< Nehemija 9 >
1 Potom dvadeset èetvrtoga dana toga mjeseca skupiše se sinovi Izrailjevi posteæi i u kostrijeti i posuvši se zemljom.
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa nguo za gunia na kujitia mavumbi vichwani mwao.
2 I odvoji se sjeme Izrailjevo od svijeh tuðinaca, i stadoše te ispovijedahu grijehe svoje i bezakonja otaca svojih.
Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
3 I stajahu na svom mjestu, te im se èitaše zakon Gospoda Boga njihova èetvrt dana, a drugu èetvrt ispovijedahu se i poklanjahu se Gospodu Bogu svojemu.
Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Bwana Mungu wao kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Bwana Mungu wao.
4 A Isus i Vanije, Kadmilo, Sevanija, Vunije, Serevija, Vanije i Hananije popevši se na mjesto podignuto za Levite vapijahu glasom velikim ka Gospodu Bogu svojemu.
Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Bwana Mungu wao kwa sauti kubwa.
5 I rekoše Leviti Isus i Kadmilo, Vanije, Asavnija, Serevija, Odija, Sevanija i Petaja: ustanite, blagosiljajte Gospoda Boga svojega od vijeka do vijeka; i da se blagosilja ime tvoje slavno i uzvišeno svrh svakoga blagoslova i hvale.
Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Bwana Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele. “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
6 Ti si sam Gospod; ti si stvorio nebo, nebesa nad nebesima i svu vojsku njihovu, zemlju i sve što je na njoj, mora i sve što je u njima, i ti oživljavaš sve to, i vojska nebeska tebi se klanja.
Wewe peke yako ndiwe Bwana. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
7 Ti si Gospod Bog, koji si izabrao Avrama i izveo iz Ura Haldejskoga i nadio mu ime Avraam;
“Wewe ni Bwana Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Abrahamu.
8 I našao si srce njegovo vjerno pred sobom, i uèinio si s njim zavjet da æeš dati zemlju Hanansku, Hetejsku, Amorejsku, Ferezejsku i Jevusejsku i Gergesejsku, da æeš dati sjemenu njegovu, i ispunio si rijeèi svoje, jer si pravedan.
Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya Agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
9 Jer si pogledao na muku otaca naših u Misiru, i viku njihovu èuo si na Moru Crvenom;
“Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
10 I uèinio si znake i èudesa na Faraonu i na svijem slugama njegovijem i na svem narodu zemlje njegove, jer si znao da su obijesno postupali s njima; i stekao si sebi ime, kao što se vidi danas.
Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
11 I more si razdvojio pred njima, te prijeðoše posred mora suhim, i bacio si u dubine one koji ih gnahu kao kamen u vodu.
Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
12 I u stupu od oblaka vodio si ih danju a noæu u stupu ognjenom svijetleæi im putem kojim æe iæi.
Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
13 I sišao si na goru Sinajsku i govorio s njima s neba, i dao im sudove prave i zakone istinite, uredbe i zapovijesti dobre.
“Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti na sheria zile ambazo ni za kweli na haki, pia amri na maagizo mazuri.
14 I obznanio si im subotu svoju svetu, i dao im zapovijesti i uredbe i zakon preko Mojsija sluge svojega.
Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Mose.
15 I hljeb s neba dao si im u gladi njihovoj, i vodu iz kamena izveo si im u žeði njihovoj, i rekao si im da idu i naslijede zemlju za koju si podigao ruku svoju da æeš im je dati.
Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kutoka kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
16 Ali oni i oci naši uzobijestiše se i otvrdnuše vratom svojim i ne slušaše zapovijesti tvojih.
“Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
17 Ne htješe slušati, i ne opominjaše se èudesa tvojih koja si im èinio, nego otvrdnuše vratom svojim, i u odmetu svom postavljaše sebi voða da se vrate u ropstvo svoje. Ali ti, Bože, koji opraštaš, koji si žalostiv i milostiv, koji dugo trpiš i velike si milosti, nijesi ih ostavio.
Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
18 I onda kad naèiniše sebi tele liveno i rekoše: ovo je tvoj Bog koji te je izveo iz Misira, i huliše veoma,
hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipofanya makufuru makubwa.
19 Ni onda ih radi velike milosti svoje nijesi ostavio u pustinji; stup od oblaka nije otstupao od njih danju vodeæi ih putem, niti stup ognjeni noæu svijetleæi im putem kojim æe iæi.
“Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
20 I dao si im dobri svoj duh da ih urazumljuje, i mane svoje nijesi ustegao od usta njihovijeh, i vode si im dao u žeði njihovoj.
Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
21 I èetrdeset godina hranio si ih u pustinji, ništa im nije nedostajalo: odijelo im ne ovetša i noge im ne otekoše.
Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
22 I dao si im carstva i narode, i podijelio si ih po krajevima, jer naslijediše zemlju Sionovu, zemlju cara Esevonskoga, i zemlju cara Vasanskoga;
“Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
23 I umnožio si sinove njihove kao zvijezde nebeske, i uveo si ih u zemlju za koju si rekao ocima njihovijem da æe uæi u nju i naslijediti je.
Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
24 I uðoše sinovi njihovi i naslijediše zemlju, i pokorio si im Hananeje stanovnike zemaljske i predao ih u njihove ruke, i careve njihove i narode zemaljske, da èine od njih što im je volja.
Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
25 I tako uzeše tvrde gradove i zemlju rodnu, i naslijediše kuæe pune svakoga dobra, studence iskopane, vinograde, maslinike i voæke mnoge, i jedoše i nasitiše se i ugojiše se, i blagovahu po velikoj tvojoj dobroti.
Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
26 Ali te razgnjeviše i odmetnuše se tebe: baciše zakon tvoj za leða i proroke tvoje pobiše, koji im svjedoèahu da bi ih obratili k tebi, i huliše veoma.
“Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakafanya makufuru makubwa.
27 Zato si ih davao u ruke neprijateljima njihovijem koji ih muèiše. A kad u nevolji svojoj vikaše k tebi, ti si ih uslišio s neba i po velikoj milosti svojoj davao si im izbavitelje, koji ih izbavljaše iz ruku neprijatelja njihovijeh.
Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Kutoka mbinguni uliwasikia, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa waokozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
28 Ali èim otpoèinuše, opet èiniše zlo pred tobom, zato si ih ostavljao u ruku neprijatelja njihovijeh da vladaju njima; a kad se obraæaše i vikaše k tebi, ti si ih uslišio s neba i izbavljao ih po milosti svojoj mnogo puta.
“Lakini mara walipokuwa na raha, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia kutoka mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
29 I opominjao si ih da bi ih obratio k zakonu svojemu, ali oni bijahu obijesni i ne slušaše zapovijesti tvojih i griješiše o tvoje zakone, koje ko vrši živ æe biti kroz njih; i izmièuæi ramena svoja otvrdnuše vratom svojim i ne slušaše.
“Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
30 I trpio si ih mnogo godina opominjuæi ih duhom svojim preko proroka svojih; ali ne slušaše; tada si ih dao u ruke narodima zemaljskim.
Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao. Kwa njia ya Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
31 Ali radi milosti svoje velike nijesi dao da sasvijem propadnu niti si ih ostavio, jer si Bog milostiv i žalostiv.
Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
32 Sada dakle, Bože naš, Bože veliki, silni i strašni, koji èuvaš zavjet i milost, nemoj da je malo pred tobom što nas snaðe sva ova muka, careve naše, knezove i sveštenike naše i proroke naše i oce naše i sav narod tvoj od vremena careva Asirskih do danas.
“Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
33 Ti si pravedan u svemu što nas je snašlo, jer si ti pravo uèinio a mi smo bezbožno radili.
Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
34 I carevi naši, knezovi naši i oci naši ne izvršivaše zakona tvojega niti mariše za zapovijesti tvoje i svjedoèanstva tvoja, kojima si im svjedoèio.
Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
35 Jer u carstvu svom i u velikom dobru tvom koje si im èinio, i u zemlji prostranoj i rodnoj koju si im dao, ne služiše tebi niti se povratiše od zlijeh djela svojih.
Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
36 Evo, mi smo danas robovi; i još u zemlji, koju si dao ocima našim da jedu rod njezin i dobra njezina, evo mi smo robovi u njoj.
“Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
37 I ona rod svoj obilati raða carevima koje si postavio nad nama za grijehe naše, i koji gospodare nad našim tjelesima i nad stokom našom po svojoj volji, te smo u velikoj tjeskobi.
Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
38 A radi svega toga èinimo tvrd zavjet i pišemo, a knezovi naši, Leviti naši, sveštenici naši peèate.
“Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”