< 2 Књига Самуилова 4 >
1 А кад чу син Саулов да је погинуо Авенир у Хеврону, клонуше му руке, и сав се Израиљ смете.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli aliposikia kwamba Abneri amekufa huko Hebroni, akakosa ujasiri, nayo Israeli yote wakatiwa hofu kuu.
2 А имаше син Саулов две војводе над четама; једном беше име Вана, другом беше име Рихав, синови Римона Вироћанина, од синова Венијаминових; јер се и Вирот бројаше Венијамину;
Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili waliokuwa viongozi wa vikundi vya uvamizi. Mmoja aliitwa Baana na mwingine Rekabu, waliokuwa wana wa Rimoni, Mbeerothi, kutoka kabila la Benyamini. Beerothi alihesabiwa kuwa sehemu ya Benyamini,
3 А Вироћани беху побегли у Гитајим, где осташе као дошљаци до данашњег дана.
kwa sababu watu wa Beerothi walikimbilia huko Gitaimu na wameishi huko kama wageni mpaka siku hii ya leo.
4 И имаше Јонатан, син Саулов, сина хромог на ногу, коме беше пет година кад дође глас о смрти Сауловој и Јонатановој из Језраела, те га узе дадиља његова и побеже, и кад брзо бежаше, он паде и охрону; а име му беше Мефивостеј.
(Yonathani mwana wa Sauli alikuwa na mwana aliyekuwa mlemavu miguu yote miwili. Alikuwa na miaka mitano wakati habari kuhusu Sauli na Yonathani zilipofika kutoka Yezreeli. Yaya wake akambeba ili kukimbia, lakini yaya alipokuwa anaharakisha kuondoka, mtoto alianguka akawa kiwete. Jina lake aliitwa Mefiboshethi.)
5 И пођоше синови Римона Вироћанина, Рихав и Вана, и дођоше у подне у кућу Исвостејеву; а он почиваше у подне.
Basi Rekabu na Baana, wana wa Rimoni Mbeerothi wakaenda nyumbani kwa Ish-Boshethi, nao walifika huko wakati alipokuwa kwenye mapumziko yake ya mchana.
6 И уђоше у кућу као да узму пшенице, и прободоше га под пето ребро Рихав и Вана, и побегоше.
Wakaingia kwenye chumba cha ndani kana kwamba wanachukua ngano, wakamchoma Ish-Boshethi mkuki wa tumboni. Ndipo Rekabu na Baana nduguye wakatoroka.
7 Кад уђоше у кућу, он лежаше на постељи својој у клети где спаваше, те га прободоше и убише, и одсекоше му главу и узеше је, па отидоше путем преко поља целу ону ноћ.
Walikuwa wameingia ndani ya nyumba wakati alipokuwa amelala kitandani chumbani kwake. Baada ya kumchoma mkuki na kumuua, walikata kichwa chake. Wakiwa wamekichukua, walitembea usiku kucha kwa njia ya Araba.
8 И донесоше главу Исвостејеву Давиду у Хеврон, и рекоше цару: Ево главе Исвостеја сина Сауловог, непријатеља твог, који је тражио душу твоју; и Господ освети данас цара, господара мог, од Саула и семена његовог.
Wakamletea Daudi kichwa cha Ish-Boshethi huko Hebroni, wakamwambia mfalme, “Hiki hapa kichwa cha Ish-Boshethi mwana wa Sauli, adui yako, aliyejaribu kuondoa uhai wako. Siku hii ya leo Bwana amemlipia kisasi mfalme bwana wangu dhidi ya Sauli na mzao wake.”
9 Али Давид одговарајући Рихаву и Вану, брату његовом, синовима Римона Вироћанина, рече им: Тако да је жив Господ, који је избавио душу моју из сваке невоље.
Daudi akawajibu Rekabu na Baana nduguye, wana wa Rimoni, Mbeerothi, akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka taabu zote,
10 Кад оног који ми јави говорећи: Гле, погибе Саул, и мишљаше да ће ми јавити добре гласе, ухватих и убих у Сиклагу, и то му би од мене дар за гласе његове,
yule mtu aliponiambia, ‘Sauli amekufa,’ akadhani ananiletea habari njema, nilimkamata, nikamuua huko Siklagi. Hiyo ndiyo zawadi niliyompa kwa ajili ya taarifa yake!
11 А камоли људе безбожне, који убише човека правог, у кући његовој, на постељи његовој! Нећу ли тражити крв његову из ваших руку, и вас истребити са земље?
Je, ni mara ngapi zaidi wakati watu waovu wamemuua mtu asiye na hatia akiwa ndani ya nyumba yake mwenyewe na kwenye kitanda chake mwenyewe? Je, sasa nisidai damu yake mikononi mwenu na kuwaondoa duniani?”
12 И заповеди Давид момцима својим, те их погубише, и одсекоше им руке и ноге, и обесише код језера хевронског; а главу Исвостејеву узеше и погребоше у гробу Авенировом у Хеврону.
Kwa hiyo Daudi akawaamuru watu wake, wakawaua. Wakakata mikono yao na miguu, na kutundika viwiliwili vyao kando ya dimbwi huko Hebroni. Lakini wakakichukua kichwa cha Ish-Boshethi na kukizika katika kaburi la Abneri huko Hebroni.