< Psalmi 96 >
1 Pjevajte Gospodu pjesmu novu, pjevaj Gospodu, sva zemljo!
Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
2 Pjevajte Gospodu, blagosiljajte ime njegovo, javljajte od dana na dan spasenje njegovo.
Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
3 Kazujte po narodima slavu njegovu, po svijem plemenima èudesa njegova.
Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
4 Jer je velik Gospod i valja ga hvaliti: strašniji je od svijeh bogova.
Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
5 Jer su svi bogovi u naroda ništa: a Gospod je nebesa stvorio.
Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
6 Slava je i velièanstvo pred licem njegovijem, (sila) i krasota u svetinji njegovoj.
Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
7 Dajte Gospodu, plemena narodna, dajte Gospodu slavu i èast.
Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
8 Dajte Gospodu slavu prema imenu njegovu. Nosite dare i idite u dvore njegove.
Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
9 Poklonite se Gospodu u svetoj krasoti. Strepi pred njim, sva zemljo!
Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
10 Recite narodima: Gospod caruje; zato je vasiljena tvrda i neæe se pomjestiti; on æe suditi narodima pravo.
Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
11 Nek se vesele nebesa, i zemlja se raduje; nek pljeska more i što je u njemu;
Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
12 Neka skaèe polje i sve što je na njemu; tada nek se raduju sva drveta šumska
Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
13 Pred licem Gospodnjim; jer ide, jer ide da sudi zemlji. Sudiæe vasiljenoj po pravdi, i narodima po istini svojoj.
mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.