< 2 Књига о царевима 16 >

1 Године седамнаесте Фекаја сина Ремалијиног зацари се Ахаз син Јотамов цар Јудин.
Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Двадесет година беше Ахазу кад поче царовати, и царова шеснаест година у Јерусалиму, али не чињаше што је право пред Господом Богом његовим као Давид отац његов.
Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake.
3 Јер хођаше путем царева Израиљевих, па и сина свог пусти кроз огањ по гадним делима народа које одагна Господ испред синова Израиљевих.
Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli.
4 И приношаше жртве и кађаше на висинама и по хумовима и под сваким зеленим дрветом.
Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.
5 Тада дође Ресин, цар сирски и Фекај, син Ремалијин цар Израиљев, дођоше да бију Јерусалим, и опколише Ахаза; али га не могоше освојити.
Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda.
6 У то време Ресин цар сирски поврати Сирцима Елат, и изагна Јудеје из Елата, и дођоше Сирци у Елат и осташе онде до данас.
Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.
7 Али Ахаз посла посланике к Теглат-Феласару цару асирском у поручи му: Слуга сам твој, ходи и избави ме из руку цара сирског и из руку цара Израиљевог, који се подигоше на ме.
Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.”
8 И узе Ахаз злато и сребро што се нађе у дому Господњем и у ризницама дома царског, и посла на дар цару асирском.
Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
9 И послуша га цар асирски, и дође на Дамаск и узе га, и пресели народ оданде у Кир, а Ресина погуби.
Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.
10 Тада цар Ахаз отиде на сусрет Теглат-Феласару цару асирском у Дамаск; и виде цар Ахаз олтар који беше у Дамаску, па посла свештенику Урији слику од тог олтара и од све направе његове.
Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake.
11 И начини свештеник Урија олтар сасвим како посла цар Ахаз из Дамаска, онако начини Урија свештеник, докле се врати цар Ахаз из Дамаска.
Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi.
12 Па кад се цар врати из Дамаска и виде олтар, приступи к њему и принесе жртву на њему.
Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake.
13 И запали жртву своју паљеницу и дар свој, и изли налив свој, и покропи олтар крвљу захвалних жртава својих.
Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu.
14 А бронзани олтар што беше пред Господом пренесе с предње стране дома да не стоји између његовог олтара и дома Господњег, и намести га покрај свог олтара к северу.
Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.
15 И заповеди цар Ахаз Урији свештенику говорећи: На великом олтару пали жртву паљеницу јутарњу и дар вечерњи и жртву паљеницу цареву с даром њеним и жртву паљеницу свега народа земаљског с даровима њиховим и наливима њиховим; и по њему кропи сваком крвљу од жртава паљеница и сваком крвљу од других жртава. А за олтар бронзани промислићу.
Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.”
16 И учини свештеник Урија све како му заповеди цар Ахаз.
Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.
17 И оплате с подножја скиде цар Ахаз и узе с њих умиваонице, и море скиде с волова бронзаних који беху под њим, и метну га на под камени.
Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe.
18 И стреху суботну, коју беху начинили у дому, и улазак царски, који беше споља, уклони такође од дома Господњег, бојећи се цара асирског.
Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.
19 А остала дела Ахазова што је чинио, нису ли записана у дневнику царева Јудиних?
Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 И почину Ахаз код отаца својих, и би погребен код отаца својих у граду Давидовом; а на његово се место зацари Језекија, син његов.
Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Књига о царевима 16 >