< 1 Књига о царевима 6 >

1 Четири стотине и осамдесете године по изласку синова Израиљевих из земље мисирске, четврте године царовања Соломуновог над Израиљем, месеца Зифа, а то је други месец, поче зидати дом Господу.
Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.
2 А дом што га зида цар Соломун Господу беше у дужину од шездесет лаката, а у ширину од двадесет лаката, а у висину од тридесет лаката.
Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini, upana wa dhiraa ishirini na kimo cha dhiraa thelathini kwenda juu.
3 И беше трем пред црквом двадесет лаката дуг, према ширини дома, а десет лаката широк пред домом.
Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu.
4 И начини прозоре на дому изнутра широке, а споља уске.
Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu.
5 И уза зид дому начини ходнике свуда унаоколо уза зид дому око цркве и светиње над светињама, и начини клети свуда унаоколо.
Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu.
6 Најдоњи ходник беше пет лаката широк, а средњи шест лаката широк, а трећи седам лаката широк; јер начини засеке на дому споља унаоколо, да се греде не улежу у зид од дома.
Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano, ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.
7 А кад зидаху дом, зидаху од камена, који довожаху сасвим приготовљен, те се ни чекић ни секира нити какво оруђе гвоздено не чу у дому кад се зидаше.
Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.
8 Врата од средњег ходника беху на десној страни дома, и излажаше се на завојницу на средњи ходник, и из средњег на трећи.
Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu.
9 Тако сазида дом, и доврши га, и покри дом гредама и даскама кедровим.
Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi.
10 И начинише ходнике око целог дома од пет лаката у висину сваки, и састављаху их с домом греде кедрове.
Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.
11 Тада дође реч Господња Соломуну говорећи:
Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema:
12 То је дом што градиш; ако узидеш по мојим уредбама, и уствориш моје законе и уздржиш све моје заповести ходећи по њима, потврдићу ти реч своју, коју сам рекао Давиду оцу твом.
“Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako.
13 И становаћу међу синовима Израиљевим, и нећу оставити народ свој Израиља.
Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”
14 И тако сазида Соломун дом, и доврши га.
Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha.
15 И обложи зидове дому изнутра даскама кедровим, од пода дома до врха зидова обложи дрветом изнутра; и под дому обложи даскама јеловим.
Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari.
16 И начини преграду од двадесет лаката од једне стране дома до друге од дасака кедрових, од пода до врх зидова; и то начини унутра за шатор, за светињу над светињама.
Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu.
17 А дом, црква напред, беше од четрдесет лаката.
Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.
18 А по даскама кедровим унутра у дому беху изрезане јабуке и цветови развијени, све од кедра тако да се не виђаше нигде камен.
Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.
19 И светињу над светињама уреди унутра у дому, да се онде намести ковчег завета Господњег.
Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana.
20 А светиња над светињама унутра беше двадесет лаката дуга, и двадесет лаката широка, и двадесет лаката висока, и обложи је чистим златом; тако обложи и олтар од кедра.
Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo.
21 И тако обложи Соломун дом изнутра чистим златом, и затеже златне ланце пред светињом над светињама, коју такође обложи златом.
Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu.
22 И сав дом обложи златом; тако и сав олтар пред светињом над светињама обложи златом.
Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.
23 А у светињи над светињама начини два херувима од дрвета маслиновог; десет лаката беше висок сваки.
Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi kwenda juu.
24 А од пет лаката беше једно крило у херувима, и од пет лаката беше друго крило у херувима; десет лаката беше од краја једног крила до краја другог крила.
Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi.
25 Тако и други херувим беше од десет лаката; једне мере и једне направе беху оба херувима.
Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo.
26 Десет лаката беше висок један херувим, тако и други.
Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi.
27 И намести херувиме усред унутрашњег дома, и раширише херувими крила своја тако да крило једног тицаше у један зид, а крило другог херувима тицаше у други зид, а усред дома тицаху крила једно у друго.
Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba.
28 И обложи херувиме златом.
Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.
29 А све зидове дому унаоколо искити резаним херувимима и палмама и развијеним цветовима изнутра и споља.
Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua.
30 И под дому обложи златом изнутра и споља.
Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.
31 И на уласку у светињу над светињама начини двокрилна врата од дрвета маслиновог, којима прагови с довратницима беху на пет углова.
Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano.
32 И на тим двокрилним вратима од дрвета маслиновог изреза херувиме и палме и развијене цветове, и обложи их златом, и херувиме и палме обложи златом.
Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa.
33 Тако и на уласку у цркву начини прагове од дрвета маслиновог на четири угла;
Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa.
34 И врата двокрилна од дрвета јеловог; на две се стране отвараше једно крило, и на две стране отвараше се друго крило.
Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine.
35 И изреза на њима херувиме и палме и развијене цветове, и обложи златом све што беше изрезано.
Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.
36 Потом начини трем унутрашњи од три реда тесаног камена и једног реда дрвета кедровог струганог.
Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.
37 Четврте године месеца Зифа би постављен темељ дому Господњем;
Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano.
38 А једанаесте године месеца Вула, који је осми месец, сврши се дом са свим стварима својим и са свим што му припада. Тако га сазида за седам година.
Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.

< 1 Књига о царевима 6 >