< Первая книга Царств 17 >

1 И собираша иноплеменницы полки своя на брань, и собрашася в Сокхофе Иудейстем, и ополчишася среде Сокхофа и среди Азика во Афесдоммине.
Basi Wafilisti walikusanya majeshi yao kwa ajili ya vita. Walikusanyika huko Soko, iliyoko Yuda. Nao wakapiga kambi kati ya Soko na Aseka katika Efesdamimu.
2 Саул же и мужие Израилевы собрашася и ополчишася во удоли Теревинфа и устрояхуся на брань противу иноплеменником.
Sauli na watu wa Israeli alijikusanya na kuweka kambi katika bonde la Ela, na wakapanga vita kukutana na Wafilisti.
3 И иноплеменницы стояху на горе отсюду особь, Израиль же стояше на горе отюнуду, и удоль между ими бяше.
Wafilisti walisimama juu ya mlima upande mmoja, na Iraeli nao walisimama juu ya mlima upande mwingine wakitenganishwa na bonde kati yao.
4 И изыде муж силен из полка иноплеменнича, имя ему Голиаф от Гефа, высота его шесть лакот и пядь:
Mtu mmoja mwenye nguvu akatoka katika kambi ya Wafilisti, mtu huyo aliitwa Goliathi wa Gathi, kimo chake mikono sita na shubiri moja.
5 и шлем медян на главе его, и в броню кольчату той оболчен бяше: и вес брони его пять тысящ сикль меди и железа:
Alikuwa na chepeo ya shaba kichwani mwake, na alivaa dirii ya chuma. Hiyo dirii ilikuwa na uzito wa shekeli elfu hamsini za shaba.
6 и поножы медяны верху голений его, и щит медян на плещах его:
Alikuwa na mabampa ya shaba kwenye miguu yake na mkuki wa shaba katikati ya mabega yake.
7 и ратовище копия его аки орудие ткущих, и копие его шесть сот сикль железа: и носяй оружие его идяше пред ним.
Ule mpini wa mkuki wake ulikuwa mkubwa, wenye kamba iliyo na kitanzi kwa ajili ya kuutupia kama kamba ya sindano ya mfumaji. Kichwa cha mkuki wake kilikuwa na uzito wa shekeli mia sita za chuma. Aliyembebea ngao alitembea mbele yake.
8 И ста и возопи пред полки Израилевыми и рече им: почто изыдосте, ополчитися ли на брань противу нам? Несмь ли аз иноплеменник, вы же Еврее Сауловы? Изберите себе мужа, и да снидет ко мне:
Alisimama akayapigia kelele majeshi ya Israeli, “Kwa nini mmekuja na mmejipanga kwa ajili ya vita? Mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli? Chagueni mtu kutoka kwenu ateremke na kuja kwangu.
9 и аще возможет со мною братися и одолеет ми, будем вам раби: аще же аз возмогу одолети ему, будете вы нам раби и поработаете нам.
Kama anaweza kupigana nami na kuniua, hapo ndipo tutakuwa watumwa wenu. Lakini kama nitamshinda na kumuua, basi mtakuwa watumwa wetu na kututumikia.”
10 И рече иноплеменник: се, аз днесь уничижих полк Израилев в сей день: дадите ми мужа, иже поборется со мною един.
Mfilisti huyo akasema tena, “Leo ninayapa changamoto majeshi ya Israeli. Mnipe mtu ili tuweze kupigana naye.”
11 И слыша Саул и весь Израиль глаголы иноплеменничи сия и ужасошася и убояшася зело.
Sauli na Israeli wote waliposikia alichosema Mfilisti huyo, walikata tamaa na kuogopa sana.
12 Давид же Ефрафеев, сей бе от Вифлеема Иудина, имя же отцу его Иессей, емуже бе осмь сынов. Во дни же Сауловы бе муж той состареся в мужех.
Basi Daudi alikuwa mwana wa Mwefraimu wa Bethtelehemu ya Yuda, aliyeitwa Yese. Naye alikuwa na watoto wanane wa kiume. Yese alikuwa mtu mzee katika siku za Sauli, mwenye umri mkubwa kati ya watu.
13 И идоша три сыны Иессеевы старейшии на брань с Саулом: имена же сынов его пошедших на брань, Елиав первородный его, и вторый Аминадав, и третий Самма.
Watoto watatu wakubwa wa Yese walimfuata Sauli vitani. Majina ya watoto wake watatu waliokwenda vitani yalikwa ni Eliabu mzaliwa wa kwanza, aliyemfuata Abinadabu, na watatu aliitwa Shama.
14 Давид же бе юнейший, и три болшии его идоша вслед Саула.
Daudi ndiye aliyekuwa mdogo kabisa. Hao wakubwa watatu walimfuata Sauli.
15 Давид же возвратився от Саула, отиде пасти овцы отца своего в Вифлеем.
Basi Daudi alikwenda na kurudi akipita kati ya majeshi ya Sauli akiwa na kondoo za baba yake huko Bethtelehemu, ili kuwachunga.
16 И прихождаше иноплеменник утро и в вечер, являяся пред Израилем четыредесять дний.
Kwa muda wa siku arobaini yule Mfilisti mwenye nguvu alikuwa akijitokeza asubuhi na jioni kwa ajili ya vita.
17 И рече Иессей Давиду сыну своему: возми убо братиям твоим меру ефи муки и десять хлеб сих, и иди в полк, и даждь братиям твоим:
Kisha Yese akamwambia mwanawe Daudi, “Wapelekee kaka zako efa ya bisi na hii mikate kumi, na uzipeleke upesi kule kambini kwa ajili ya kaka zako.
18 и десять сыров от млека сего, и даждь тысящнику: и братию свою посети в мире, и еликих аще требуют, увеси, субботствовати же будеши со мною.
Pia peleka hizi jibini kumi kwa jemedari wa kikosi chao cha elfu. Ukawaangalie wako na hali gani kisha uniletee habari kuhusu wanavyoendelea vizuri.
19 Саул же и вси людие бяху во удоли дуба ратующеся со иноплеменники.
Kaka zako wako pamoja na Sauli na watu wote wa Israeli katika bonde la Ela, wanapigana na Wafilisti.”
20 И воста Давид рано, овцы же остави со стражею, и взя, и отиде, якоже заповеда ему отец его Иессей: и прииде на место, идеже исхождаху сильнии на брань и вопияху в полцех.
Daudi aliamka asubuhi na mapema na kuliacha kundi chini ya uangalizi wa mchungaji. Akachukua vile vitu na kuondoka, kama Yese alivyomwamuru. Akafika kambini wakati jeshi linaondoka kwenda uwanja wa vita wakipiga kelele za vita.
21 Занеже вооружашеся Израиль противу иноплеменником, и иноплеменницы вооружахуся противу Израиля.
Nao Israeli na Wafilisti walijipanga kivita, jeshi dhidi ya jeshi.
22 И положи Давид бремя свое в руках стража, и тече в полк, и пришед вопроси братию свою в мире.
Daudi aliviacha vitu vyake kwa mtunza mahitaji, akalikimbilia jeshi, na kuwasalimia kaka zake.
23 Глаголющу же ему с ними, и се, муж месейский, емуже имя Голиаф, Филистимлянин от Гефы, изыде от полков иноплеменничих и глагола по словесем сим, и услыша Давид.
Alipoongea nao, yule mtu mwenye nguvu, Mfilisti wa Gathi, jina lake Goliathi, akajitokeza kutoka majeshi ya Wafilisti, naye akasema maneno yaleyale kama hapo mwanzo. Naye Daudi akayasikia.
24 И вси мужие Израилевы егда увидеша мужа, и бежаша от лица его и убояшася зело.
Watu wote wa Israeli walipomwona Goliathi, walimkimbia na waliogopa sana.
25 И реша мужие Израилтестии: видесте ли мужа сего восходяща, яко поносити Израиля прииде? И аще будет муж, иже убиет его, обогатит его царь богатством велиим, и дщерь свою даст ему, и дом отца его сотворит свободен во Израили.
Watu wa Israeli walisema, “Umemuona mtu huyu aliyejitokeza? Amekuja kuipa changamoto Israeli. Basi mfalme atampa mali nyingi mtu atakayemua, atamuozesha binti yake, na familia ya baba yake haitalipa kodi katika Israeli.”
26 И рече Давид к мужем стоящым с ним, глаголя: что сотворите мужу, иже убиет иноплеменника онаго и отимет поношение от Израиля? Яко кто есть иноплеменник необрезанный сей, иже поносит полку Бога живаго?
Daudi akawauliza watu waliosimama karibu naye, “Atafanyiwa nini mtu ambaye atamuua Mfilisti huyu na kuiondolea Israeli fedheha? Ni nani Mfilisti huyu asiyetahiriwa ayatukanaye majeshi ya Mungu aliye hai?”
27 И рекоша ему людие по словеси сему, глаголюще: тако сотворится мужу, иже убиет его.
Ndipo watu wakarudia kile walichokuwa wamesema na kumwambia, “Ndivyo iitakavyofanyika kwa mtu atakayemuua.”
28 И услыша Елиав брат его болший, внегда глаголати ему к мужем: и разгневася яростию Елиав на Давида и рече: почто семо пришел еси? И кому оставил еси малыя овцы оны в пустыни? Вем аз гордость твою и злобу сердца твоего, яко видения ради брани пришел еси.
Kaka yake mkubwa Eliabu, alisikia wakati akisema na watu. Hasira ya Eliabu ikawaka moto dhidi ya Daudi, naye akamuuliza, “Kwa nini umekuja hapa? Wale kondoo wachache umewaacha na nani huko nyikani? Nakijua kiburi chako, na utundu wa moyo wako; maana umekuja hapa ili uweze kuona mapigano.”
29 И рече Давид: что сотворих ныне? Несть ли речь?
Naye Daudi akamjibu, “Nimefanya nini sasa? Mimi si nuliuliza swali tu?
30 И отвратися от него ко иному и рече по словеси сему. И отвещаша ему людие по словеси прежнему.
Akamgeukia mtu mwingine na kumwacha huyo, na kusema vivyo hivyo. Nao watu wakajibu vilevile kama mwanzo.
31 И слышаны быша глаголы, ихже глагола Давид, и возвестиша пред Саулом: и пояша его людие и приведоша его пред Саула.
Maneno aliyosema Daudi yaliposikika, askari waliyasema tena kwa Sauli, naye akawatuma kwa Daudi.
32 И рече Давид к Саулу: да не ужасается сердце господину моему о сем, раб твой пойдет и поборется со иноплеменником сим.
Kisha Daudi akamwambia Sauli, “Pasiwepo moyo wa mtu atakayezimia kwa sababu ya Mfilisti huyo; Mtumishi wako atakwenda kupigana na Mfilisti huyu.”
33 И рече Саул к Давиду: не возможеши пойти ко иноплеменнику сему братися с ним, яко ты детищь еси, сей же муж борец есть от юности своея.
Sauli akamwambia Daudi, “Huwezi kumpinga Mfilisti ama kupigana naye; wewe ni kijana tu, na yeye amekuwa mtu wa vita tangu ujana wake.”
34 И рече Давид к Саулу: егда пасяше раб твой отца своего стадо, и егда прихождаше лев или медведица и восхищаше от стада овцу едину:
Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake. Mara simba au dubu alikuja akamchukua mwana kondoo kutoka kundini,
35 и аз вслед его исхождах и поражах его, и исторгах из уст его (взятое): и аще воспротивляшеся ми, то взем за гортань его, поражах и умерщвлях его:
Nilimfukuza na kumshambulia na kumpokonya kutoka kinywani mwake. Na aliponirukia, nilimshika ndevu zake, nilimpiga, na kumuua.
36 и льва и медведицу бияше раб твой, и будет иноплеменник необрезанный сей яко един от сих: не поиду ли, и поражу его, и отиму днесь поношение от Израиля? Понеже кто необрезанный сей, иже уничижи полк Бога жива?
Mtumishi wako amekwisha kmuua simba na dubu. N huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa wanyama hao, kwa kuwa ameyadharau majeshi ya Mungu aliye hai.”
37 И рече Давид: Господь иже изят мя от руки львовы и от руки медведицы, той измет мя от руки иноплеменника сего необрезаннаго. И рече Саул к Давиду: иди, и да будет Господь с тобою.
Daudi akasema, “BWANA aliyeniokoa kutoka makucha ya simba na makucha ya dubu. Ataniokoa kutoka mkono wa Mfilisti huyu.” Kisha Sauli akamwambia Daudi, “Nenda, BWANA awe pamoja nawe.”
38 И облече Саул Давида одеждею, и шлем медян возложи на главу его,
Sauli akamvika Daudi vazi lake la vita. Akamvika chepeo ya shaba kichwani pake, na akamvika koti la chuma.
39 и препояса Давида оружием своим верху одежды его. Давид же походив (во оружии) семо и овамо, утрудися, яко не обыче. И рече Давид Саулу: не могу ити в сих, яко не обыкох. И взяша от него сия.
Daudi akaufunga upanga wake juu ya vazi la Sauli. Lakini hakuweza kutembea, kwa sababu hakupata mafunzo kwa mavazi hayo. Ndipo Daudi akamwambia Sauli, “Siwezi kwenda kupigana nikiwa na haya, maana sikupata mafunzo kwa haya.” Kwa hiyo Daudi akayavua.
40 И взя палицу свою в руку свою, и избра себе пять камений гладких от потока, и вложи я в тоболец пастырский егоже ношаше, и пращу свою имый в руце своей, и иде к мужу иноплеменнику.
Akachukua fimbo mkononi mwake na akachagua mawe matano laini kutoka katika kijito; akayaweka kwenye mfuko wake wa kichungaji. Kombeo lake lilikuwa mkononi akawa anamsogelea yule Mfilisti.
41 И идяше иноплеменник приближаяся к Давиду, и носяй оружие его пред ним (идяше).
Yule Mfilisti akaja na kumsogelea Daudi, mbeba ngao yake akiwa mbele yake.
42 И виде Голиаф иноплеменник Давида и обезчествова его, зане той детищь бе, и чермен и леп очима.
Mfilisti alipotazama kila upande na kumuona Daudi, akamdharau, maana alikuwa kijana tu, mwekundu, na umbo la kupendeza.
43 И рече иноплеменник к Давиду: еда пес аз есмь, яко ты идеши противу мене с палицею и камением? И рече Давид: ни, но и хуждший пса. И прокля иноплеменник Давида боги своими.
Ndipo Mfilisti akamuuliza Daudi, “Je, mimi ni mbwa, hata ukanijia na fimbo? Naye Mfilisti kwa miungu yake akamlaani Daudi.
44 И рече иноплеменник к Давиду: гряди ко мне, и дам плоть твою птицам небесным и зверем земным.
Huyo Mfilisti akamwambia Daudi, “Njoo kwangu, na nyama yako nitawatupia ndege wa angani na wanyama wa mwituni.”
45 И рече Давид иноплеменнику: ты идеши на мя с мечем и с копием и щитом, аз же иду на тя во имя Господа Бога Саваофа, Бога ополчения Израилева, егоже ты уничижил еси днесь:
Daudi akamjibu Mfilisti, “Unaniijia kwa upanga, kwa mkuki na mkuki mdogo. Bali mimi nakuijia kwa jina la BWANA wa majeshi, Mungu wa Majeshi ya Israeli, uliyemdharau.
46 и предаст тя Господь днесь в руце мои, и убию тя, и отиму главу твою от тебе, и дам тело твое и телеса полка иноплеменнича в день сей птицам небесным и зверем земным: и уразумеет вся земля, яко есть Господь Бог во Израили,
Leo BWANA atanipa ushindi dhidi yako, na nitakuua na kukiondoa kichwa chako kwenye kiwiliwili. Leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni walioko duniani mizoga ya jeshi la Wafilisti, ili dunia yote ijue kwamba yupo Mungu katika Israeli,
47 и уразумеет весь сонм сей, яко не мечем ни копием спасает Господь, яко Господня брань, и предаст Господь вас в руки нашя.
na kusanyiko hili lote lijue kwamba BWANA hatoi ushindi kwa upanga wala kwa mkuki. Kwa kuwa vita ni ya BWANA, na atawaweka katika mkono wetu.”
48 И воста иноплеменник и иде во сретение Давиду. И ускори Давид и тече на сражение во сретение иноплеменнику.
Mfilisti aliponyanyuka na kukaribia akutane na Daudi, ndipo Daudi akakimbia kwa haraka kuelekea jeshi la adui ili akutane naye.
49 И простре Давид руку свою в тоболец, и изя из него камень един, (и вложи в пращу, ) и верже пращею, и порази иноплеменника в чело его, и унзе камень под шлемом его в чело его, и паде (Голиаф) на лицы своем на землю.
Daudi aliweka mkono wake mfukoni, akachukua jiwe kutoka humo, akalitupa kwa kombeo, na likampiga Mfilisti kwenye paji la uso, akaanguka chini kifudifudi.
50 И укрепися Давид над иноплеменником пращею и каменем, и порази иноплеменника, и умертви его: оружия же не бе в руце Давидове.
Daudi alimshinda Mfilisti kwa kombeo na kwa jiwe moja. Alimpiga huyo Mfilisti na kumuua. Mkononi mwa Daudi hakukuwa na upanga.
51 И тече скоро Давид, и ста над ним, и взя мечь его, и извлече его от недр его, и умертви его, и отсече им главу его. И видеша иноплеменницы, яко умре сильный их, и бежаша.
Ndipo Daudi akakimbia akasimama juu ya Mfilisti na kutwaa upanga wake, akauchomoa kutoka alani, akamuua, na kukata kichwa chake kwa upanga huo.
52 И восташа мужие Израилевы и Иудины и воскликнуша, и погнаша созади их даже до входа Гефова и до врат Аскалонских: и падоша уязвленни (мнози) иноплеменницы по пути врат и даже до Гефа и Аккарона.
Ndipo watu wa Israeli na wale wa Yuda wakaamka kwa kelele, na kuwafukuza Wafilisti kuvuka bonde na malango ya Ekroni. Na maiti za Wafilisti walilala katika njia iendayo Shaaraimu, na njia yote kuelekea Gathi na Ekroni.
53 И возвратишася мужие Израилевы гнавшии вслед иноплеменник, и потопташа полки их.
Watu wa Israeli wakarejea kutoka kuwafukuza Wafilisti, na wakateka nyara kambi yao.
54 И взя Давид главу иноплеменника и внесе ю во Иерусалим, и оружие его положи во храмине своей.
Daudi akachukua kichwa cha Mfilisti na kukipeleka Yerusalemu, lakini akaliweka vazi la vita katika hema lake.
55 И егда виде Саул Давида исходяща во сретение иноплеменника, рече ко Авениру князю силы: чий есть сын юноша сей, Авенире? И рече Авенир: да живет душа твоя, царю, яко не вем.
Sauli alipomuona Daudi akienda kukabiliana na yule Mfilisti, akamwambia Abneri, jemedari wa jeshi, “Abneri, kijana huyu ni mtoto wa nani? Abneri akasema, “Kama uishivyo, mfalme, mimi sijui.”
56 И рече царь: вопроси убо ты, чий есть сын юноша сей?
Naye mfalme akasema, “Waulize wanaoweza kufahamu, mvulana huyu ni kijana wa nani.”
57 Егда же возвратися Давид по убиении иноплеменника, взя его Авенир и приведе его пред Саула: глава же иноплеменнича бе в руце его.
Daudi aliporudi kutoka kumuua yule Mfilisti, Abneri alimchukuwa, na kumleta mbele ya Sauli akiwa na kichwa cha Mfilisti mkononi mwake.
58 И рече к нему Саул: чий еси сын, юноше? И рече Давид: сын раба твоего Иессеа от Вифлеема.
Sauli akamuuliza, “Kijana, wewe ni mtoto wa nani? Na Daudi akamjibu, “Mimi ni mtoto wa mtumishi wako Yese Mbethlehemu.”

< Первая книга Царств 17 >