< Псалми 137 >
1 На водама вавилонским сеђасмо и плакасмо опомињући се Сиона.
Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
2 О врбама сред њега вешасмо харфе своје.
Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
3 Онде искаху који нас заробише да певамо, и који нас оборише да се веселимо: "Певајте нам песму сионску."
Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
4 Како ћемо певати песму Господњу у земљи туђој?
Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
5 Ако заборавим тебе, Јерусалиме, нека ме заборави десница моја.
Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6 Нека прионе језик мој за уста моја, ако тебе не успамтим, ако не уздржим Јерусалима сврх весеља свог.
Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
7 Напомени, Господе, синовима Едомовим дан јерусалимски, кад говорише: Раскопајте, раскопајте га до темеља.
Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
8 Кћери вавилонска, крвницо, благо ономе ко ти плати за дело које си нама учинила!
Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
9 Благо ономе који узме и разбије децу твоју о камен.
Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.