< Psalmi 36 >

1 Bezakoniku je bezbožna rijeè u srcu; nema straha Božijega pred oèima njegovijem.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 Ali laže sebi u oèi, mjesto da prizna svoje bezakonje i omrzne na nj.
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3 Rijeèi su usta njegovijeh nepravda i lukavstvo, neæe da se opameti da tvori dobro.
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 Bezakonje smišlja na postelji svojoj, stoji na putu rðavom, zlo mu nije mrsko.
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
5 Gospode! do neba je milost tvoja, i istina tvoja do oblaka.
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
6 Pravda je tvoja kao gore Božije, sudovi tvoji bezdana velika; ljude i stoku ti èuvaš, Gospode!
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
7 Kako je dragocjena milost tvoja, Bože! sinovi ljudski u sjenu krila tvojih ne boje se.
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 Hrane se od izobila doma tvojega, i iz potoka sladosti svojih ti ih napajaš.
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 Jer je u tebe izvor životu, tvojom svjetlošæu vidimo svjetlost.
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
10 Raširi milost svoju na one koji te znadu, i pravdu svoju na dobra srca.
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11 Ne daj da stane na mene noga ohola, i ruka bezbožnièka da me zaljulja.
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12 Onamo neka padnu koji èine bezakonje, neka se stropoštaju i ne mogu ustati.
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!

< Psalmi 36 >