< Первая книга Царств 15 >

1 И рече Самуил к Саулу: посла мя Господь помазати тя на царство в людех Его во Израили: и ныне послушай гласа словес Господних:
Samweli akamwambia Sauli, “Mimi ndiye ambaye Bwana alinituma nikutie mafuta uwe mfalme juu ya watu wake Israeli, basi sasa sikiliza ujumbe kutoka kwa Bwana.
2 сия рече Господь Саваоф: ныне отмщу, яже сотвори Амалик Израилю, егда срете его на пути, восходящу ему от Египта:
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu Waamaleki kwa kile walichowatendea Israeli walipowavizia wakati walipanda kutoka Misri.
3 и ныне ты иди, и поразиши Амалика и Иерима, и вся яже суть его, и не снабдиши от них (ничтоже), и искорениши его: и прокленеши его и вся сущая его, и не пощадиши его: и да убиеши от мужеска полу и до женска и от юнош и до ссущих млеко, и от говяд до овец и от велблюд до ослят.
Basi sasa nenda ukawashambulie Waamaleki na kuwaangamiza kabisa pamoja na kila kitu kilicho mali yao. Usiwahurumie; waue wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, ngʼombe na kondoo, ngamia na punda.’”
4 И собра люди Саул и сочте я в Галгалех двесте тысящ пеших и десять тысящ от Иуды в полцех:
Ndipo Sauli akawaita watu na kuwapanga huko Telaimu, askari wa miguu 200,000 pamoja na watu 10,000 kutoka Yuda.
5 и прииде Саул до градов Амаликовых и засяде в потоце.
Sauli akaenda katika mji wa Amaleki na kuwavizia bondeni.
6 И рече Саул ко Кинеови: иди и уклонися от среды Амалика, да не погублю тя с ним, ты бо сотворил еси милость с сынми Израилевыми, егда исхождаху из Египта. И уклонися Киней от среды Амалика.
Kisha akawaambia Wakeni, “Ondokeni, waacheni Waamaleki ili nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao, kwa kuwa ninyi mliwatendea mema Waisraeli wote wakati walipanda kutoka Misri.” Basi Wakeni wakaondoka, wakawaacha Waamaleki.
7 И порази Саул Амалика от Евилы даже до Сура, иже пред лицем Египта:
Ndipo Sauli akawashambulia Waamaleki toka Havila mpaka Shuri, hadi mashariki ya Misri.
8 и ят Агага царя Амаликова жива, и вся люди изби, и Иерима уби мечем.
Akamchukua Agagi, mfalme wa Waamaleki akiwa hai, nao watu wake wote akawaangamiza kabisa kwa upanga.
9 И сохрани Саул и вси людие Агага царя жива и благая от стад и буйволов, и снедей (и одежд), и виноградов и от всех благих: и не хотяху искоренити я, точию хуждшее и уничиженое истребиша.
Lakini Sauli na hilo jeshi wakamhifadhi hai Agagi na kondoo na ngʼombe walio wazuri, mafahali na wana-kondoo walionona kila kitu kilichokuwa kizuri. Hivi vitu hawakuwa radhi kuviangamiza kabisa, bali kila kitu kilichodharauliwa na kilicho dhaifu wakakiangamiza kabisa.
10 И бысть глаголгол Господень к Самуилу, глаголя:
Kisha neno la Bwana likamjia Samweli kusema:
11 раскаяхся, яко помазах Саула на царство, понеже отвратися от Мене и словес Моих не соблюде. И опечалися Самуил и вопияше ко Господу всю нощь.
“Ninasikitika kwamba nimemfanya Sauli kuwa mfalme, kwa sababu ameacha kunifuata mimi na hakutimiza maagizo yangu.” Samweli akafadhaika, naye akamlilia Bwana usiku ule wote.
12 И воста рано Самуил, и идяше на сретение Израилтяном рано. И возвестиша Самуилу, глаголюще: идет Саул в Кармил, и се, воздвиже руку себе, и возврати колесницу, и сниде в Галгалы. И прииде Самуил к Саулу, и се, той возношаше всесожжение Господу, первая от корыстей, ихже взя от Амаликов.
Asubuhi na mapema Samweli akaamka kwenda kukutana na Sauli, lakini akaambiwa, “Sauli amekwenda Karmeli. Huko amesimamisha mnara kwa heshima yake mwenyewe naye ameendelea na kuteremkia Gilgali.”
13 И прииде Самуил к Саулу, и рече ему Саул: благословен ты Господу, сотворих бо вся, елика (ми) глагола Господь.
Samweli alipomfikia, Sauli akamwambia, “Bwana akubariki! Nimetimiza yale Bwana aliniagiza.”
14 И рече Самуил: и кий глас стад сих во ушию моею, и глас говяд, егоже аз слышу?
Lakini Samweli akasema, “Nini basi huu mlio wa kondoo masikioni mwangu? Huu mlio wa ngʼombe ninaousikia ni kitu gani?”
15 И рече Саул: от Амалика пригнах я, ихже сохраниша людие лучшая от стад и от волов, еже пожрети я Господу Богу твоему, прочая же избих.
Sauli akajibu, “Askari wamewaleta kutoka kwa Waamaleki, waliwaacha wale kondoo na ngʼombe wazuri ili kuwatoa dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, lakini tuliwaangamiza kabisa wengine wote.”
16 И рече Самуил к Саулу: потерпи, и возвещу ти, яже глагола Господь ко мне нощию.
Samweli akamwambia Sauli, “Ngoja! Nami nitakuambia lile Bwana aliloniambia usiku huu.” Sauli akajibu, “Niambie.”
17 И рече ему (Саул): глаголи. И рече Самуил к Саулу: еда не мал был еси ты пред Ним, и не властелина ли тя постави хоругви колена Израилева? И помаза тя Господь на царство Израилево:
Samweli akamwambia, “Ingawa zamani ulijiona mdogo machoni pako mwenyewe, Je, hukuwa kiongozi wa kabila za Israeli? Bwana alikutia mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli.
18 и посла тя Господь путем и рече тебе: иди и искорени Амалика, и погуби согрешших предо Мною, и воюй их, дондеже скончаеши их:
Naye akakutuma kwa kazi maalum, akisema, ‘Nenda ukaangamize kabisa wale watu waovu, wale Waamaleki, upigane nao vita mpaka utakapowaangamiza kabisa.’
19 и почто не послушал еси гласа Господня по всему, елико глагола тебе, но устремился еси на корысти и сотворил еси лукавое пред Господем?
Kwa nini hukumtii Bwana? Kwa nini ulivamia nyara na kufanya uovu machoni pa Bwana?”
20 И рече Саул к Самуилу: послушах гласа людий и идох путем, имже посла мя Господь, и приведох Агага царя Амаликова, и Амалики искорених:
Sauli akasema, “Lakini nilimtii Bwana. Nilikamilisha ile kazi ambayo Bwana alinituma. Niliwaangamiza Waamaleki kabisa na kumleta Agagi mfalme wao.
21 и взяша людие корысти от стад и буйволы, первая от истребляемых на пожрение Господу Богу нашему в Галгалех.
Askari walichukua kondoo na ngʼombe kutoka kwenye nyara, zile ambazo ni nzuri sana zimewekwa wakfu kwa Mungu, ili zitolewe dhabihu kwa Bwana Mungu wako huko Gilgali.”
22 И рече Самуил: еда угодны Господу всесожжения и жертвы, якоже послушати гласа Господня? Се, послушание паче жертвы благи, и покорение паче тука овня:
Lakini Samweli akajibu: “Je, Bwana anafurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama vile kuitii sauti ya Bwana? Kutii ni bora zaidi kuliko dhabihu, nako kusikia ni bora kuliko mafuta ya kondoo dume.
23 якоже грех есть чарование, тако (грех есть) противление, и якоже грех есть идолопоклонение, тако непокорение: понеже уничижил еси глаголгол Господень, и уничижит тя Господь не быти тебе царем во Израили.
Kwa maana kuasi ni kama dhambi ya uaguzi, nao ukaidi ni kama uovu wa kuabudu sanamu. Kwa sababu umelikataa neno la Bwana, naye amekukataa wewe kuendelea kuwa mfalme.”
24 И рече Саул к Самуилу: согреших, яко преступих слово Господне и глагол твой, убояхся бо людий и послушах гласа их:
Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi. Nimevunja amri ya Bwana na maagizo yako. Niliwaogopa watu na kwa hiyo nikafanya walivyotaka.
25 и ныне возми грех мой и возвратися со мною, да поклонюся Господу Богу твоему.
Sasa ninakusihi usamehe dhambi yangu, nawe urudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana.”
26 И рече Самуил к Саулу: не возвращуся с тобою, яко уничижил еси глаголгол Господень, и уничижит тя Господь не быти тебе царем во Израили.
Lakini Samweli akamwambia, “Sitarudi pamoja nawe. Umelikataa neno la Bwana, naye Bwana amekukataa wewe, usiendelee kuwa mfalme juu ya Israeli!”
27 И отврати Самуил лице свое еже отити: и ят Саул за воскрилие ризы его и раздра е.
Samweli alipogeuka ili aondoke, Sauli akangʼangʼania pindo la joho lake, nalo likararuka.
28 И рече ему Самуил: раздра Господь царство Израилево от руку твоею днесь, и даст е ближнему твоему, лучшему паче тебе,
Samweli akamwambia, “Bwana ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako leo, naye ameutia kwa mmoja wa majirani zako, aliye bora kuliko wewe.
29 и разделится Израиль на двое: и не обратится, ниже раскается Святый Израилев, занеже не яко человек есть, еже раскаятися Ему, запретит, и не пребудет.
Yeye aliye Utukufu wa Israeli hasemi uongo wala hana kigeugeu; kwa kuwa yeye si mwanadamu, hata abadili nia yake.”
30 И рече Саул: согреших, но прослави мя ныне пред старейшины Израилевы и пред людьми моими, и возвратися со мною, и поклонюся Господу Богу твоему.
Sauli akajibu, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali niheshimu mbele ya wazee wa watu wangu na mbele ya Israeli; rudi pamoja nami, ili nipate kumwabudu Bwana Mungu wako.”
31 И возвратися Самуил вслед Саула, и поклонися Саул Господу.
Hivyo Samweli akarudi pamoja na Sauli, naye Sauli akamwabudu Bwana.
32 И рече Самуил: приведите ми Агага царя Амаликова. И прииде к нему Агаг трепеща, и рече Агаг: тако ли горька смерть?
Ndipo Samweli akasema, “Niletee Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akaja kwake kwa ujasiri, akifikiri, “Hakika uchungu wa mauti umepita.”
33 И рече Самуил ко агагу: якоже обезчадствова жен оружие твое, тако обезчадится в женах мати твоя. И закла Самуил Агага пред Господем в Галгалех.
Lakini Samweli akasema, “Kama upanga wako ulivyofanya wanawake kufiwa na watoto wao, ndivyo mama yako atakavyokuwa hana mtoto miongoni mwa wanawake.” Naye Samweli akamuua Agagi mbele za Bwana huko Gilgali.
34 И отиде Самуил во Армафем: и Саул отиде в дом свой в Гаваю.
Kisha Samweli akaenda Rama, lakini Sauli akapanda nyumbani kwake huko Gibea ya Sauli.
35 И не приложи Самуил ктому видети Саула даже до дне смерти своея, понеже плакаше Самуил о Сауле, занеже раскаяся Господь, яко постави Саула царя во Израили.
Hadi siku Samweli alipofariki hakwenda kumwona Sauli tena, ingawa Samweli alimwombolezea. Naye Bwana alihuzunika kwamba alimfanya Sauli kuwa mfalme juu ya Israeli.

< Первая книга Царств 15 >