< Levitski Zakonik 18 >
1 Još reèe Gospod Mojsiju govoreæi:
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
2 Kaži sinovima Izrailjevim, i reci im: ja sam Gospod Bog vaš.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
3 Nemojte èiniti što se èini u zemlji Misirskoj, u kojoj ste živjeli, niti èinite što se èini u zemlji Hananskoj, u koju vas vodim, i po uredbama njihovijem nemojte živjeti.
Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
4 Nego moje zakone vršite i moje uredbe držite živeæi po njima. Ja sam Gospod Bog vaš.
Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
5 Držite uredbe moje i zakone moje; ko ih vrši, živ æe biti kroz njih. Ja sam Gospod.
Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
6 Niko da ne pristupa k rodici svojoj po krvi, da otkrije golotinju njezinu. Ja sam Gospod.
Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
7 Golotinje oca svojega ni golotinje matere svoje ne otkrij; mati ti je; ne otkrij golotinje njezine.
Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
8 Golotinje žene oca svojega ne otkrij; golotinja je oca tvojega.
Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
9 Golotinje sestre svoje, kæeri oca svojega ili kæeri matere svoje, koja je roðena u kuæi ili izvan kuæe, ne otkrij golotinje njihove.
Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
10 Golotinje kæeri sina svojega, ili kæeri kæeri svoje ne otkrij; jer je tvoja golotinja.
Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
11 Golotinje kæeri žene oca svojega, koju je rodio otac tvoj, ne otkrij; sestra ti je.
Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12 Golotinje sestre oca svojega ne otkrij; jedna je krv s ocem tvojim.
Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13 Golotinje sestre matere svoje ne otkrij; jer je jedna krv s materom tvojom.
Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14 Golotinje brata oca svojega ne otkrij pristupajuæi k ženi njegovoj; strina ti je.
Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15 Golotinje žene sina svojega ne otkrij; snaha ti je, ne otkrij golotinje njezine.
Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
16 Golotinje žene brata svojega ne otkrij; golotinja je brata tvojega.
Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
17 Golotinje žene i kæeri njezine ne otkrij; kæeri sina njezina ni kæeri kæeri njezine nemoj uzeti da otkriješ golotinju njihovu; jedna su krv; zlo je.
Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
18 Nemoj uzeti žene preko jedne žene, da je ucvijeliš otkrivajuæi golotinju drugoj za života njezina.
Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
19 K ženi dokle se odvaja radi neèistote svoje ne idi da otkriješ golotinju njezinu.
Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
20 Sa ženom bližnjega svojega ne lezi skvrneæi se s njom.
Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
21 Od sjemena svojega ne daj da se odnese Molohu, da ne oskvrniš imena Boga svojega; ja sam Gospod.
Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
22 S muškarcem ne lezi kao sa ženom; gadno je.
Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
23 Živinèeta nikakoga nemoj obležati skvrneæi se s njim; i žena da ne legne pod živinèe; grdilo je.
Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
24 Nemojte se skvrniti nijednom ovom stvarju; jer su se svijem tijem stvarima oskvrnili narodi koje æu odagnati ispred vas.
Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
25 Jer se oskvrnila zemlja, i nevaljalstvo æu njezino pohoditi na njoj, i izmetnuæe zemlja stanovnike svoje.
Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
26 Nego vi držite zakone moje i uredbe moje, i ne èinite nijednoga ovoga gada, ni domorodac ni došljak koji se bavi meðu vama;
Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
27 Jer sve ove gadove èiniše ljudi u ovoj zemlji koji su bili prije vas, i zemlja je od toga oskvrnjena;
Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
28 Da ne izmetne zemlja vas, ako je oskvrnite, kao što je izmetnula narod koji je bio prije vas.
Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
29 Jer ko uèini štogod od ovijeh gadova, istrijebiæe se iz naroda svojega duše koje uèine.
Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
30 Zato držite što sam naredio da se drži, da ne èinite što od gadnijeh obièaja koji su bili prije vas, i da se ne skvrnite o njih. Ja sam Gospod Bog vaš.
Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.