< Четвертая книга Царств 9 >
1 Елиссей пророк призва единаго от сынов пророчих и рече ему: препояши чресла своя, и возми сосуд елеа сего в руку твою, и иди в Рамоф Галаадский:
Nabii Elisha akamwita mmoja wa watoto wa manabii na kumwambia, “Vaa kwa kwa safari, halafu chukua hii chupa ndogo ya mafuta kwenye mikono yako na uende Romoth Geliadi.
2 и внидеши тамо, и узриши тамо Ииуа сына Иосафата сына Намессиева, и внидеши, и изведеши его от среды братии его, и введеши его во внутреннюю клеть:
Wakati utakapofika, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi, na uende ukaingie na kumfanya ainuke kutoka miongoni mwa rafiki zake, na ukampeleke katika chumba cha ndani.
3 и возмеши сосуд елеа, и возлиеши на главу его, и рцы: сице глаголет Господь: помазах тя в царя над Израилем: и отверзеши двери, и да бежиши, и да не пребудеши тамо.
Kisha chukua ile chupa ya mafuta na imiminie kwenye kichwa chake na kusema, 'Yahwe anasema hivi: “Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli. “Halafu fungua mlango, na kukimbia; usichelewe.”
4 И иде отрочищь пророк в Рамоф Галаадский:
Basi yule kijana, yule nabii kijana, akaenda Romoth Geliadi.
5 и вниде, и се, князи силы седяху, и рече: слово ми есть к тебе, о, княже. И рече Ииуй: к кому от всех нас? И рече: к тебе, княже.
Wakati alipofika, kumbe, wale manahodha wa lile jeshi walikuwa wamekaa. Hivyo yule nabii kijana akasema, “Nimekuja mara moja naneno kwako, nahodha.” Yehu akajibu, “kwa yupi katika sisi?” Yule nabii kijana akajibu, “Kwako nahodha.”
6 И воста и вниде в дом: и возлия елей на главу его и рече ему: сице глаголет Господь Бог Израилев: помазах тя в царя над людьми Господними, над Израилем.
Basi Yehu akainuka na kwenda kwenye nyumba, na yule nabii akammiminia mafuta kwenye kichwa chake na kumwambia Yehu, “Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: 'Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Yahwe, juu ya Isaraeli.
7 И да потребиши дом Ахаава господина твоего от лица Моего, и отмстиши кровь рабов Моих пророков и кровь всех рабов Господних от руки Иезавелины.
Wewe lazima uiue familia ya Ahabu bwana wako, ili niweze kulipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa Yahwe, ambao waliokuwa wameuawa kwa mkono wa Yezebeli.
8 И от руки всего дому Ахаавля, и потребиши от дому Ахаавля мочащагося к стене, и содержащагося, и оставльшагося во Израили:
Kwa kuwa nyumba yote ya Ahabu itaangamia, na nitamkatilia mbali kila mtoto wa kiume wa Ahabu, yeyote awe mtumwa au mtu huru.
9 и предам дом Ахаавль, якоже дом Иеровоама сына Наватова и якоже дом Ваасы сына Ахиина:
Nitaifanya nyumba ya Ahabu kama nyumba ya Yerobohamu mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
10 и Иезавель снедят пси в части Иезраеля, и не будет погребающаго ю. И отверзе двери и убежа.
Mbwa watamla Yezebeli katika Yezreeli, na hakutakuwa na mtu wa kumzika.” Kisha nabii akafungua mlango na kukimbia.
11 Ииуй же изыде ко отроком господина своего. И реша ему: мир ли? Что яко вниде неистовый сей к тебе? И рече им: вы весте мужа и суесловие его.
Kisha Yehu akatoka kwenda kwa watumishi wa bwana wake, na mmoja akamwambia, “Je kila kitu kiko sawa? Kwa nini huyu mwenda wazimu amekuja kwako?” Yehu akawajibu, “Mnamjua huyo mtu na mambo asemayo.”
12 И реша: не правда, (аще не возвестиши?) возвести убо нам. И рече Ииуй к ним: тако и тако рече ко мне, глаголя: сице глаголет Господь: помазах тя в царя над Израилем.
Wakasema, “Huo ni uongo. Tuambie.” Yehu akajibu, “Alisema hivi na vile juu yangu, na pia akasema, 'hivi ndivyo Yahwe asemavyo: Nimekumiminia mafuta kama mfalme juu ya Israeli.””
13 И слышавше текоша спешно, и взя кийждо ризы своя, и положиша под ним, понеже на единем от степений седяше, и вострубиша в рог и реша: воцарися Ииуй.
Kisha kila mmoja wao akachukua vazi haraka na kuweka chini ya Yehu juu ya madaraja. Wakapiga baragumu na kusema, “Yehu ni mfalme.”
14 И возвратися Ииуй сын Иосафата сына Намессиева ко Иораму. Иорам же сам стрежаше в Рамофе Галаадстем и весь Израиль от лица Азаила царя Сирийска.
Katika njia hii Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi akafanya njama juu ya Yoramu. Basi Yoramu alikuwa akiilinda Ramothi Gileadi, yeye na Israeli yote, kwa sababu ya Hazaeli mfalme wa Shamu,
15 И возвратися Иорам царь целитися во Иезраели от язв, имиже уязвиша его Сиряне, егда брашеся со Азаилом царем Сирийским. И рече Ииуй: аще есть душа ваша со мною, да не изыдет из града беглец, ити и возвестити во Иезраели.
lakini mfalme Yoramu alikuwa amesharudi kwa Yezreeli ili kuponywa yale majeraha aliyokuwa ameyapewa na Washami, wakati akiwa anapigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Yehu akawaambia watumishi wa Yoramu, “kama hili ndilo wazo lako, kisha usimwache mtu aondoke na kwenda nje ya mji, ili aende kupeleka habari hii Yezreeli.”
16 И вседе на коня, и пойде Ииуй, и сниде во Иезраель, яко Иорам царь Израилев целяшеся во Иезраели от стреляний, имиже устрелиша его Арамины в Рамофе на брани со Азаилом царем Сирским, яко той бе силен и муж силы, и лежаше тамо. И Охозиа царь Иудин прииде видети Иорама.
Basi Yehu akaendesha gari la farasi mpaka Yezreeli; kwa kuwa Yoramu alikuwa amelala huko. Basi Ahazi mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka chini kuonana na Yoramu.
17 И страж взыде на столп во Иезраели, и виде прах Ииуев, егда ити ему и рече: прах аз вижу. И рече Иорам: всади мужа на конь и посли противу им, и да речет: мир ли?
Mlinzi alikuwa amesimama juu ya mnara katika Yezreeli, akaliona lile kundi la Yehu alipokuwa akija kwa mbali kidogo; akasema, “Naona kundi la watu wanakuja.” Yoramu akasema, “Chukua mwendesha farasi, na umtume akakutane nao; mwambie aseme, “Je mnakuja kwa amani?””
18 И иде всадник конный на сретение ему и рече: тако глаголет царь: мир ли? И рече Ииуй: что тебе и миру? Обратися вслед мене. И возвести страж, глаголя: прииде посланный до них и не возвратися.
Hivyo mwendesha farasi akatoka kumlaki; akasema, “Mfalme asema hivi: Je mnakuja kwa amani?”' Basi Yehu akasema, “Wewe una nini na amani? Geuka na unifuate nyuma.” Kisha yule mlinzi akamwambia mfalme, Yule mjumbe ameshaonana nao, lakini anarudi.”
19 И посла всадника коннаго втораго, и прииде к нему и рече: тако рече царь: мир ли? И рече Ииуй: что тебе и миру? Возвратися вслед мене.
Kisha akapeleka mpanda farasi wa pili, ambaye alikuja kwao na kusema, “Mfalme asema hivi: 'Je mnakuja na amani?”' Yehu akajibu, “Wewe una nini na amani? Geuka na kunifuata nyuma.
20 И возвести страж, глаголя: прииде до них и не возвратися: и вождь ведяше Ииуа сына Намессиина, яко в премене бысть.
Tena yule mlinzi akatoa taarifa, “Amekwisha kuonana nao, lakini hatorudi. Kwa kuwa hilo gari la farasi limekuwa likiendeshwa ndivyo ambavyo Yehu mwana wa Nimshi aendeshavyo; anaendesha kwa kasi.”
21 И рече Иорам: впрязите. И впрягоша колесницу: и изыде Иорам царь Израилев и Охозиа царь Иудин, кийждо на колеснице своей, и изыдоста на сретение Ииуа, и обретоста его и части Навуфеа Иезраилитина.
Hivyo Yoramu akasema, “Andaa gari langu la farasi liwe tayari.” Wakaandaa gari lake la farasi, na Yoramu mfalme wa Israeli na Ahazi mfalme wa Yuda akaendesha, kila mmoja kwenye gari lake la farasi, kumlaki Yehu. Wakamkuta kwenye mali ya Nabothi Myezreeli.
22 И бысть яко увиде Иорам Ииуа, и рече мир ли, Ииуе? И рече Ииуй что тебе и миру? Еще блуды Иезавели матери твоея, и чарове ея многия.
Wakati Yoramu alipomuona Yehu, alisema, “Je unakuja katika hali ya amani, Yehu?” Akajibu, “Amani gani hapo, wakati uzinzi wa ukahaba hufanywa na uchawi wa mama yako Yezebeli umejaa tele?”
23 И обрати Иорам руки своя и бежа, и рече ко Охозии: лесть, Охозие.
Basi Yoramu akarudisha magari yake ya farasi na kukimbia na kumwambia Ahazia, “Kuna udanganyifu, Ahazia.
24 И наляче Ииуй рукою своею лук и устрели Иорама посреде плещу его, и изыде стрела сквозе сердце его: и преклонися на колена своя.
Ndipo Yehu akauvuta upinde wake kwa nguvu zake zote na kumpiga Yoramu kati ya mabega yake; mshale ukaenda kwenye moyo wake, akaanguka chini kwenye gari lake la farasi.
25 И рече Ииуй к Вадекару тристату своему: возми и верзи его на части села Навуфеа Иезраилитина, яко помню, аз и ты вседшии на колесницы идохом вслед Ахаава отца его, и Господь рече о нем пррочество сие, глаголя:
Ndipo Yehu akamwambia Bidkari nahodha wake, “Mchukue na mtupie kwenye shamba la Nabothi Myezreeni. Fikiria kuhusu vile ambavyo wewe na mimi tulivyoendesha pamoja baada ya Ahabu baba yake, Yahwe aliuweka juu unabii dhidi yake:
26 не видех ли крове Навуфеевы и крове сынов его вчера, рече Господь? И воздам ему на части сей, рече Господь: и ныне убо взем поверзи его на части сей по глаголу Господню.
Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya watoto wake - asema Yahwe - na nitahakikisha unalipia hili shamba - asema Yahwe. Sasa basi, mchukue na mtupe kwenye hili shamba, sawa sawa na neno la Yahwe.”
27 И Охозиа царь Иудин виде, и побеже путем вефган и гна по нем Ииуй и рече: и сего (не имам оставити). И порази его на колеснице егда идяше в Гай, иже есть Иевлаам и убежа в Магеддон, и умре тамо.
Wakati Ahazi yule mfalme wa Yuda alipoliona hili, akakimbia kwa njia ya Bethi Hagani. Lakini Yehu akamfuata, na kusema, “Muulie humo kwenye gari la farasi,” na wakampiga mahali pa kupandia Guri, karibu na Ebleamu. Ahazi akakimbilia Megido na kufia pale.
28 И возложиша его отроцы его на колесницу и везоша его во Иерусалим, и погребоша его во гробе его во граде Давидове.
Watumishi wake wakaubeba mwili wake kwa magari ya farasi kwenda Yerusalemu na kumzika kwenye kaburi lake pamoja na baba zake katika mji wa Daudi.
29 И в первоенадесять лето Иорама царя Израилева воцарися Охозиа над Иудою.
Basi ilikuwa mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu huyo Ahazia akaanza kutawala juu ya Yuda.
30 И прииде Ииуй во Иезраель (град). Иезавель же услыша, и намаза лице свое и украси главу свою, и приниче окном.
Wakati Yahu alipokuja kwa Yezebeli, Yezebeli akasikia juu ya hilo, akapaka wanja kwenye macho yake, akatengeneza nywele zake vizuri, na kuchungulia kwenye dirisha.
31 И Ииуй вхождаше во град и рече: мир ли Замврию, убийце господина своего?
Kadiri Yehu alipokuwa akiingia kwenye lango, akamwambia, “Je unakuja kwa amani, wewe Zimri, muuaji wa bwana wako?”
32 И воззре лицем своим на окно и виде ю и рече: кто ты еси? Сниди ко мне. И преклонистася к нему два скопца.
Yehu akatazama juu ya dirisha na kusema, “Ni nani yuko upande wangu? Nani?” Matowashi wawili au watatu wakachungulia nje.
33 И рече Ииуй: сверзита ю. И свергоста ю, и окропишася кровию ея стены и кони, и попраша ю.
Basi Yehu aksema, “Mtupeni chini.” Hivyo wakamtupa Yezebeli chini, na damu yake nyingine ikamwagika kwenye ukuta na farasi, na Yehu akamkanyaga kanyaga chini ya miguu.
34 И вниде Ииуй, и яде и пи, и рече: осмотрите ныне проклятую сию, и погребите ю, яко дщерь царева есть.
Basi Yehu akaingia hiyo sehemu, akala na kunywa. Kisha akasema, “Mtazamani sasa huyu mwanamke aliyelaaniwa na kumzika, kwa kuwa ni binti wa mfalme.”
35 И идоша погребсти ю, и не обретоша от нея ничто ино, токмо лоб и ноги и длани рук.
Wakaenda kumzika, lakini hawakumkuta ila fuvu, miguu, na viganga vya mikono yake.
36 И возвратишася и возвестиша ему. И рече: слово Господне, еже глагола рукою раба Своего Илии Фесвитянина, глаголя: в части Иезраеля снедят пси плоть Иезавелину:
Basi wakarudi na kumwambia Yehu. Akasema, “Hili ndilo neno la Yahwe ambalo ameliongea kupitia Eliya Mtishbi, likisema, 'Katika nchi Yezreeli mbwa ataula mwili wa Yezebeli,
37 и будет труп Иезавелин аки гной на лицы села в части Иезраеля, яко не рещи им: сия есть Иезавель.
na mwili wa Yezebeli utakuwa kama kinyesi juu ya uso wa mashamba katika nchi ya Yezreeli, kwa hiyo basi hakuna atakayeweza kusema, “Huyu ni Yezebeli.””