< Psalmi 26 >

1 Sudi mi, Gospode, jer u prostoti svojoj hodim i u Gospoda se uzdam; neæu se pokolebati.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2 Ispitaj me, Gospode, i iskušaj me; pretopi što je u meni i srce moje.
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3 Jer je milost tvoja pred oèima mojima, i hodim u istini tvojoj.
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4 Ne sjedim s bezumnicima, i s lukavima se ne miješam.
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5 Nenavidim društvo bezakonièko, i s bezbožnicima ne sjedim.
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 Umivam pravdom ruke svoje, i idem oko žrtvenika tvojega, Gospode,
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 Da razglašujem hvalu tvoju i kazujem sva èudesa tvoja.
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 Gospode! omilio mi je stan doma tvojega, i mjesto naselja slave tvoje.
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9 Nemoj duše moje pogubiti, ni života mojega s krvopilcima,
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10 Kojima je zloèinstvo u rukama, i kojima je desnica puna mita.
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 A ja hodim u prostoti svojoj, izbavi me, i smiluj se na me.
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12 Noga moja stoji na pravom putu; na skupštinama æu blagosiljati Gospoda.
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.

< Psalmi 26 >