< Poslovice 6 >

1 Sine moj, kad se podjemèiš za prijatelja svojega, i daš ruku svoju tuðincu,
Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
2 Vezao si se rijeèima usta svojih, uhvatio si se rijeèima usta svojih.
kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
3 Zato uèini tako, sine moj, i oprosti se, jer si dopao u ruke bližnjemu svojemu; idi, pripadni, i navali na bližnjega svojega.
basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
4 Ne daj sna oèima svojima, ni vjeðama svojima drijema.
Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
5 Otmi se kao srna iz ruke lovcu, i kao ptica iz ruke ptièaru.
Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
6 Idi k mravu, ljenivèe, gledaj putove njegove, i omudraj.
Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
7 Nema voða ni upravitelja ni gospodara;
Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
8 I opet pripravlja ljeti sebi hranu, zbira uz žetvu piæu svoju.
lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9 Dokle æeš, ljenivèe, ležati? kad æeš ustati od sna svojega?
Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
10 Dok malo prospavaš, dok malo prodrijemlješ, dok malo sklopiš ruke da prilegneš,
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
11 Utom æe doæi siromaštvo tvoje kao putnik i oskudica tvoja kao oružan èovjek.
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
12 Èovjek nevaljao i nitkov hodi sa zlijem ustima;
Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
13 Namiguje oèima, govori nogama, pokazuje prstima;
ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
14 Svaka mu je opaèina u srcu, kuje zlo svagda, zameæe svaðu.
ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
15 Zato æe ujedanput doæi pogibao njegova, èasom æe se satrti i neæe biti lijeka.
Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
16 Na ovo šestoro mrzi Gospod, i sedmo je gad duši njegovoj:
Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
17 Oèi ponosite, jezik lažljiv i ruke koje proljevaju krv pravu,
macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
18 Srce koje kuje zle misli, noge koje brzo trèe na zlo,
moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
19 Lažan svjedok koji govori laž, i ko zameæe svaðu meðu braæom.
shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
20 Èuvaj, sine moj, zapovijest oca svojega, i ne ostavljaj nauke matere svoje.
Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 Priveži ih sebi na srce zasvagda, i spuèi ih sebi oko grla.
Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
22 Kuda god poðeš, vodiæe te; kad zaspiš, èuvaæe te; kad se probudiš, razgovaraæe te;
Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
23 Jer je zapovijest žižak, i nauka je vidjelo, i put je životni karanje koje pouèava;
Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
24 Da te èuvaju od zle žene, od jezika kojim laska žena tuða.
yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
25 Ne zaželi u srcu svom ljepote njezine, i nemoj da te uhvati vjeðama svojim.
Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
26 Jer sa žene kurve spada èovjek na komad hljeba, i žena pusta lovi dragocjenu dušu.
kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
27 Hoæe li ko uzeti ognja u njedra a haljine da mu se ne upale?
Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
28 Hoæe li ko hoditi po živom ugljevlju a nogu da ne ožeže?
Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
29 Tako biva onome koji ide k ženi bližnjega svojega; neæe biti bez krivice ko je se god dotakne.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
30 Ne sramote lupeža koji ukrade da nasiti dušu svoju, buduæi gladan;
Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
31 Nego kad ga uhvate plati samosedmo, da sve imanje doma svojega.
Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
32 Ali ko uèini preljubu sa ženom, bezuman je, dušu svoju gubi ko tako èini;
Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
33 Muke i ruga dopada, i sramota se njegova ne može izbrisati.
Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
34 Jer je ljubavna sumnja žestoka u muža i ne štedi na dan osvete;
kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
35 Ne mari ni za kakav otkup, i ne prima ako æeš i mnogo darova davati.
Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.

< Poslovice 6 >