< Levitski Zakonik 11 >

1 I reèe Gospod Mojsiju i Aronu govoreæi im:
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
2 Kažite sinovima Izrailjevim i recite: ovo su životinje koje æete jesti izmeðu svijeh životinja na zemlji:
“Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:
3 Što god ima papke i papci su mu razdvojeni i preživa izmeðu životinja, to jedite.
Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.
4 Ali onijeh što samo preživaju ili što samo imaju papke razdvojene, ne jedite, kao što je kamila, jer preživa ali nema papaka razdvojenih; da vam je neèista;
“‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
5 I pitomi zec, jer preživa ali nema papaka razdvojenih; neèist da vam je;
Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
6 I zec divlji, jer preživa ali nema papaka razdvojenih; neèist da vam je;
Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
7 I svinja, jer ima papke razdvojene ali ne preživa; neèista da vam je;
Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
8 Mesa od njih ne jedite niti se strva njihova dodijevajte; jer vam je neèisto.
Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.
9 A izmeðu svega što je u vodi ovo jedite: što god ima pera i ljusku u vodi, po moru i po rijekama, jedite.
“‘Kuhusu viumbe wote wanaoishi ndani ya maji ya bahari na vijito, mtakula wale wote wenye mapezi na magamba.
10 A što nema pera i ljuske u moru i u rijekama izmeðu svega što se mièe po vodi i živi u vodi, da vam je gadno.
Lakini viumbe wote ndani ya bahari au vijito wasio na mapezi na magamba, wakiwa miongoni mwa makundi au viumbe wote ndani ya maji, hao ni machukizo kwenu.
11 Gadno da vam je; mesa da im ne jedete, i na strv njihov da se gadite.
Nao watakuwa machukizo kwenu. Msile nyama yao, nayo mizoga yao itakuwa machukizo.
12 Što god nema pera i ljuske u vodi, to da vam je gadno.
Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba kitakuwa chukizo kwenu.
13 A izmeðu ptica ove da su vam gadne i da ih ne jedete: orao i jastrijeb i morski orao,
“‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,
14 Eja i kraguj po svojim vrstama,
mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
15 I svaki gavran po svojim vrstama,
aina zote za kunguru,
16 I sovuljaga i æuk i liska i kobac po svojim vrstama,
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
17 I buljina i gnjurac i ušara,
bundi, mnandi, bundi mkubwa,
18 I labud i gem i svraka,
mumbi, mwari, nderi,
19 I roda i èaplja po svojim vrstama, i pupavac i ljiljak.
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
20 Što god gamiže a ima krila i ide na èetiri noge, da vam je gadno.
“‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
21 Ali izmeðu svega što gamiže a ima krila i ide na èetiri noge jedite što ima stegna na nogama svojim, kojima skaèe po zemlji.
Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.
22 Izmeðu njih jedite ove: arba po vrstama njegovim, salema po vrstama njegovim, argola po vrstama njegovim i agava po vrstama njegovim.
Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.
23 A što još gamiže a ima krila i èetiri noge, da vam je gadno.
Lakini viumbe wengine wote wenye mabawa na wenye miguu minne ni machukizo kwenu.
24 I o njih æete se oskvrniti; ko se god dotakne mrtva tijela njihova, da je neèist do veèera.
“‘Mtajinajisi kwa wanyama hawa. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
25 I ko bi god nosio mrtva tijela njihova, neka opere haljine svoje, i da je neèist do veèera.
Yeyote atakayebeba mizoga ya viumbe hawa ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
26 Svaka životinja koja ima papke ali nerazdvojene i ne preživa, da vam je neèista; ko ih se god dotakne, da je neèist.
“‘Kila mnyama mwenye ukwato ulioachana lakini haukugawanyika kabisa, au yule asiyecheua, huyo ni najisi kwenu; yeyote agusaye mzoga wowote wa hao atakuwa najisi.
27 I što god ide na šapama izmeðu svijeh životinja èetvoronogih, da vam je neèisto; ko bi se dotakao strva njihova, da je neèist do veèera.
Miongoni mwa wanyama wote watembeao kwa miguu minne, wale watembeao kwa vitanga vyao ni najisi kwenu; yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
28 I ko bi nosio strv njihov, neka opere haljine svoje, i da je neèist do veèera; to da vam je neèisto.
Yeyote atakayebeba mizoga yao ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Wanyama hawa ni najisi kwenu.
29 I izmeðu životinja koje pužu po zemlji da su vam neèiste: lasica i miš i kornjaèa po svojim vrstama,
“‘Kuhusu wanyama watambaao juu ya ardhi, hawa ni najisi kwenu: kicheche, panya, aina yoyote ya mijusi mikubwa,
30 I jež i gušter i tvor i puž i krtica.
guruguru, kenge, mijusi ya ukutani, goromoe na kinyonga.
31 To vam je neèisto izmeðu životinja koje pužu; ko ih se dotakne mrtvijeh, da je neèist do veèera.
Hao wote watambaao juu ya ardhi ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
32 I svaka stvar na koju padne koje od njih mrtvo biæe neèista, bila sprava drvena ili haljina ili koža ili torba, i svaka stvar koja treba za kakav posao, neka se metne u vodu, i da je neèista do veèera, poslije da je èista.
Ikiwa mmoja wao atakufa na kuangukia juu ya kitu fulani, chombo hicho, hata kikiwa cha matumizi gani, kitakuwa najisi, kiwe kimetengenezwa kwa mti, nguo, ngozi au gunia. Kiweke ndani ya maji; kitakuwa najisi mpaka jioni, kisha kitakuwa safi tena.
33 A svaki sud zemljani, u koji padne što od toga, i što god u njemu bude, biæe neèist, i razbijte ga.
Ikiwa mmoja wa wanyama aliyekufa ataangukia ndani ya chungu, kila kilichomo katika chungu hicho kitakuwa najisi, nawe ni lazima uvunje chungu hicho.
34 I svako jelo što se jede, ako na njega doðe onaka voda, da je neèisto, i svako piæe što se pije u svakom takom sudu, da je neèisto.
Chakula chochote ambacho chaweza kuliwa lakini kikawa kimeingia maji kutoka kwenye chungu hicho ni najisi, na kitu chochote cha majimaji ambacho chaweza kunyweka kutoka kwenye chungu hicho ni najisi.
35 I na što bi palo što od tijela njihova mrtva sve da je neèisto, i peæ i ognjište neka se razvali, jer je neèisto i neka vam je neèisto.
Chochote ambacho mzoga wa mmojawapo utaangukia kitakuwa najisi. Jiko au chungu cha kupikia ni lazima kivunjwe. Ni najisi, nawe ni lazima uvihesabu kuwa najisi.
36 A studenac i ubao, gdje se voda skuplja, biæe èist; ali što se dotakne strva njihova, biæe neèisto.
Lakini chemchemi au kisima, mahali pa kuchota maji, patakuwa safi, lakini yeyote atakayegusa moja ya mizoga hii ni najisi.
37 Ako li što od strva njihova padne na sjeme, koje se sije, ono æe biti èisto.
Kama mzoga ukianguka juu ya mbegu zozote ambazo ni za kupanda, zinabaki safi.
38 Ali ako bude polito sjeme vodom, pa onda padne što od strva njihova na sjeme, da vam je neèisto.
Lakini kama mbegu imetiwa maji na mzoga ukaanguka juu yake, hiyo mbegu ni najisi kwenu.
39 I kad ugine životinja od onijeh koje jedete, ko se dotakne strva njezina, da je neèist do veèera.
“‘Kama mnyama ambaye mnaruhusiwa kumla akifa, yeyote atakayeugusa mzoga wake atakuwa najisi mpaka jioni.
40 A ko bi jeo od strva njezina, neka opere haljine svoje i da je neèist do veèera; i ko bi odnio strv njezin, neka opere haljine svoje, i da je neèist do veèera.
Yeyote atakayekula sehemu ya mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayebeba mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
41 I sve što puže po zemlji, da vam je gadno, da se ne jede.
“‘Kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi ni chukizo; kisiliwe.
42 Što god ide na trbuhu i što god ide na èetiri noge ili ima više noga izmeðu svega što puže po zemlji, to ne jedite, jer je gad.
Msile kiumbe chochote kitambaacho juu ya ardhi, kiwe kitambaacho kwa tumbo lake, au kitambaacho kwa miguu minne au kwa miguu mingi; ni chukizo.
43 Nemojte se poganiti nièim što gamiže i nemojte se skvrniti njima, da ne budete neèisti s njih.
Msijitie unajisi kwa chochote katika viumbe hivi. Msijitie unajisi kwa viumbe hivyo au kutiwa unajisi navyo.
44 Jer ja sam Gospod Bog vaš; zato se osveæujte i budite sveti, jer sam ja svet; i nemojte se skvrniti nièim što puže po zemlji.
Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; jitakaseni mwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu. Msijitie unajisi wenyewe kwa kiumbe chochote kile kiendacho juu ya ardhi.
45 Jer ja sam Gospod, koji sam vas izveo iz zemlje Misirske da vam budem Bog; budite dakle sveti, jer sam ja svet.
Mimi ndimi Bwana niliyewapandisha mtoke Misri ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo kuweni watakatifu kwa sababu Mimi ni mtakatifu.
46 Ovo je zakon za zvijeri i za ptice, i za sve životinje što se mièu po vodi, i za svaku dušu živu koja puže po zemlji,
“‘Haya ndiyo masharti kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho ndani ya maji, na kila kiumbe kiendacho juu ya ardhi.
47 Da se raspoznaje neèisto od èistoga i životinja koja se jede od životinje koja se ne jede.
Ni lazima mpambanue kati ya kilicho najisi na kilicho safi, kati ya viumbe hai vinavyoweza kuliwa na vile visivyoweza kuliwa.’”

< Levitski Zakonik 11 >