< Jov 28 >

1 Da, srebro ima žice, i zlato ima mjesto gdje se topi.
“Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
2 Gvožðe se vadi iz praha, i iz kamena se topi mjed.
Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
3 Mraku postavlja meðu, i sve istražuje èovjek do kraja, i kamenje u tami i u sjenu smrtnom.
Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
4 Rijeka navre s mjesta svojega da joj niko ne može pristupiti; ali se odbije i odlazi trudom èovjeèjim.
Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
5 Iz zemlje izlazi hljeb, i pod njom je drugo, kao oganj.
Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
6 U kamenju je njezinu mjesto safiru, a ondje je prah zlatni.
yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
7 Te staze ne zna ptica, niti je vidje oko kragujevo;
Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
8 Ne ugazi je mlado zvijerje, niti njom proðe lav.
Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
9 Na kremen diže ruku svoju; prevraæa gore iz dna.
Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
10 Iz stijene izvodi potoke, i svašta dragocjeno vidi mu oko.
Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
11 Ustavlja rijeke da ne teku, i što je sakriveno iznosi na vidjelo.
Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
12 Ali mudrost gdje se nalazi? i gdje je mjesto razumu?
“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
13 Ne zna joj èovjek cijene, niti se nahodi u zemlji živijeh.
Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
14 Bezdana veli: nije u meni; i more veli: nije kod mene.
Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
15 Ne može se dati èisto zlato za nju, niti se srebro izmjeriti u promjenu za nju.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
16 Ne može se cijeniti zlatom Ofirskim, ni dragim onihom ni safirom.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
17 Ne može se izjednaèiti s njom ni zlato ni kristal, niti se može promijeniti za zaklade zlatne.
Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
18 Od korala i bisera nema spomena, jer je vrijednost mudrosti veæa nego dragom kamenju.
Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
19 Ne može se s njom izjednaèiti topaz Etiopski, niti se može cijeniti èistijem zlatom.
Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
20 Otkuda dakle dolazi mudrost? i gdje je mjesto razumu?
“Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
21 Sakrivena je od oèiju svakoga živoga, i od ptica nebeskih zaklonjena.
Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
22 Pogibao i smrt govore: ušima svojima èusmo slavu njezinu.
Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
23 Bog zna put njezin, i poznaje mjesto njezino.
Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
24 Jer gleda do krajeva zemaljskih i vidi sve što je pod svijem nebom.
kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
25 Kad davaše vjetru težinu, i mjeraše vodu mjerom,
Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
26 Kad postavljaše zakon daždu i put munji gromovnoj.
alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
27 Još je onda vidje i oglasi je, uredi je i pretraži je.
ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
28 A èovjeku reèe: gle, strah je Božji mudrost, i uklanjati se oda zla jest razum.
Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”

< Jov 28 >