili.
2 Смеху рекох: погрешение, и веселию: что сие твориши?
Nikasema, “Kicheko nacho ni upumbavu. Nayo matokeo ya anasa ni nini?”
3 И разсмотрих, аще сердце мое повлечет аки вино плоть мою: и сердце мое настави мя в мудрости, и еже удержати веселие, дондеже увижду, кое благо сыном человеческим, еже творят под солнцем в число дний живота своего.
Nikajaribu kujifurahisha kwa mvinyo na kukumbatia upumbavu, huku bado akili yangu inaniongoza kwa hekima. Nilitaka kuona ni lipi bora watu wafanye kwa siku chache wanazoishi chini ya mbingu.
4 Возвеличих творение мое: создах ми домы, насадих ми винограды,
Nikafanya miradi mikubwa: Nikajijengea majumba na kulima mashamba ya mizabibu.
5 сотворих ми вертограды и сады и насадих в них древес всякаго плода,
Nikatengeneza bustani na viwanja vya starehe nikaotesha huko kila aina ya miti ya matunda.
6 сотворих ми купели водныя, еже напаяти от них прозябение древес:
Nikajenga mabwawa ya kukusanya maji ya kunyweshea hii miti iliyokuwa inastawi vizuri.
7 притяжах рабы и рабыни, и домочадцы быша ми: и стяжание скота, и стад много ми бысть, паче всех бывших прежде мене во Иерусалиме:
Nikanunua watumwa wa kiume na wa kike na watumwa wengine walizaliwa nyumbani mwangu. Pia nilikuwa na makundi ya ngʼombe, kondoo na mbuzi kuliko mtu yeyote aliyewahi kuishi Yerusalemu kabla yangu.
8 собрах ми злато и сребро и имения царей и стран, сотворих ми поющих и поющыя, и услаждения сынов человеческих, виночерпцы и виночерпицы.
Nikajikusanyia fedha na dhahabu, hazina za wafalme na za majimbo. Nikajipatia waimbaji wanaume na wanawake, nazo nyumba za masuria: vitu ambavyo moyo wa mwanadamu hufurahia.
9 И возвеличихся, и приложихся мудрости паче всех бывших прежде мене во Иерусалиме: и мудрость моя пребысть со мною.
Nikawa maarufu sana kuliko mtu mwingine yeyote aliyepata kuishi Yerusalemu kabla yangu. Katika haya yote bado nikawa nina hekima.
10 И все, егоже просиста очи мои, не отях от них и не возбраних сердцу моему от всякаго веселия моего, яко сердце мое возвеселися во всяцем труде моем. И сие бысть часть моя от всего труда моего.
Sikujinyima kitu chochote ambacho macho yangu yalikitamani, hakuna anasa ambayo niliunyima moyo wangu. Moyo wangu ulifurahia kazi zangu zote, hii ilikuwa thawabu ya kazi zangu zote.
11 И призрех аз на вся творения моя, яже сотвористе руце мои, и на труд, имже трудихся творити. И се, вся суета и произволение духа, и несть изюбилие под солнцем.
Hata hivyo nilipokuja kuangalia yote ambayo mikono yangu ilikuwa imefanya na yale niliyotaabika kukamilisha, kila kitu kilikuwa ni ubatili, ni kukimbiza upepo; hapakuwa na faida yoyote chini ya jua.
12 И призрех аз видети мудрость, лесть и безумие: яко кто человек, иже пойдет вслед совета, елика сотвори в нем?
Kisha nikageuza mawazo yangu kufikiria hekima, wazimu na upumbavu. Ni nini zaidi mtu anayetawala baada ya mfalme anachoweza kufanya ambacho hakijafanywa?
13 И видех аз, яко есть изюбилие мудрости паче безумия, якоже изюбилие света паче тмы:
Nikaona kuwa hekima ni bora kuliko upumbavu, kama vile nuru ilivyo bora kuliko giza.
14 мудраго очи его во главе его, а безумный во тме ходит: и уведех и аз, яко случай един случится всем им.
Mtu mwenye hekima ana macho katika kichwa chake, lakini mpumbavu anatembea gizani; lakini nikaja kuona kwamba wote wawili hatima yao inafanana.
15 И рех аз в сердцы моем: якоже случай безумнаго, и мне случится: и вскую умудрихся? Аз тогда излишше глаголах в сердцы моем, яко и сие суета, понеже безумный от избытка глаголет:
Kisha nikafikiri moyoni mwangu, “Hatima ya mpumbavu itanipata mimi pia. Nitafaidi nini basi kwa kuwa na hekima?” Nikasema moyoni mwangu, “Hili nalo ni ubatili.”
16 яко несть памяти мудраго с безумным во век, зане уже во днех грядущих вся забвена быша: и како умрет мудрый с безумным?
Kwa maana kwa mtu mwenye hekima, kama ilivyo kwa mpumbavu, hatakumbukwa kwa muda mrefu, katika siku zijazo wote watasahaulika. Kama vile ilivyo kwa mpumbavu, mtu mwenye hekima pia lazima atakufa!
17 И возненавидех живот, яко лукавно мне сотворение сотворенное под солнцем: понеже всяческая суета и произволение духа.
Kwa hiyo nikachukia maisha, kwa sababu kazi inayofanyika chini ya jua ilikuwa masikitiko kwangu. Yote hayo ni ubatili, ni kukimbiza upepo.
18 И возненавидех аз всяческая мира и труд мой, имже аз труждаюся под солнцем, яко оставляю его человеку будущему по мне.
Nikachukia kila kitu nilichokuwa nimetaabikia chini ya jua, kwa sababu ni lazima nimwachie yule ajaye baada yangu.
19 И кто весть, мудр ли будет или безумен? И обладати ли имать всем трудом моим, имже трудихся и имже мудрствовах под солнцем? И сие же суета.
Nani ajuaye kama atakuwa ni mtu mwenye hekima au mpumbavu? Lakini hata hivyo yeye ndiye atakayetawala kazi zote ambazo nimemiminia juhudi na ustadi chini ya jua. Hili nalo ni ubatili.
20 И обратихся аз отрещися сердцу моему о всем труде, имже трудихся под солнцем:
Kwa hiyo moyo wangu ukaanza kukata tamaa juu ya kazi yangu yote niliyoifanya kwa taabu chini ya jua.
21 яко есть человек, егоже труд в мудрости и в разуме и в мужестве: и человек, иже не потрудися о нем, даст ему часть свою. И сие суета и лукавство велие.
Kwa kuwa mtu anaweza kufanya kazi yake kwa hekima, maarifa na ustadi, kisha analazimika kuacha vyote alivyo navyo kwa mtu mwingine ambaye hajavifanyia kazi. Hili nalo pia ni ubatili tena ni balaa kubwa.
22 Яко бывает человеку во всем труде его и в произволении сердца его, имже той труждается под солнцем,
Mtu atapata nini kwa taabu yote na kuhangaika kwa bidii katika kazi anayotaabikia chini ya jua?
23 яко вси дние его болезней и ярости попечение ему, ибо в нощи не спит сердце его. И сие же суета есть.
Siku zake zote kazi yake ni maumivu na masikitiko, hata usiku akili yake haipati mapumziko. Hili nalo pia ni ubatili.
24 Несть благо человеку, но (разве) еже яст и пиет и еже покажет души своей благо в труде своем: и сие видех аз, яко от руки Божия есть:
Hakuna kitu bora anachoweza kufanya mtu zaidi ya kula na kunywa na kuridhika katika kazi yake. Hili nalo pia, ninaona, latokana na mkono wa Mungu,
25 яко кто яст и пиет кроме Его?
kwa sababu pasipo yeye, ni nani awezaye kula na kufurahi?
26 Яко человеку благу пред лицем Его даде мудрость и разум и веселие, согрешающему же даде попечение, еже прилагати и собирати, во еже дати благому пред лицем Божиим: яко и сие суета и произволение духа.
Kwa yule mtu anayempendeza Mungu, Mungu humpa hekima, maarifa na furaha, bali kwa mwenye dhambi Mungu humpa kazi ya kukusanya na kuhifadhi utajiri ili Mungu ampe yule anayempenda. Hili nalo pia ni ubatili, ni kukimbiza upepo.