< Isus Navin 22 >
1 Tada sazva Isus sinove Ruvimove i sinove Gadove i polovinu plemena Manasijina,
Kwa wakati huo, Yoshua aliwaita Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase.
2 I reèe im: vi držaste sve što vam je zapovjedio Mojsije sluga Gospodnji, i slušaste glas moj u svemu što sam vam zapovijedao.
Aliwaambia, “Mmefanya kila kitu ambacho Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi. Mmeitii sauti yangu katika yote niliyowaagiza.
3 Ne ostaviste braæe svoje dugo vremena, do ovoga dana, i dobro èuvaste zapovijest Gospoda Boga svojega.
Bado hamjawaacha ndugu zenu hawa kwa siku zote hizi, mpaka siku hii ya leo. Na mmetimiza wajibu unaotakiwa na amri za Yahweh Mungu wenu.
4 A sada Gospod je Bog vaš smirio braæu vašu, kako im je rekao; sada dakle vratite se i idite u šatore svoje u zemlju našljedstva svojega, koju vam je dao Mojsije sluga Gospodnji s onu stranu Jordana.
Sasa Yahweh Mungu wenu amewapa pumziko ndugu zenu, kama alivyowaahidi. Hivyo basi, rudini na mwende katika hema zenu katika nchi mnayoimiliki, ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapeni katika upande mwingine wa Yordani.
5 Samo pazite dobro da vršite zapovijest i zakon, što vam je zapovjedio Mojsije sluga Gospodnji, da ljubite Gospoda Boga svojega i da hodite svijem putovima njegovijem, i èuvate zapovijesti njegove i držite ih se, i da mu služite svijem srcem svojim i svom dušom svojom.
Lakini zingatieni kuzishika amri na sheria ambazo Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi, kumpenda Yahweh Mungu wenu, kutembea katika njia zake, kuzitunza amri zake, na kuambatana naye na kumwabudu yeye kwa moyo wenu wote na kwa roho zenu zote.
6 I blagoslovi ih Isus, i otpusti ih da idu u svoje šatore.
Basi Yoshua akawabariki na kisha akawaacha waende zao, nao wakarudi katika hema zao.
7 A polovini plemena Manasijina bješe dao Mojsije našljedstvo u Vasanu, a drugoj polovini dade Isus s braæom njihovom s ovu stranu Jordana k zapadu. I otpuštajuæi ih Isus u šatore njihove blagoslovi ih,
Na kwa nusu ya kabila la Manase, Musa alikuwa amewapa urithi katika Bashani, lakini kwa nusu ya kabila hilo, Yoshua aliwapa urithi karibu na ndugu zao katika nchi magharibi mwa Yordani. Yoshua aliwaaga waende katika hema zao; aliwabarikia,
8 I reèe im govoreæi: s velikim blagom vraæate se u šatore svoje, sa stokom vrlo mnogom; sa srebrom i zlatom i mjeðu i gvožðem i odijelom vrlo mnogim; podijelite plijen od neprijatelja svojih s braæom svojom.
na kisha akawaambia, “Rudini katika hema zenu mkiwa na pesa nyingi, na mkiwa na mifugo mingi, pamoja na na fedha, na dhahabu, na shaba na chuma, na nguo nyingi. Gawaneni na ndugu zenu nyara mlizochukua kutoka kwa maadui zenu.
9 I vrativši se sinovi Ruvimovi i sinovi Gadovi i polovina plemena Manasijina otidoše od sinova Izrailjevijeh iz Siloma, koji je u zemlji Hananskoj, iduæi u zemlju Galadsku, u zemlju našljedstva svojega, koju naslijediše, kako bješe Gospod zapovjedio preko Mojsija.
Hivyo, wazawa wa Rubeni, wazawa wa Gadi na nusu ya kabila la Manase walirudi nyumbani, waliwaacha watu wa Isaeli hapo Shilo, ambayo imo ndani ya nchi ya Kanaani. Waliondoka wakaenda katika mkoa wa Gileadi, katika nchi yao, ambayo wao wenyewe waliimiliki, katika utiifu wa amri za Yahweh, kwa mkono wa Musa.
10 A kad doðoše na meðu Jordansku u zemlji Hananskoj, naèiniše sinovi Ruvimovi i sinovi Gadovi i polovina plemena Manasijina oltar ondje na Jordanu, oltar velik i naoèit.
Nao walipofika hapo Yordani iliyo katika nchi ya Kanaani, Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase walijenga madhabahu karibu na Yordani, madhabahu kubwa na iliyotokeza na mashuhuri.
11 I èuše sinovi Izrailjevi gdje se govori: gle, sinovi Ruvimovi i sinovi Gadovi i polovina plemena Manasijina naèiniše oltar prema zemlji Hananskoj na meði Jordanskoj, pokraj sinova Izrailjevijeh.
Watu wa Israeli walisikia habari hizo na wakaseam, “Tazama! Watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wamejenga madhabahu mbele ya nchi ya Kanaani, huko Gelilothi, katika mkoa karibu na Yordani, katika upande ambao ni miliki ya watu wa Israeli.”
12 A kad èuše sinovi Izrailjevi, skupi se sav zbor sinova Izrailjevijeh u Silom da idu da se biju s njima.
Wakati watu wa Israeli waliposikia hivyo, kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika kwa pamoja huko Shilo ili wapande kupigana vita nao.
13 I poslaše sinovi Izrailjevi k sinovima Ruvimovijem i sinovima Gadovijem i polovini plemena Manasijina u zemlju Galadsku Finesa sina Eleazara sveštenika,
Kisha watu wa Israeli walituma wajumbe kwa Warubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi. Walimtuma pia Finehasi mwana wa Eliezari, kuhani,
14 I s njim deset knezova, po jednoga kneza od doma otaèkoga od svijeh plemena Izrailjevijeh, a svaki ih bješe poglavar u domu otaca svojih u tisuæama Izrailjevijem.
na viongozi kumi pamoja naye, mmoja kutoka katika familia za mababa wa Israeli, na kila mmoja wao alikuwa ni kiongozi wa ukoo miongoni mwa watu wa Israeli.
15 A oni doðoše k sinovima Ruvimovijem i sinovima Gadovijem i polovini plemena Manasijina u zemlju Galadsku, i rekoše im govoreæi:
Walienda kwa watu wa Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi, na wakawaambia:
16 Ovako veli sav zbor Gospodnji: kakav je to grijeh kojim se ogriješiste Bogu Izrailjevu odvrativši se danas od Gospoda naèinivši oltar da se odmetnete danas od Gospoda?
“Kusanyiko lote la Yahweh linasema kuwa, ' Ni jambo gani hili lisilo la uaminifu ambalo mmelitenda kinyume na Mungu wa Israeli, kwa kugeuka badala ya kumfuata Yahweh siku hii na kujijengea wenyewe madhabahu katika uasi kinyume na Yahweh katika siku hii?
17 Malo li nam je grijeha Fegorova, od kojega se još nijesmo oèistili do danas i s kojega doðe pogibao na zbor Gospodnji,
Je dhambi zetu huko Peori hazikututosha? Bado hata sasa hatujajitakasa wenyewe kwa dhambi hiyo. Kwa ajili ya dhambi ile lilikuja pigo kwa kusanyiko lote la Yahweh.
18 Te se danas odvraæate od Gospoda, i odmeæete se danas od Gospoda, da se sjutra razgnjevi na sav zbor Izrailjev?
Je, nanyi leo pia mwageuka na kuacha kumfuata Yahweh? Kama mtaasi kinyume na Yahweh leo, kesho atakuwa na hasira na kusanyiko lote la Israeli.
19 Ako je zemlja našljedstva vašega neèista, prijeðite u zemlju našljedstva Gospodnjega, u kojoj stoji šator Gospodnji, i uzmite našljedstvo meðu nama; samo se ne odmeæite od Gospoda i ne odmeæite se od nas gradeæi sebi oltar mimo oltar Gospoda Boga našega.
Na kama nchi ambayo mnaimiliki imetiwa unajisi, basi mwaweza kuvuka katika nchi ambayo Sanduku la Yahweh lasimama na mjichukulie kwa ajili yenu umiliki miongoni mwetu. Hamtakiwi kuasi kinyume na Yahweh tu, wala kuasi kinyume chetu kwa kujenga madhabahu kwa ajili yenu wenyewe badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wa wetu.
20 Nije li se Ahan sin Zarin ogriješio o stvari proklete, te doðe gnjev na sav zbor Izrailjev? i on ne pogibe sam za grijeh svoj.
Je hakuwa Akani mwana wa Zera aliyeivunja imani kwa vitu vile ambavyo vilikuwa vimetunzwa kwa ajili ya Mungu? Na je ghadhabu ya Mungu haikushuka kwa watu wote wa Israeli? Mtu yule hakuangamia peke yake kwa uovu wake.
21 A sinovi Ruvimovi i sinovi Gadovi i polovina plemena Manasijina odgovoriše i rekoše poglavarima tisuæa Izrailjevih:
Kisha makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakawajibu wazee wa koo za Israeli:
22 Gospod Bog nad bogovima, Gospod Bog nad bogovima, on zna, i Izrailj neka zna. Ako smo radi odmetati se i griješiti Gospodu, neka nas ne saèuva danas.
“Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yeye anajua, na Israeli naijue yenyewe! Kama ilikuwa ni katika uasi au katika kuvunja imani kinyume na Yahweh, msituache hai katika siku hii ya leo
23 Ako smo naèinili oltar da se odvratimo od Gospoda ili da prinosimo na njemu žrtve paljenice ili dare ili da prinosimo na njemu žrtve zahvalne, Gospod neka traži.
kwa ajili ya kujenga madhabahu ili tugeuka na kuacha kumfuata Yahweh. Kama tumejenga madhabahu hii ili kutoa juu yake sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, au sadaka ya amani, basi Yahweh na atuadhibu.
24 Nego to uèinismo bojeæi se ovoga: rekosmo: sjutra æe reæi sinovi vaši sinovima našim govoreæi: šta vi imate s Gospodom Bogom Izrailjevim?
La hasha, tulifanya hivyo kwa sababu ya hofu kwamba katika siku zijazo watoto wenu wanaweza kuwaambia watoto wetu, ' Mna nini ninyi na Yahweh, Mungu wa Israeli?
25 Meðu je postavio Gospod izmeðu nas i vas, sinovi Ruvimovi i Gadovi, Jordan; vi nemate dijela u Gospoda. Te æe sinovi vaši odbiti sinove naše da se ne boje Gospoda.
Kwa kuwa Yahweh ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi. Ninyi watu wa Rubeni na watu wa Gadi, hamna kitu chochote naYahweh.' Na kwa hali hiyo, watoto wenu wanaweza kuwafanya watoto wetu waacha kumwabudu Yahweh.
26 Zato rekosmo: uèinimo tako, i naèinimo oltar, ne za žrtvu paljenicu ni za drugu žrtvu,
Basi tukasema, 'Hebu na tujenge sasa madhabahu, si kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa wala si kwa sadaka yoyote ile,
27 Nego da bude svjedok meðu nama i vama, i meðu natražjem našim nakon nas, da bismo služili Gospodu pred njim žrtvama svojim paljenicama i prinosima svojim, i žrtvama svojim zahvalnim, i da ne bi rekli kadgod sinovi vaši sinovima našim: vi nemate dijela u Gospoda.
ila iwe ni ushahidi kati yetu na ninyi, na kati ya kizazi chetu baada yetu, kwamba tutafanya ibada ya Yahweh mbele yake, pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa na dhabihu zetu na sadaka zetu za amani, ili kwamba watoto wenu wasiweze kuwaambia watoto wetu katika siku zijazo kuwa, “Hamna sehemu katika Yahweh.”'
28 Jer rekosmo: ako kad reku tako nama ili natražju našemu, tada æemo im kazati: vidite sliku od oltara Gospodnjega koju naèiniše oci naši ne za žrtvu paljenicu ni za drugu žrtvu, nego da je svjedoèanstvo meðu nama i vama.
Hivyo tukasema, 'kama hili litasemwa kwa kwetu au kwa watoto wetu katika siku zijazo, tutasema, “Tazama! Huu ni mfano wa madhabahu ya Yahweh, ambayo mababu zetu waliifanya, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala si kwa dhabihu, bali kwa ajili ya ushahidi kati yetu ninyi.”
29 Ne daj Bože da se odmeæemo Gospodu i da se danas odvraæamo od Gospoda naèinivši oltar za žrtvu paljenicu, za dar ili za prinos, mimo oltar Gospoda Boga našega, koji je pred šatorom njegovijem.
Na iwe mbali nasi kwamba tunataka kugeuka kinyume na Yahweh, na kuacha kumfuata yeye kwa kujenga madhabahu kwa ajili sadaka ya kuteketezwa, na kwa sadaka ya nafaka, au kwa dhabihu, badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wetu ambayo iko mbele ya hema la kukutania.'”
30 A kad èu Fines sveštenik i knezovi od zbora, poglavari od tisuæa Izrailjevih koji bijahu s njim, rijeèi koje im rekoše sinovi Ruvimovi i sinovi Gadovi i sinovi Manasijini, bi im po volji.
Finehasi kuhani na viongozi wa watu, ambao ni wakuu wa koo za Waisraeli ambao walikuwa pamoja naye, waliposikia maneno amabayo watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, kwamba yalikuwa ni mazuri machoni pao.
31 I reèe Fines sin Eleazara sveštenika sinovima Ruvimovijem i sinovima Gadovijem i sinovima Manasijinim: danas poznasmo da je meðu nama Gospod kad se ne ogriješiste Gospodu tijem grijehom, i saèuvaste sinove Izrailjeve od ruku Gospodnjih.
Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani aliwaambia watu wa Rubeni, Gadi na Manase, “Leo tumejua kwambaYahweh yuko miongoni mwetu, kwa kuwa hamjatenda uvunjaji wa imani kinyume naye. Sasa, mmewaokoa watu wa Israeli kutoka katika mkono wa Yahweh.”
32 I Fines sin Eleazara sveštenika i oni knezovi vratiše se od sinova Ruvimovijeh i od sinova Gadovijeh iz zemlje Galadske u zemlju Hanansku k sinovima Izrailjevijem, i javiše im stvar.
Kisha Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani, na viongozi walirudi kutoka kwa Warubeni na Wagadi, kutoka katika nchi ya Gileadi, na kurudi katika nchi ya Kanaani, kwa watu wa Israeli, na waliwaletea taarifa.
33 I bi po volji sinovima Izrailjevijem; i hvališe Boga sinovi Izrailjevi, i ne govoriše više da idu da se biju s njima da potru zemlju, u kojoj žive sinovi Ruvimovi i sinovi Gadovi.
Taarifa yao ilikuwa nzuri katika macho ya watu wa Israeli. Watu wa Israeli walimbarikia Mungu na hawakuendelea kusema tena juu ya kuinua vita dhidi ya Warubeni na Wagadi, ili kuiharibu nchi ambayo walikuwa wanaishi.
34 I prozvaše sinovi Ruvimovi i sinovi Gadovi onaj oltar Ed govoreæi: svjedok je meðu nama da je Gospod Bog.
Warubeni na Wagadi waliita ile madhabahu “Ushahidi,” kwa kuwa walisema, “Ni ushahidi miongoni mwetu kuwa Yahweh ni Mungu.”