< Poslovice 29 >
1 Èovjek koji po karanju ostaje tvrdoglav, ujedanput æe propasti, da neæe biti lijeka.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 Kad se umnožavaju pravednici, veseli se narod; a kad vlada bezbožnik, uzdiše narod.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 Ko ljubi mudrost, veseli oca svojega; a ko se druži s kurvama, rasipa svoje dobro.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 Car pravdom podiže zemlju; a ko uzima mito, satire je.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 Ko laska prijatelju svojemu, razapinje mrežu nogama njegovijem.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 U grijehu je zla èovjeka zamka, a pravednik pjeva i veseli se.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 Pravednik razumije parbu nevoljnijeh, a bezbožnik ne mari da zna.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Potsmjevaèi raspaljuju grad, a mudri utišavaju gnjev.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 Mudar èovjek kad se pre s ludijem, ili se srdio ili smijao, nema mira.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 Krvopije mrze na bezazlenoga, a pravi se brinu za dušu njegovu.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 Sav gnjev svoj izliva bezumnik, a mudri ustavlja ga natrag.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 Koji knez sluša lažne rijeèi, sve su mu sluge bezbožne.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 Siromah i koji daje na dobit sretaju se; obojici Gospod prosvjetljuje oèi.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 Koji car pravo sudi siromasima, njegov æe prijesto stajati dovijeka.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 Prut i kar daju mudrost, a dijete pusto sramoti mater svoju.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 Kad se umnožavaju bezbožnici, umnožavaju se grijesi, a pravednici æe vidjeti propast njihovu.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Karaj sina svojega, i smiriæe te, i uèiniæe milinu duši tvojoj.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 Kad nema utvare, rasipa se narod; a ko drži zakon, blago njemu!
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 Rijeèima se ne popravlja sluga, jer ako i razumije, opet ne sluša.
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 Jesi li vidio èovjeka nagla u besjedi svojoj? više ima nadanja od bezumna nego od njega.
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 Ako ko mazi slugu od malena, on æe najposlije biti sin.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 Gnjevljiv èovjek zameæe svaðu, i ko je naprasit, mnogo griješi.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 Oholost ponižuje èovjeka, a ko je smjeran duhom, dobija slavu.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 Ko dijeli s lupežem, mrzi na svoju dušu, èuje prokletstvo i ne prokazuje.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 Strašiv èovjek meæe sebi zamku; a ko se u Gospoda uzda, biæe u visokom zaklonu.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Mnogi traže lice vladaoèevo, ali je od Gospoda sud svakome.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 Pravednima je mrzak nepravednik, a bezbožniku je mrzak ko pravo hodi.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.