< Вторая книга Паралипоменон 3 >
1 И нача Соломон созидати дом Господень во Иерусалиме, на горе Амориа, на месте, еже уготова Давид на гумне Орны Иевусеанина:
Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi.
2 нача же созидати в месяц вторый лета четвертаго царства своего.
Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.
3 И сице нача Соломон созидати дом Божий: в долготу лакот, размер первый, лакот шестьдесят, в широту же лакот двадесять:
Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini na upana dhiraa ishirini.
4 и притвор пред лицем дому, долгота по лицу широты дому, лакот двадесять, высота же лакот сто двадесять и позлати его внутрь златом чистым.
Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini. Akaufunika ndani kwa dhahabu safi.
5 Дом же великий окры дсками кедровыми и позлати златом чистым: извая же на нем подобия фиников и яко мрежицы промежь себе сплетающяся,
Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo.
6 и украси храм камением драгим славно, и позлати златом, еже от Фаруима.
Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu.
7 И позлати дом и стены его, и врата и праги, и окна и двери златом, и извая херувимы на стенах.
Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.
8 Сотвори же дом Святая Святых, долгота его по лицу широты дому, лакот двадесять, широта такожде двадесять лакот, и позлати и златом чистым на херувимех, талант шесть сот.
Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 120 za dhahabu safi.
9 И вес гвоздий, вес гвоздя единаго пятьдесят сикль злата, и горницу позлати златом.
Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.
10 И сотвори в дому Святая Святых Херувима два, дело от древ негниюших и позлати их златом.
Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu.
11 И криле херувимов, долгота двадесять лакот, и едино крило лакот пяти, прикасающееся стене дому,
Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano, nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine.
12 и другое крило пяти лакот, прикасающееся крилу херувима другаго:
Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza.
13 криле же херувимов сих распростерте на лакот двадесять, тии же стояху на нозех своих, лица же их (зряще) к дому.
Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.
14 Сотвори же завесу от синеты и багряницы, и червленицы и виссона, и сотка на ней херувимы.
Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.
15 И сотвори пред храмом столпа два, лакот тридесять пять в высоту, и главы их пять лакот.
Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano.
16 И сотвори чепи в давире и положи на главах столпов, и шипков сотвори сто, ихже положи на мрежи.
Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo.
17 И постави столпы пред лицем храма, единаго одесную, а другаго ошуюю: и нарече имя сущему одесную Исправление, имя же сущему ошуюю Крепость.
Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.