< 2 Књига Самуилова 21 >

1 И би глад за времена Давидовог три године заредом. И Давид потражи лице Господње; а Господ му рече: То је са Саула и с дома његовог крвничког, што погуби Гаваоњане.
Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
2 Тада цар сазва Гаваоњане и говори им. А Гаваоњани не беху од синова Израиљевих, него остатак од Амореја, којима се беху заклели синови Израиљеви, али Саул гледаше да их побије ревнујући за синове Израиљеве и Јудине.
Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
3 И рече Давид Гаваоњанима: Шта да вам учиним и чим да вас намирим, да благословите достојање Господње?
Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
4 А Гаваоњани му рекоше: Не тражимо ни сребро ни злато од Саула или од дома његовог, нити да се ко погуби у Израиљу. А он рече: Шта дакле велите да вам учиним?
Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
5 Тада рекоше цару: Ко нас је потро и радио да нас истреби, да нас не буде нигде у међама Израиљевим,
Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
6 Од његових синова нека нам се да седам људи да их обесимо Господу у Гаваји Саула изабраника Господњег. И рече цар: Ја ћу дати.
tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
7 Али цар поштеде Мефивостеја сина Јонатана сина Сауловог ради заклетве Господње, која би међу њима, међу Давидом и Јонатаном сином Сауловим.
Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
8 И узе цар два сина Ресфе, кћери Ајине, које роди Саулу, Армонија и Мефивостеја, и пет синова Михале кћери Саулове, које роди Адрилу сину Варзелаја Меолаћанина.
Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
9 И даде их у руке Гаваоњанима, а они их обесише на гори пред Господом; и сва седморица погибоше заједно; а бише убијени првих дана жетве, у почетку јечмене жетве.
Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
10 А Ресфа кћи Ајина узе врећу, и простре по стени у почетку жетве докле не паде на њих дажд са неба, и не даде птицама небеским да падају на њих дању ни зверима пољским ноћу.
Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
11 И јавише Давиду шта учини Ресфа кћи Ајина, иноча Саулова.
Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
12 И Давид отиде те узе кости Саулове и кости Јонатана сина његовог од грађана у Јавису Галадовом, који их беху украли с улице вет-санске, где их обесише Филистеји кад убише Филистеји Саула на Гелвуји.
alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
13 И однесе оданде кости Саулове и кости Јонатана сина његовог, па скупише и кости обешених.
Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
14 И погребоше их с костима Сауловим и Јонатана сина његовог у земљи Венијаминовој у Сили, у гробу Киса оца његовог, и учинише све како заповеди цар. Тако се после тога умилостиви Господ земљи.
Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
15 И наста опет рат између Филистеја и Израиља, и Давид отиде са слугама својим, и тукоше се с Филистејима тако да Давид суста.
Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
16 Тада Јесви-Венов, који беше од синова Рафајевих, и у копљу му беше триста сикала бронзе, и имаше ново оружје, хтеде да убије Давида.
Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
17 Али му поможе Ависај, син Серујин, и удари Филистејина и уби га. Тада се заклеше људи Давидови рекавши му: Нећеш више ићи с нама у бој да не угасиш видело Израиљево.
Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
18 После тога наста опет рат с Филистејима у Гову; и тада Сивехај Хусаћанин уби Сафа, који беше од синова Рафајевих.
Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
19 И опет наста други рат у Гову с Филистејима; и тада Елханан, син Јаре-Орегимов Витлејемац, уби брата Голијата Гетејина, коме копљача беше као вратило.
Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
20 И опет наста рат у Гату, где беше један човек врло висок, који имаше по шест прста на рукама и на ногама, свега двадесет и четири, и он беше такође рода Рафајевог.
Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
21 И ружаше Израиља те га уби Јонатан, син Саме, брата Давидовог.
Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
22 Та четворица беху синови истог Рафаја из Гата, и погибоше од руке Давидове и од руке слуга његових.
Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.

< 2 Књига Самуилова 21 >