< Psalmi 57 >
1 Smiluj se na me, Bože, smiluj se na me; jer se u tebe uzda duša moja, i pod sjen krila tvojih sklanjam se dok ne proðu nevolje.
Unihurumie, Mungu, unihurumie mimi, kwa maana ninakukimbilia wewe mpaka matatizo haya yaishe. Ninakaa chini ya mbawa za zako kwa ajili ya ulinzi mpaka huu uharibifu utakapoisha.
2 Prizivam Boga višnjega, Boga, koji mi dobro èini;
Nitakulilia Mungu uliye hai, kwa Mungu, afanyaye mambo yote kwa ajili yangu.
3 Da pošlje s neba i saèuva me, da posrami onoga koji traži da me proždre; da pošlje Bog milost svoju i istinu svoju.
Yeye atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa, ana hasira na wale wanaonishambulia. (Selah) Mungu atanitumia upendo wake mwema na uaminifu wake.
4 Duša je moja meðu lavovima, ležim meðu onima koji dišu plamenom. Zubi su sinova ljudskih koplja i strijele, i njihov jezik maè oštar.
Uhai wangu uko katikati ya simba; niko katikati ya wale walio tayari kunila. Niko katikati ya watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, na ambao ndimi zao ni kali kama upanga.
5 Uzvisi se više nebesa, Bože, po svoj zemlji neka bude slava tvoja!
Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu, utukufu wako uwe juu ya nchi yote.
6 Metnuše zamku nogama mojima, i stegoše dušu moju, iskopaše preda mnom jamu, i sami padoše u nju.
Wao walisambaza nje wavu kwa ajili ya miguu yangu; nilikuwa na shida sana. Walichimba shimo mbele yangu. Wao wenyewe wameangukia katikati ya shimo! (Selah)
7 Utvrdilo se srce moje, Bože, utvrdilo se srce moje; pjevaæu te i slaviæu.
Moyo wangu umeponywa, Mungu, moyo wangu umeponywa, nitaimba, ndiyo, nitaimba sifa.
8 Probudi se, slavo moja, probudi se, psaltire i gusle; ustaæu rano.
Inuka, moyo wa thamani; inuka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
9 Hvaliæu Gospoda po narodima, pjevaæu ti po plemenima.
Nitakushukuru wewe, Bwana, kati ya watu; Kati ya mataifa nitakuimbia sifa.
10 Jer je velika do nebesa milost tvoja, i istina tvoja do oblaka.
Maana upendo wako usiokwisha, huzifikia mbingu; na uaminifu wako mawinguni.
11 Uzvisi se više nebesa, Bože, po svoj zemlji neka bude slava tvoja!
Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu; na utukufu wako uinuliwe juu ya nchi yote.