< Вторая книга Паралипоменон 29 >
1 И Езекиа нача царствовати сый двадесяти и пяти лет, и двадесять девять лет царствова во Иерусалиме. Имя же матери его Авиа, дщерь Захариина.
Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
2 Сотвори же правое пред Господем по всем, яже сотвори Давид отец его.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.
3 И бысть егда ста на царстве своем в месяц первый, отверзе двери дому Господня и обнови их,
Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati.
4 и введе священники и левиты, и постави их на стране яже к востоку,
Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki
5 и рече им: послушайте мя, левити, ныне очиститеся и очистите дом Господа Бога отец наших, и изрините нечистоту из святилища:
na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu.
6 яко отступиша отцы наши и сотвориша лукавое пред Господем Богом нашим, и оставиша Его, и отвратиша лице свое от скинии Господни, и даша хребет,
Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao.
7 и заключиша врата храма, и погасиша светилники, и фимиамом не кадиша, и всесожжений не принесоша во святилищи Богу Израилеву:
Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli.
8 и разгневася яростию Господь на Иуду и на Иерусалим, и предаде их во ужас и погубление и на звиздание, якоже вы видите очима вашима:
Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe.
9 и се, поражени быша отцы наши мечем, и сынове наши и дщери нашя и жены нашя в пленении в земли не своей, якоже и ныне суть:
Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka.
10 ныне убо положите на сердца ваша, еже завещати завет с Господем Богом Израилевым, и отвратит гнев ярости Своея от нас:
Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi.
11 и ныне не пренебрегайте, яко вас избра Господь стояти пред Ним, служити Ему, и да будете Ему служаще и кадяще.
Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”
12 И восташа левити, Маал сын Амасиев и Иоиль сын Захариев от сынов Каафовых, и от сынов Мерариных Кис сын Авдиев и Азариа сын Илаелилов, и от сынов Гедсоних Иоадад сын Земмань и Иоадам, сии сынове Иоахаини:
Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi: Kutoka kwa Wakohathi, Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria; kutoka kwa Wamerari, Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli; kutoka kwa Wagershoni, Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;
13 от сынов Елисафаних Самарий и Иеиил, и от сынов Асафовых Захариа и Матфаниа,
kutoka kwa wana wa Elisafani, Shimri na Yeieli; kutoka kwa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
14 и от сынов Еманих Иеиил и Семей, от сынов же Идифумлих Самафиа и Озиил:
kutoka kwa wana wa Hemani, Yehieli na Shimei; kutoka kwa wana wa Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
15 собраша же братию свою и освятишася по заповеди цареве повелением Господним, да очистят дом Божий:
Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana.
16 и внидоша священницы внутрь церкве Господни, да очистят ю, и извергоша всю нечистоту обретенную в дому Господни и во дворе дому Господня: и вземше левити, изнесоша к потоку Кедрску вон.
Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni.
17 И начаша в первый день новомесячия перваго месяца очищати, и в день осмый того месяца внидоша во храм Господень, и очистиша церковь Господню во осми днех, и в день шестыйнадесять месяца перваго совершиша.
Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.
18 И внидоша внутрь ко Езекии царю и рекоша: очистихом вся, яже в дому Господни, олтарь всесожжения и сосуды его, и трапезу предложения со всеми сосуды ея,
Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
19 и вся сосуды, яже оскверни царь Ахаз в царство свое во отступлении своем, уготовахом и очистихом, и се, суть пред олтарем Господним.
Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”
20 И воста рано Езекиа царь, и собра началники града, и взыде в дом Господень,
Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana.
21 и вознесе телцев седмь и овнов седмь, агнцев седмь и козлов от коз седмь за грех, за царство и за святилище и за Израиля, и рече сыном Аароним священником, да взыдут на олтарь Господень жрети телцев.
Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana.
22 И заклаша телцев, и взяша кровь священницы и излияша на олтарь: и заклаша овнов и кровь на олтарь возлияша: и заклаша агнцев и облияша кровию олтарь:
Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu.
23 и приведоша козлов, иже за грех, пред царя и церковь, и возложиша руки своя на них,
Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu.
24 и пожроша их священницы, и покропиша кровию их пред олтарем, и помолишася о всем Израили: зане рече царь, о всем Израили всесожжение и яже о гресе.
Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.
25 Постави же левиты в дому Господни с кимвалы и псалтирми и гусльми, по заповеди Давида царя и Гада провидца царю и Нафана пророка, яко по заповеди Господней повеление (бысть) рукою пророков Его.
Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake.
26 Сташа же левити со органы Давидовы и священницы с трубами.
Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.
27 И повеле Езекиа, да вознесут всесожжение на олтарь: и егда начаша возносити всесожжение, начаша хвалы пети Господеви и трубити при органех Давида царя Израилева.
Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli.
28 И вся церковь покланяшеся, и певцы пояху, и трубы трубяху, дондеже совершися всесожжение.
Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.
29 Егда же скончаша приношение, преклонися царь и вси иже бяху с ним и поклонишася Господеви.
Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu.
30 Повеле же Езекиа царь и князи левитом, да восхвалят Господа словесы Давидовыми и Асафа пророка: иже восхвалиша в веселии, и падоша, и поклонишася Господеви.
Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.
31 И отвеща Езекиа и рече: ныне исполнисте руки вашя Господу, приведите и принесите жертвы хваления в дом Господень. И принесе (все) собрание жертвы и хвалы в дом Господень, и всяк усердный сердцем всесожжения.
Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.
32 И бысть число всесожжения, еже принесе собрание, телцев седмьдесят, овнов сто, агнцев двести, вся сия во всесожжение Господеви:
Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana.
33 освященных же телцев шестьсот, овец три тысящы.
Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000.
34 Но священницы не мнози бяху и не можаху одирати кож всесожжения, и помогоша им братия их левити, дондеже исполнися дело и дондеже освятишася жерцы, левити бо усерднее освятишася, нежели священницы:
Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani.
35 всесожжения же много в туках совершения спасения, и возлияний всесожжения: и исправися дело в дому Господни.
Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa. Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya.
36 Возвеселися же Езекиа и вси людие, яко уготова Бог людем, понеже внезапу бысть слово.
Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.