< Књига пророка Данила 8 >
1 Треће године царовања Валтасаровог показа се мени Данилу утвара после оне која ми се показала пре.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Belshaza, mimi Danieli, nilipata maono, baada ya maono ambayo yalikuwa yamenitokea mbeleni.
2 И видех у утвари; а бејах у Сусану у граду који је у земљи Еламу, кад видех, и видех у утвари и бејах на води Улају.
Katika maono yangu, nilijiona nikiwa ndani ya ngome ya Shushani katika jimbo la Elamu. Katika maono nilikuwa kando ya Mto Ulai.
3 И подигох очи своје и видех, и гле, стајаше крај воде ован, који имаше два рога, а рогови беху високи, али један виши од другог, и виши нарасте после.
Nikatazama juu, na hapo mbele yangu kulikuwa na kondoo dume mwenye pembe mbili, akiwa amesimama kando ya mto, nazo pembe zake zilikuwa ndefu. Pembe moja ilikuwa ndefu kuliko hiyo nyingine, lakini iliendelea kukua baadaye.
4 Видех овна где боде на запад и на север и на југ, и ниједна звер не могаше му одолети, и не беше никога ко би избавио од њега, него чињаше шта хоћаше, и осили.
Nikamtazama yule kondoo dume alivyokuwa akishambulia kuelekea magharibi, kaskazini na kusini. Hakuna mnyama yeyote aliyeweza kusimama dhidi yake, wala hakuna aliyeweza kuokoa kutoka nguvu zake. Alifanya kama atakavyo, naye akawa mkuu.
5 А кад ја мотрах, гле, иђаше јарац од запада поврх све земље, а не дотицаше се земље; и тај јарац имаше рог знаменит међу очима својим.
Nilipokuwa ninatafakari hili, ghafula beberu mwenye pembe moja kubwa sana katikati ya macho yake alikuja kutoka magharibi, akiruka kasi juu ya dunia yote bila kugusa ardhi.
6 И дође до овна који имаше два рога, ког видех где стоји крај воде, и потрча на њ гневно силом својом.
Alikuja akimwelekea yule kondoo dume mwenye pembe mbili niliyemwona akisimama kando ya mto, akamshambulia kwa hasira nyingi.
7 И видех га где дође до овна, и разгневивши се на њ удари овна, те му сломи оба рога и не беше силе у овну да му одоли, него га обори на земљу и погази га, и не беше никога да избави овна од њега.
Nikamwona akimshambulia yule kondoo dume kwa hasira nyingi, akimpiga yule kondoo dume na kuvunja pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuwa na nguvu za kumzuia yule beberu, hivyo akamwangusha yule kondoo dume chini na kumkanyaga, wala hakuna aliyeweza kumwokoa yule kondoo dume kutoka nguvu za huyo beberu.
8 И јарац поста врло велик; а кад осили, сломи се велики рог, и место њега нарастоше знаменита четири рога према четири ветра небеска.
Yule beberu akawa mkubwa sana, lakini katika kilele cha nguvu zake ile pembe yake ndefu ilivunjika, na mahali pake pakaota pembe nne kubwa kuelekea pande nne za dunia.
9 И из једног од њих изиђе један рог мален и нарасте врло велик према југу и истоку и према красној земљи.
Kutoka mojawapo ya zile pembe nne palitokea pembe ndogo ukaongezeka nguvu kuelekea kusini, na kuelekea mashariki, na kuelekea Nchi ya Kupendeza.
10 И нарасте дори до војске небеске, и обори на земљу неке од војске и од звезда, и погази их.
Pembe hiyo ikaendelea kukua hadi kufikia jeshi la mbinguni, nayo ikalitupa baadhi ya jeshi la vitu vya angani hapa chini duniani, na kulikanyaga.
11 И нарасте дори до поглавара тој војсци, и узе Му свагдашњу жртву, и свети стан Његов обори.
Pembe hiyo ikajikweza ili iwe kama Mkuu wa hilo jeshi; ikamwondolea dhabihu ya kila siku, napo mahali pake patakatifu pakashushwa chini.
12 И војска би дана у отпад од жртве свагдашње, и обори истину на земљу, и шта чињаше напредоваше му.
Kwa sababu ya uasi, jeshi la watakatifu na dhabihu za kila siku vikatiwa mikononi mwake. Ikafanikiwa katika kila kitu ilichofanya, nayo kweli ikatupwa chini.
13 Тада чух једног свеца где говораше; и један светац рече некоме који говораше: Докле ће трајати та утвара за свагдашњу жртву и за отпад пустошни да се гази светиња и војска?
Kisha nikamsikia mtakatifu mmoja akizungumza na mtakatifu mwingine, akamwambia, “Je, itachukua muda gani maono haya yatimie: maono kuhusu dhabihu ya kila siku, uasi unaosababisha ukiwa, kutwaliwa kwa mahali patakatifu, na jeshi litakalokanyagwa chini ya nyayo?”
14 И рече ми: До две хиљаде и три стотине дана и ноћи; онда ће се светиња очистити.
Akaniambia, “Itachukua siku 2,300. Ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.”
15 А кад видех ја Данило ову утвару, и заисках да разумем, гле, стаде преда ме као човек.
Mimi Danieli nilipokuwa ninaangalia maono na kujaribu kuelewa, mbele yangu alisimama mmoja aliyefanana na mwanadamu.
16 И чух глас човечији насред Улаја, који повика и рече: Гаврило, кажи овоме утвару.
Kisha nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka Mto Ulai ikiita, “Gabrieli, mwambie mtu huyu maana ya maono haya.”
17 И дође где ја стајах; и кад дође уплаших се, и падох на лице своје; а он ми рече: Пази, сине човечији, јер је ова утвара за последње време.
Alipokuwa akikaribia pale nilipokuwa nimesimama, niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Akaniambia, “Mwana wa mwanadamu, fahamu kuwa maono haya yanahusu siku za mwisho.”
18 А док ми он говораше, ја бејах изван себе лежећи ничице на земљи; а он ме се дотаче, и исправи ме, те стадох.
Alipokuwa akinena nami, nilikuwa katika usingizi mzito, huku nimelala kifudifudi. Ndipo aliponigusa na kunisimamisha wima.
19 И рече: Ево, ја ћу ти казати шта ће бити на крају гнева; јер ће у одређено време бити крај.
Akaniambia, “Nitakuambia yale yatakayotokea baadaye wakati wa ghadhabu, kwa sababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho ulioamriwa.
20 Ован што си га видео, који има два рога, то су цареви мидски и персијски.
Kondoo dume mwenye pembe mbili ambaye ulimwona anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi.
21 А руњави је јарац цар грчки; и велики рог што му беше међу очима, то је први цар.
Yule beberu mwenye nywele nyingi ni mfalme wa Uyunani, nayo ile pembe ndefu katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 А шта се он сломи, и место њега нарастоше четири, то су четири царства, која ће настати иза тог народа, али не његовом силом.
Zile pembe nne zilizoota badala ya ile pembe iliyovunjika zinawakilisha falme nne ambazo zitatokea kutoka taifa lake, lakini hakuna hata mmoja utakaokuwa na nguvu kama ule uliovunjika.
23 А на крају царовања њиховог, кад безаконици наврше меру, настаће цар бестидан и лукав.
“Katika sehemu ya mwisho ya utawala wao, wakati waasi watakapokuwa waovu kabisa, atainuka mfalme mwenye uso mkali, aliye stadi wa hila.
24 Сила ће му бити јака, али не од његове јачине, и чудесно ће пустошити, и биће срећан и свршиваће, и губиће силне и народ свети.
Atakuwa na nguvu nyingi, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe. Atasababisha uharibifu wa kutisha, na atafanikiwa kwa chochote anachofanya. Atawaangamiza watu maarufu na watu watakatifu.
25 И лукавством његовим напредоваће превара у његовој руци, и подигнуће се у срцу свом, и у миру ће погубити многе, и устаће на Кнеза над кнезовима, али ће се потрти без руке.
Atasababisha udanganyifu ustawi, naye atajihesabu mwenyewe kuwa bora. Wakati wajisikiapo kuwa wako salama, atawaangamiza wengi, na kushindana na Mkuu wa wakuu. Lakini ataangamizwa, isipokuwa si kwa uwezo wa mwanadamu.
26 А речена утвара о дану и ноћи истина је; зато ти запечати утвару, јер је за много времена.
“Maono kuhusu jioni na asubuhi ambayo umepewa ni kweli, lakini yatie muhuri maono haya, kwa maana yanahusu wakati mrefu ujao.”
27 Тада ја Данило занемогох, и боловах неко време; после устах и врших послове цареве; и чудих се утвари, али нико не дозна.
Mimi Danieli nilikuwa nimechoka sana, na nikalala nikiwa mgonjwa kwa siku kadhaa. Ndipo nikaamka, nikaenda kwenye shughuli za mfalme. Nilifadhaishwa na maono hayo, nami sikuweza kuyaelewa.