< Psalmi 71 >
1 U tebe se, Gospode, uzdam, nemoj me ostaviti pod sramotom vjeènom.
Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
2 Pravdom svojom izbavi me, i oprosti me, prigni k meni uho svoje i pomozi mi.
Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
3 Budi mi grad gdje bih svagda dolazio da živim, uredi spasenje moje; jer si ti grad moj i krjepost moja.
Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 Bože moj! uzmi me iz ruke bezbožnikove, iz ruke bezakonikove i nasilnikove.
Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
5 Jer si ti nadanje moje, Gospod je Gospod pouzdanje moje od mladosti moje.
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
6 Tebe se držim od roðenja, od utrobe matere moje ti si braniè moj; tobom se hvalim svagda.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
7 Èudo sam mnogima, a ti si utoèište moje jako.
Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 Usta su moja puna hvale tvoje, slave tvoje svaki dan.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
9 Nemoj me odbaciti pod starost, kad me izdaje snaga moja, nemoj me ostaviti.
Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
10 Jer neprijatelji moji misle o meni, i koji vrebaju dušu moju dogovaraju se,
Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
11 Govoreæi: Bog ga je ostavio, potjerajte i uhvatite ga, jer ga nema ko izbaviti.
Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
12 Bože! Ne budi daleko od mene; Bože moj! pohitaj mi u pomoæ.
Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
13 Nek se postide i poginu protivnici duše moje; neka popadne stid i sramota na one koji mi traže zla!
Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
14 A ja æu se svagda uzdati, i ponavljaæu hvale tebi.
Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
15 Usta æe moja kazivati pravdu tvoju, svaki dan dobroèinstva tvoja, jer im ne znam broja.
Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
16 Uæi æu u sili Gospoda Gospoda, i slaviæu samo tvoju pravdu.
Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
17 Bože! ti si me uèio od mladosti, i do danas kazujem èudesa tvoja.
Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 Ni u starosti i kad osijedjeh nemoj me ostaviti, Bože, eda bih kazivao mišicu tvoju natražju, svoj omladini silu tvoju.
Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
19 Pravda je tvoja, Bože, do najviše visine; u velikim djelima, koja si uèinio, Bože, ko je kao ti?
Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 Koliko si me puta bacao u velike i ljute nevolje, pak si me opet ostavio meðu živima i iz bezdana me zemaljskih opet izvadio.
Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
21 Mnogo si me puta podizao i ponavljao utjehe.
Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
22 I ja te hvalim uz psaltir, tvoju vjernost, Bože moj; udaram ti u gusle, sveèe Izrailjev!
Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
23 Raduju se usta moja kad pjevam tebi, i duša moja, koju si izbavio.
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
24 I jezik moj svaki dan kazuje pravdu tvoju; jer su postiðeni i posramljeni koji mi traže zla.
Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.