< Титу 2 >

1 А ти говори шта пристоји здравој науци:
Lakini wewe unapaswa kuhubiri mafundisho safi.
2 Старцима да буду трезни, поштени, чисти, здрави у вери, у љубави, у трпљењу;
Waambie wazee kwamba wanapaswa kuwa na kiasi, wawe na busara na wataratibu; wanapaswa kuwa timamu katika imani yao, upendo na uvumilivu.
3 Старицама, такође, да живе као што се пристоји светима, да не буду опадљиве, да се не предају врло вину, да уче добру,
Hali kadhalika waambie wanawake wazee wawe na mwenendo wa uchaji wa Mungu; wasiwe wachongezi, au watumwa wa pombe. Wanapaswa kufundisha mambo mema,
4 Да уче младе да љубе мужеве, да љубе децу,
ili wawazoeze kina mama vijana kuwapenda waume zao na watoto,
5 Да буду поштене, чисте, добре домаћице, благе, покорне својим мужевима, да се не хули на реч Божију.
wawe na kiasi na safi, waangalie vizuri mambo ya nyumbani, na wawatii waume zao, ili ujumbe wa Mungu usije ukadharauliwa.
6 Тако и младиће саветуј да буду поштени.
Kadhalika, wahimize vijana wawe na kiasi.
7 А у свему сам себе подај за углед добрих дела, у науци целост, поштење,
Katika mambo yote wewe mwenyewe unapaswa kuwa mfano wa matendo mema. Uwe mnyofu na uwe na uzito katika mafundisho yako.
8 Реч здраву, незазорну: да се посрами онај који се противи, не имајући ништа зло говорити за нас.
Maneno yako yasiwe na hitilafu yoyote ili adui zako waaibike wasipopata chochote kibaya cha kusema juu yetu.
9 Слуге да слушају своје господаре, да буду угодни у свачему, да не одговарају,
Watumwa wanapaswa kuwatii wakuu wao na kuwapendeza katika mambo yote. Wasibishane nao,
10 Да не краду, него у свачему да показују добру веру, да науку Спаситеља нашег Бога украшују у свачему.
au kuiba vitu vyao. Badala yake wanapaswa kuonyesha kwamba wao ni wema na waaminifu daima, ili, kwa matendo yao yote, wayapatie sifa njema mafundisho juu ya Mungu, Mwokozi wetu.
11 Јер се показа благодат Божја која спасава све људе,
Maana neema ya Mungu imedhihirishwa kwa ajili ya wokovu wa watu wote.
12 Учећи нас да се одрекнемо безбожности и жеља овог света, и да поштено и праведно и побожно поживимо на овом свету, (aiōn g165)
Neema hiyo yatufunza kuachana na uovu wote na tamaa za kidunia; tuwe na kiasi, tuishi maisha adili na ya kumcha Mungu katika ulimwengu huu wa sasa, (aiōn g165)
13 Чекајући блажену наду и јављање славе великог Бога и Спаса нашег Исуса Христа,
tukiwa tunangojea siku ile ya heri tunayoitumainia, wakati utakapotokea utukufu wa Mungu Mkuu na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
14 Који је дао себе за нас да нас избави од сваког безакоња, и да очисти себи народ избрани који чезне за добрим делима.
Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu ili atukomboe kutoka katika uovu wote na kutufanya watu safi walio wake yeye mwenyewe, watu walio na hamu ya kutenda mema.
15 Ово говори, и саветуј, и карај са сваком заповешћу да те нико не презире.
Basi, fundisha mambo hayo na tumia mamlaka yako yote ukiwahimiza na kuwaonya wasikilizaji wako. Mtu yeyote na asikudharau.

< Титу 2 >