< Isaija 66 >
1 Ovako veli Gospod: nebo je prijesto moj i zemlja podnožje nogama mojim: gdje je dom koji biste mi sazidali, i gdje je mjesto za moje poèivanje?
Hili ndilo asemalo Bwana, “Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Iko wapi nyumba mtakayoijenga kwa ajili yangu? Mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
2 Jer je sve to ruka moja stvorila, to je postalo sve, veli Gospod; ali na koga æu pogledati? na nevoljnoga i na onoga ko je skrušena duha i ko drkæe od moje rijeèi.
Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote, hivyo vikapata kuwepo?” asema Bwana. “Mtu huyu ndiye ninayemthamini: yeye ambaye ni mnyenyekevu na mwenye roho yenye toba, atetemekaye asikiapo neno langu.
3 Ko kolje vola, to je kao da ubije èovjeka; ko kolje ovcu, to je kao da zakolje psa; ko prinosi dar, to je kao da prinese krv svinjeæu; ko kadi kadom, to je kao da blagoslovi idola. To oni izabraše na putovima svojim, i duši se njihovoj mile gadovi njihovi.
Lakini yeyote atoaye dhabihu ya fahali ni kama yeye auaye mtu, na yeyote atoaye sadaka ya mwana-kondoo, ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa. Yeyote atoaye sadaka ya nafaka, ni kama yule aletaye damu ya nguruwe, na yeyote afukizaye uvumba wa kumbukumbu, ni kama yule aabuduye sanamu. Wamejichagulia njia zao wenyewe, nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao.
4 Izabraæu i ja prema nevaljalstvu njihovu, i pustiæu na njih èega se boje; jer zvah a niko se ne odazva, govorih a oni ne slušaše, nego èiniše što je zlo preda mnom i izabraše što meni nije po volji.
Hivyo, mimi pia nitawachagulia mapigo makali, nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa. Kwa maana nilipoita, hakuna yeyote aliyejibu, niliposema, hakuna yeyote aliyesikiliza. Walifanya maovu machoni pangu na kuchagua lile linalonichukiza.”
5 Slušajte rijeè Gospodnju, koji drkæete od njegove rijeèi: braæa vaša, koja mrze na vas i izgone vas imena mojega radi, govore: neka se pokaže slava Gospodnja. I pokazaæe se na vašu radost, a oni æe se posramiti.
Sikieni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia ninyi na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema, ‘Bwana na atukuzwe, ili tupate kuona furaha yenu!’ Hata sasa wataaibika.
6 Vika ide iz grada, glas iz crkve, glas Gospodnji koji plaæa neprijateljima svojim.
Sikieni hizo ghasia kutoka mjini, sikieni hizo kelele kutoka hekaluni! Ni sauti ya Bwana ikiwalipa adui zake yote wanayostahili.
7 Ona se porodi prije nego osjeti bolove, prije nego joj doðoše muke, rodi djetiæa.
“Kabla hajasikia utungu, alizaa; kabla hajapata maumivu, alizaa mtoto mwanaume.
8 Ko je igda èuo to? ko je vidio tako što? Može li zemlja roditi u jedan dan? može li se narod roditi ujedanput? a Sion rodi sinove svoje èim osjeti bolove.
Ni nani amepata kusikia jambo kama hili? Ni nani amepata kuona mambo kama haya? Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja, au taifa laweza kutokea mara? Mara Sayuni alipoona utungu, alizaa watoto wake.
9 Eda li ja, koji otvoram matericu, ne mogu roditi? veli Gospod; eda li æu ja, koji dajem da se raða, biti bez poroda? veli Bog tvoj.
Je, nilete mwana hadi wakati wa kuzaliwa na nisizalishe?” asema Bwana. “Je, nifunge tumbo la uzazi wakati mimi ndiye nizalishaye?” asema Mungu wako.
10 Radujte se s Jerusalimom i veselite se u njemu svi koji ga ljubite; radujte se s njim svi koji ga žaliste.
“Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi kwa ajili yake, ninyi nyote mnaompenda, shangilieni kwa nguvu pamoja naye, ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.
11 Jer æete sati sise od utjehe njegove, i nasitiæete se, saæete i naslaðivaæete se u svjetlosti slave njegove.
Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka katika faraja ya matiti yake; mtakunywa sana, na kuufurahia wingi wa mafuriko ya ustawi wake.”
12 Jer ovako veli Gospod: gle, ja æu kao rijeku dovesti k njemu mir i slavu naroda kao potok bujan, pa æete sati; biæete nošeni na rukama i milovani na koljenima.
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho; utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kubembelezwa magotini pake.
13 Kao kad koga mati njegova tješi tako æu ja vas tješiti, i utješiæete se u Jerusalimu.
Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”
14 Vidjeæete i obradovaæe se srce vaše i kosti æe se vaše pomladiti kao trava, i znaæe se ruka Gospodnja na slugama njegovijem i gnjev na neprijateljima njegovijem.
Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia, nanyi mtastawi kama majani; mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake, bali ghadhabu yake kali itaonyeshwa kwa adui zake.
15 Jer, gle, Gospod æe doæi s ognjem, i kola æe mu biti kao vihor, da izlije gnjev svoj u jarosti i prijetnju u plamenu ognjenom.
Tazama, Bwana anakuja na moto, magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli, atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali, na karipio lake pamoja na miali ya moto.
16 Jer æe Gospod suditi ognjem i maèem svojim svakom tijelu, i mnogo æe biti pobijenijeh od Gospoda.
Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake Bwana atatekeleza hukumu juu ya watu wote, nao wengi watakuwa ni wale waliouawa na Bwana.
17 Koji se osveštavaju i koji se oèišæaju u vrtovima jedan za drugim javno, koji jedu meso svinjeæe i stvari gadne i miše, svi æe izginuti, veli Gospod.
“Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asema Bwana.
18 A ja znam djela njihova i misli njihove, i doæi æe vrijeme, te æu sabrati sve narode i jezike, i doæi æe i vidjeæe slavu moju.
“Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.
19 I postaviæu znak na njih, i poslaæu izmeðu njih koji se spasu k narodima u Tarsis, u Ful i u Lud, koji natežu luk, u Tuval i u Javan i na daljna ostrva, koja ne èuše glasa o meni niti vidješe slave moje, i javljaæe slavu moju po narodima.
“Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Puli na Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.
20 I svu æe braæu vašu iz svijeh naroda dovesti Gospodu na dar na konjima i na kolima i na nosilima i na mazgama i na kamilama ka svetoj gori mojoj u Jerusalim, veli Gospod, kao što prinose sinovi Izrailjevi dar u èistu sudu u dom Gospodnji.
Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asema Bwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu la Bwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.
21 I izmeðu njih æu uzeti sveštenike i Levite, veli Gospod.
Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asema Bwana.
22 Jer kao što æe nova nebesa i nova zemlja, što æu ja naèiniti, stajati preda mnom, veli Gospod, tako æe stajati sjeme vaše i ime vaše.
“Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asema Bwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.
23 I od mladine do mladine, i od subote do subote dolaziæe svako tijelo da se pokloni preda mnom, veli Gospod.
Kutoka Mwezi Mpya hata mwingine, na kutoka Sabato hadi nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asema Bwana.
24 I izlaziæe i gledaæe mrtva tjelesa onijeh ljudi koji se odmetnuše od mene; jer crv njihov neæe umrijeti i oganj njihov neæe se ugasiti, i biæe gad svakom tijelu.
“Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi. Funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”