< Nehemija 2 >

1 A mjeseca Nisana godine dvadesete Artakserksa cara bijaše vino pred njim, i ja uzev vino dadoh ga caru. A preðe ne bijah neveseo pred njim.
Katika mwezi wa Nisani mwaka wa ishirini wa utawala wa Mfalme Artashasta, wakati divai ilipoletwa kwake, niliichukua na kumpa mfalme. Sikuwahi kuonekana mwenye huzuni mbele yake kabla ya hapo.
2 I reèe mi car: što si lica nevesela, kad nijesi bolestan? nije drugo nego tuga u srcu. A ja se uplaših vrlo.
Basi mfalme akaniuliza, “Kwa nini uso wako unaonekana una huzuni wakati wewe si mgonjwa? Jambo hili si kitu kingine bali ni huzuni ya moyo.” Niliogopa sana,
3 I rekoh caru: da je živ car dovijeka! kako ne bih bio lica nevesela, kad je grad gdje su grobovi mojih otaca opustio i vrata mu ognjem spaljena?
lakini nikamwambia mfalme, “Mfalme na aishi milele! Kwa nini uso wangu usiwe na huzuni wakati mji walipozikwa baba zangu umebaki magofu, na malango yake yameteketezwa kwa moto?”
4 A car mi reèe: šta hoæeš? Tada se pomolih Bogu nebeskomu,
Mfalme akaniambia, “Je, haja yako ni gani?” Ndipo nikaomba kwa Mungu wa mbinguni,
5 I rekoh caru: ako je ugodno caru i ako ti je mio sluga tvoj, pošlji me u Judeju u grad gdje su grobovi otaca mojih da ga sagradim.
na nikamjibu mfalme, “Kama ikimpendeza mfalme, na kama mtumishi wako amepata kibali machoni pake, anitume kule mji wa Yuda, mahali baba zangu walipozikwa, ili niweze kuujenga upya.”
6 A car mi reèe, a žena njegova sjeðaše do njega: koliko ti vremena treba na put, i kad æeš se vratiti? I bi ugodno caru, i pusti me kad mu kazah vrijeme.
Kisha mfalme, na malkia akiwa ameketi karibu naye, akaniuliza, “Safari yako itachukua muda gani, nawe utarudi lini?” Ilimpendeza mfalme kunituma, kwa hiyo nikapanga muda.
7 Potom rekoh caru: ako je ugodno caru, da mi se da knjiga na knezove preko rijeke da me prate dokle ne doðem u Judeju,
Pia nikamwambia, “Kama ikimpendeza mfalme, naomba nipewe barua kwa watawala wa Ngʼambo ya Frati, ili wanipe ulinzi mpaka nifike Yuda.
8 I knjiga na Asafa èuvara šume careve da mi da drva za brvna na vrata od dvora uz dom Božji i za zid gradski i za kuæu u koju æu uæi. I dade mi car, jer dobra ruka Boga mojega bješe nada mnom.
Naomba nipewe barua nipeleke kwa Asafu, mtunzaji wa msitu wa mfalme, ili anipe miti ya kutengeneza boriti kwa ajili ya malango ya ngome ya Hekalu, na ukuta wa mji, na makao yangu nitakapoishi.” Kwa kuwa mkono wenye neema wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu, mfalme akanijalia ombi langu.
9 I tako doðoh ka knezovima preko rijeke, i dadoh im knjige careve. A car posla sa mnom vojvode i konjike.
Basi nilienda kwa watawala wa Ngʼambo ya Frati na kuwapa barua za mfalme. Pia mfalme alikuwa ametuma maafisa wa jeshi na askari wapanda farasi pamoja nami.
10 A kad to èu Sanavalat Oronjanin i Tovija sluga Amonac, bi im vrlo mrsko što doðe èovjek da se postara za dobro sinovima Izrailjevijem.
Sanbalati Mhoroni na Tobia afisa Mwamoni waliposikia juu ya jambo hili, waliudhika sana kwamba amekuja mtu kuinua ustawi wa Waisraeli.
11 Potom doðoh u Jerusalim, i bih ondje tri dana.
Nilienda Yerusalemu, na baada ya kukaa huko siku tatu,
12 Pa ustah noæu s nekoliko ljudi, a nikomu ne kazah što mi je Bog moj dao u srce da uèinim u Jerusalimu; i ne imah kljuseta sa sobom osim onoga na kom jahah.
nikaondoka wakati wa usiku pamoja na watu wachache. Sikuwa nimemwambia mtu yeyote kile ambacho Mungu wangu alikuwa ameweka moyoni mwangu kufanya kwa ajili ya Yerusalemu. Hapakuwepo na mnyama yeyote pamoja nami isipokuwa yule niliyekuwa nimempanda.
13 I izidoh noæu na vrata od doline, na izvor zmajevski, i na vrata gnojna, i razgledah zidove Jerusalimske kako bjehu razvaljeni i kako mu vrata bjehu ognjem popaljena.
Nikatoka nje usiku kupitia Lango la Bondeni, kuelekea Kisima cha Joka na Lango la Samadi, nikikagua kuta za Yerusalemu zilizokuwa zimebomolewa, na malango yake yaliyokuwa yameteketezwa kwa moto.
14 Otuda proðoh na izvorska vrata i na carsko jezero, a ondje ne bješe mjesta da kljuse poda mnom prijeðe.
Kisha nikaelekea mpaka Lango la Chemchemi na Bwawa la Mfalme, lakini hapakuwepo nafasi ya kutosha kwa ajili ya mnyama wangu kupita,
15 Zato jahah uz potok po noæi i razgledah zid, pa se vratih na vrata od doline, i tako doðoh natrag.
kwa hiyo nikapandia bondeni usiku nikikagua ukuta. Mwishoni nikarudi na kuingia tena kupitia Lango la Bondeni.
16 Ali poglavari ne znadijahu kuda sam išao ni šta sam radio, jer do tada ne bijah ništa rekao ni Judejcima ni sveštenicima ni knezovima ni poglavarima ni drugima koji upravljahu poslom.
Maafisa hawakujua nilikokwenda wala nilichokuwa nikifanya, kwa sababu mpaka sasa nilikuwa bado sijasema lolote kwa Wayahudi, wala makuhani, wala wakuu, wala maafisa, wala mtu yeyote ambaye angefanya kazi.
17 Zato im rekoh: vidite u kakvom smo zlu, Jerusalim pust i vrata mu popaljena ognjem; dajte da zidamo zidove Jerusalimske, da više ne budemo rug.
Ndipo nilipowaambia, “Mnaona taabu tuliyo nayo: Yerusalemu imebaki magofu na malango yake yameteketezwa kwa moto. Njooni tujenge upya ukuta wa Yerusalemu, nasi hatutakuwa tena katika aibu hii.”
18 I kazah im kako je dobra ruka Boga mojega nada mnom i rijeèi careve koje mi je rekao. Tada rekoše: ustanimo i zidajmo. I ukrijepiše im se ruke na dobro.
Pia niliwaambia kuhusu mkono wenye neema wa Mungu wangu uliokuwa juu yangu, na kile mfalme alichokuwa ameniambia. Wakajibu, “Haya! Tuanze kujenga tena.” Kwa hiyo wakaanza kazi hii njema.
19 A kad to èu Sanavalat Oronjanin i Tovija sluga Amonac i Gisem Arapin, potsmijevaše nam se i rugaše nam se govoreæi: šta to radite? da se neæete odmetnuti caru?
Lakini Sanbalati Mhoroni, Tobia afisa Mwamoni, na Geshemu Mwarabu waliposikia kuhusu jambo hili, walitudhihaki na kutucheka. Wakauliza, “Ni nini hiki mnachokifanya? Je, mnaasi dhidi ya mfalme?”
20 A ja im odgovorih i rekoh: Bog nebeski daæe nam sreæu, a mi sluge njegove ustasmo i zidamo; ali vi nemate dijela ni prava ni spomena u Jerusalimu.
Nikawajibu kwa kusema, “Mungu wa mbinguni atatufanikisha. Sisi watumishi wake tutaanza kujenga upya, lakini kwenu ninyi, hamna sehemu wala dai lolote wala kumbukumbu la haki katika Yerusalemu.”

< Nehemija 2 >