< 1 Мојсијева 7 >
1 И рече Господ Ноју: Уђи у ковчег ти и сав дом твој; јер те нађох праведна пред собом овог века.
Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
2 Узми са собом од свих животиња чистих по седморо, све мужјака и женку његову; а од животиња нечистих по двоје, мужјака и женку његову,
Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
3 Такође и од птица небеских по седам, мужјака и женку његову, да им се сачува семе на земљи.
Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
4 Јер ћу до седам дана пустити дажд на земљу за четрдесет дана и четрдесет ноћи, и истребићу са земље свако тело живо, које сам створио.
Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
5 И Ноје учини све што му заповеди Господ.
Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
6 А беше Ноју шест стотина година кад дође потоп на земљу.
Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
7 И уђе Ноје у ковчег и синови његови и жена његова и жене синова његових с њим ради потопа.
Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
8 Од животиња чистих и од животиња нечистих и од птица и од свега што се миче по земљи,
Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
9 Уђе к Ноју у ковчег по двоје, мушко и женско, као што беше Бог заповедио Ноју.
wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
10 А у седми дан дође потоп на земљу.
Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
11 Кад је било Ноју шест стотина година, те године другог месеца, седамнаести дан тога месеца, тај дан развалише се сви извори великог бездана, и отворише се уставе небеске;
Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
12 И удари дажд на земљу за четрдесет дана и четрдесет ноћи.
Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
13 Тај дан уђе у ковчег Ноје и Сим и Хам и Јафет, синови Нојеви, и жена Нојева и три жене синова његових с њима;
Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
14 Они, и свакојаке звери по врстама својим, и свакојака стока по врстама својим, и шта се год миче по земљи по врстама својим, и птице све по врстама својим, и шта год лети и има крила,
Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
15 Дође к Ноју у ковчег по двоје од сваког тела, у коме има жива душа,
Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
16 Мушко и женско од сваког тела уђоше, као што беше Бог заповедио Ноју; па Господ затвори за њим.
Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
17 И би потоп на земљи за четрдесет дана; и вода дође и узе ковчег, и подиже га од земље.
Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
18 И навали вода, и уста јако по земљи, и ковчег стаде пловити водом.
Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
19 И наваљиваше вода све већма по земљи, и покри сва највиша брда што су под целим небом.
Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
20 Петнаест лаката дође вода изнад брда, пошто их покри.
Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
21 Тада изгибе свако тело што се мицаше на земљи, птице и стока, и звери и све што гамиже по земљи, и сви људи.
Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
22 Све што имаше душу живу у носу, све што беше на сувом, помре.
Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
23 И истреби се свако тело живо на земљи, и људи и стока и шта год гамиже и птице небеске, све, велим, истреби се са земље; само Ноје оста и шта с њим беше у ковчегу.
Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
24 И стајаше вода поврх земље сто педесет дана.
Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.