< Књига пророка Данила 8 >

1 Треће године царовања Валтасаровог показа се мени Данилу утвара после оне која ми се показала пре.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
2 И видех у утвари; а бејах у Сусану у граду који је у земљи Еламу, кад видех, и видех у утвари и бејах на води Улају.
Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
3 И подигох очи своје и видех, и гле, стајаше крај воде ован, који имаше два рога, а рогови беху високи, али један виши од другог, и виши нарасте после.
Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
4 Видех овна где боде на запад и на север и на југ, и ниједна звер не могаше му одолети, и не беше никога ко би избавио од њега, него чињаше шта хоћаше, и осили.
Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
5 А кад ја мотрах, гле, иђаше јарац од запада поврх све земље, а не дотицаше се земље; и тај јарац имаше рог знаменит међу очима својим.
Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
6 И дође до овна који имаше два рога, ког видех где стоји крај воде, и потрча на њ гневно силом својом.
Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
7 И видех га где дође до овна, и разгневивши се на њ удари овна, те му сломи оба рога и не беше силе у овну да му одоли, него га обори на земљу и погази га, и не беше никога да избави овна од њега.
Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
8 И јарац поста врло велик; а кад осили, сломи се велики рог, и место њега нарастоше знаменита четири рога према четири ветра небеска.
Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
9 И из једног од њих изиђе један рог мален и нарасте врло велик према југу и истоку и према красној земљи.
Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
10 И нарасте дори до војске небеске, и обори на земљу неке од војске и од звезда, и погази их.
Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
11 И нарасте дори до поглавара тој војсци, и узе Му свагдашњу жртву, и свети стан Његов обори.
Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
12 И војска би дана у отпад од жртве свагдашње, и обори истину на земљу, и шта чињаше напредоваше му.
Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
13 Тада чух једног свеца где говораше; и један светац рече некоме који говораше: Докле ће трајати та утвара за свагдашњу жртву и за отпад пустошни да се гази светиња и војска?
Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
14 И рече ми: До две хиљаде и три стотине дана и ноћи; онда ће се светиња очистити.
Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
15 А кад видех ја Данило ову утвару, и заисках да разумем, гле, стаде преда ме као човек.
Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
16 И чух глас човечији насред Улаја, који повика и рече: Гаврило, кажи овоме утвару.
Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
17 И дође где ја стајах; и кад дође уплаших се, и падох на лице своје; а он ми рече: Пази, сине човечији, јер је ова утвара за последње време.
Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
18 А док ми он говораше, ја бејах изван себе лежећи ничице на земљи; а он ме се дотаче, и исправи ме, те стадох.
Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
19 И рече: Ево, ја ћу ти казати шта ће бити на крају гнева; јер ће у одређено време бити крај.
Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
20 Ован што си га видео, који има два рога, то су цареви мидски и персијски.
Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
21 А руњави је јарац цар грчки; и велики рог што му беше међу очима, то је први цар.
Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 А шта се он сломи, и место њега нарастоше четири, то су четири царства, која ће настати иза тог народа, али не његовом силом.
Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
23 А на крају царовања њиховог, кад безаконици наврше меру, настаће цар бестидан и лукав.
Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
24 Сила ће му бити јака, али не од његове јачине, и чудесно ће пустошити, и биће срећан и свршиваће, и губиће силне и народ свети.
Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
25 И лукавством његовим напредоваће превара у његовој руци, и подигнуће се у срцу свом, и у миру ће погубити многе, и устаће на Кнеза над кнезовима, али ће се потрти без руке.
Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
26 А речена утвара о дану и ноћи истина је; зато ти запечати утвару, јер је за много времена.
Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
27 Тада ја Данило занемогох, и боловах неко време; после устах и врших послове цареве; и чудих се утвари, али нико не дозна.
Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.

< Књига пророка Данила 8 >