< Isaija 30 >

1 Teško sinovima odmetnicima, govori Gospod, koji sastavljaju namjere koje nijesu od mene, zaklanjaju se za zaklon koji nije od moga duha, da domeæu grijeh na grijeh;
Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
2 Koji slaze u Misir ne pitajuæi šta æu ja reæi, da se ukrijepe silom Faraonovom i da se zaklone pod sjenom Misirskim.
wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
3 Jer æe vam sila Faraonova biti na sramotu, i zaklon pod sjenom Misirskim na porugu.
Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
4 Jer knezovi njegovi biše u Soanu, i poslanici njegovi doðoše u Hanes.
Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
5 Ali æe se svi posramiti s naroda, koji im neæe pomoæi, niti æe im biti na korist ni na dobit, nego na sramotu i na porugu.
kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
6 Tovar æe biti na stoci južnoj: u zemlju gdje je nevolja i muka, gdje su lavovi i laviæi, guje i zmajevi ognjeni krilati, odnijeæe blago svoje magarcima na ramenima i bogatstvo svoje kamilama na grbama, k narodu koji neæe pomoæi.
Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
7 Jer æe Misirci uzalud i naprazno pomagati; zato vièem o tom: jaèina im je da sjede s mirom.
kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
8 Sada idi, napiši ovo pred njima na dašèicu, napiši u knjigu, da ostane za vremena koja æe doæi, dovijeka;
Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
9 Jer su narod nepokoran, sinovi lažljivi, sinovi koji neæe da slušaju zakona Gospodnjega;
Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
10 Koji govore vidiocima: nemojte viðati, i prorocima: nemojte nam prorokovati što je pravo, govorite nam mile stvari, prorokujte prijevaru;
Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
11 Svrnite s puta, otstupite od staze, neka nestane ispred nas sveca Izrailjeva.
Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
12 Zato ovako veli svetac Izrailjev: kad odbacujete ovu rijeè, i uzdate se u prijevaru i opaèinu i na nju se oslanjate,
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
13 Zato æe vam to bezakonje biti kao pukotina u zidu koji hoæe da padne, koja izdigne zid visoko, te se naglo ujedanput obori.
dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
14 I razbiæe ga kao što se razbija razbijen sud lonèarski, ne žali se, te se ne naðe ni crijepa kad se razbije da uzmeš oganj s ognjišta ili da zahvatiš vode iz jame.
Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
15 Jer ovako govori Gospod Gospod, svetac Izrailjev: ako se povratite i budete mirni, izbaviæete se, u miru i uzdanju biæe sila vaša; ali vi neæete.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
16 Nego govorite: ne; nego æemo na konjma pobjeæi. Zato æete bježati. Pojahaæemo brze konje. Zato æe biti brži koji æe vas tjerati.
Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
17 Bježaæe vas tisuæa kad jedan povièe; kad povièu petorica, bježaæete svi, dokle ne ostanete kao okresano drvo navrh gore i kao zastava na humu.
Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
18 A zato èeka Gospod da se smiluje na vas, i zato æe se uzvisiti da vas pomiluje; jer je Gospod pravedan Bog; blago svjema koji ga èekaju.
Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
19 Jer æe narod nastavati u Sionu, u Jerusalimu; neæeš više plakati, doista æe te pomilovati kad povièeš; èim te èuje, odazvaæe ti se.
Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
20 Premda æe vam Gospod dati hljeba tužnoga i vode nevoljnièke; ali ti se više neæe uzimati uèitelji tvoji, nego æe oèi tvoje gledati uèitelje tvoje,
Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
21 I uši æe tvoje slušati rijeè iza tebe gdje govori: to je put, idite njim, ako biste svrnuli nadesno ili nalijevo.
Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
22 I oprzniæete posrebrene likove svoje rezane i zlatno odijelo likova livenijeh, i baciæete ih kao neèistotu, i reæi æeš im: odlazite.
Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
23 I daæe dažd sjemenu tvojemu koje posiješ na njivi, i hljeb od roda zemaljskoga biæe obilat i sit; tada æe stoka tvoja pasti na paši prostranoj.
Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
24 Volovi i magarci, što rade zemlju, ješæe èistu zob ovijanu lopatom i rešetom.
Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
25 I na svakoj gori visokoj i na svakom humu visokom biæe izvori i potoci, kad bude pokolj veliki, kad popadaju kule.
Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
26 I svjetlost æe mjeseèna biti kao svjetlost sunèana, a svjetlost æe sunèana biti sedam puta veæa, kao svjetlost od sedam dana, kad Gospod zavije ulom narodu svojemu i iscijeli rane koje mu je zadao.
Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
27 Gle, ime Gospodnje ide izdaleka, gnjev njegov gori i vrlo je težak; usne su mu pune ljutine i jezik mu je kao oganj koji sažiže.
Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
28 A duh mu je kao potok koji plavi i dopire do grla, da rasije narode da otidu u ništa, i biæe u èeljustima narodima uzda koja æe ih goniti da lutaju.
Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
29 Pjevaæete kao noæu uoèi praznika, i veseliæete se od srca kao onaj koji ide sa sviralom na goru Gospodnju, k stijeni Izrailjevoj,
Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
30 I Gospod æe pustiti da se èuje slava glasa njegova, i pokazaæe kako maše rukom svojom s ljutijem gnjevom i plamenom ognjenijem koji proždire, s raspom i sa silnijem daždem i s gradom.
Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
31 Jer æe se od glasa Gospodnjega prepasti Asirac, koji je bio palicom.
Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
32 I kuda god proðe palica pouzdana, kojom æe Gospod navaliti na nj, biæe bubnji i gusle, i ratovima žestokim ratovaæe na njih.
Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
33 Jer je veæ pripravljen Tofet, i samom caru pripravljen je, naèinio je dubok i širok; mjesta, ognja i drva ima mnogo; dah Gospodnji kao potok sumporni upaliæe ga.
Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.

< Isaija 30 >