< 2 Мојсијева 37 >
1 И начини Веселеило ковчег од дрвета ситима, два и по лакта дуг и подруг лакта широк и подруг лакта висок.
Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
2 И покова га чистим златом изнутра и споља; и начини му златан венац унаоколо.
Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
3 И сали му четири биочуга од злата на четири угла његова: два биочуга с једне стране а два с друге.
Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
4 И начини полуге од дрвета ситима, и окова их златом.
Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
5 И провуче полуге кроз биочуге с обе стране ковчегу, да се може носити ковчег.
Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
6 И начини заклопац од чистог злата, у дужину од два и по лакта, а у ширину од подруг лакта.
Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
7 И начини два херувима од злата, једноставне начини их, на два краја заклопцу,
Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
8 Једног херувима на крају одовуд, а другог херувима на крају одонуд; заклопцу на оба краја начини херувиме.
Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
9 И у херувима беху крила раширена у вис, и заклањаху крилима својим заклопац, и лицем беху окренути један другом, и гледаху према заклопцу херувими.
Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
10 И начини сто од дрвета ситима, у дужину од два лакта а у ширину од лакта, и од подруг лакта у висину.
Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
11 И покова га чистим златом, и начини му венац златан унаоколо.
Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
12 И начини му оплату с подланице унаоколо, и начини венац златан уз оплату унаоколо.
Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
13 И сали му четири биочуга од злата, и метну биочуге на четири угла, који му беху на четири ноге.
Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
14 Према оплати беху биочузи, а у њима полуге, да се може носити сто.
Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
15 А полуге начини од дрвета ситима, и окова их златом, да се може носити сто.
Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
16 И начини од чистог злата посуђе што се меће на сто: зделе и чаше и котлиће и ведра, којим ће се преливати.
Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
17 И начини свећњак од чистог злата, једноставан начини свећњак; ступ му и гране, чашице и јабуке и цветови излажаху из њега.
Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
18 Шест грана излажаху му са страна; три гране свећњака с једне стране а три гране свећњака с друге стране;
Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
19 Три чашице као бадем на једној грани и јабука и цвет, а три чашице као бадем на другој грани и јабука и цвет; тако на свих шест грана које излажаху из свећњака.
Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
20 А на самом свећњаку беху четири чашице као бадем са својим јабукама и цветовима,
Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
21 Једна јабука беше под две гране из њега, и једна јабука под друге две гране из њега, и једна јабука под друге две гране из њега; тако под шест грана које излажаху из њега.
Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
22 Јабуке њихове и гране им излажаху из њега, све беше од чистог злата једноставно.
Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
23 И начини му седам жижака и усекаче и спремице за гар од чистог злата.
Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
24 Од таланта чистог злата начини га са свим справама његовим.
Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
25 И начини олтар кадиони од дрвета ситима у дужину од једног лакта, и у ширину од једног лакта, четвороугласт, и од два лакта у висину; из њега излажаху му рогови.
Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
26 И покова га чистим златом озго и са стране унаоколо, и рогове; и начини му венац од злата унаоколо.
Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
27 И два биочуга од злата начини му испод венца на два угла његова с обе стране, да у њима стоје полуге да се може носити о њима.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
28 А полуге начини од дрвета ситима, и окова их златом.
Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
29 И начини уље за свето помазање и чисти кад мирисни вештином апотекарском.
Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.