< Postanak 31 >

1 A Jakov èu gdje sinovi Lavanovi govore: Jakov uze sve što bješe našega oca, i od onoga što bješe našega oca steèe sve ovo blago.
Yakobo akawasikia wana wa Labani wakisema, “Yakobo amechukua kila kitu kilichokuwa cha baba yetu naye amepata utajiri huu wote kutokana na vile vilivyokuwa mali ya baba yetu.”
2 I vidje Jakov gdje lice Lavanovo nije prema njemu kao prije.
Yakobo akatambua kwamba moyo wa Labani kwake haukuwa kama ulivyokuwa mwanzo.
3 I Gospod reèe Jakovu: vrati se u zemlju otaca svojih i u rod svoj, i ja æu biti s tobom.
Ndipo Bwana akamwambia Yakobo, “Rudi katika nchi ya baba zako na kwa watu wako, nami nitakuwa pamoja nawe.”
4 I poslav Jakov dozva Rahilju i Liju u polje k stadu svojemu.
Hivyo Yakobo akatuma ujumbe kwa Raheli na Lea waje machungani yalikokuwa makundi yake.
5 I reèe im: vidim gdje lice oca vašega nije prema meni kao prije; ali je Bog oca mojega bio sa mnom.
Akawaambia, “Naona moyo wa baba yenu kwangu sivyo kama ulivyokuwa mwanzoni, lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami.
6 I vi znate da sam služio ocu vašemu kako sam god mogao;
Mnajua kwamba nimemtumikia baba yenu kwa nguvu zangu zote,
7 A otac me je vaš varao i mijenjao mi platu deset puta; ali mu Bog ne dade da me ošteti;
hata hivyo baba yenu amenidanganya kwa kubadilisha ujira wangu mara kumi. Hata hivyo, Mungu hakumruhusu kunidhuru.
8 Kad on reèe: što bude šareno neka ti je plata, onda se mladilo sve šareno; a kad reèe: s biljegom što bude neka ti je plata, onda se mladilo sve s biljegom.
Kama alisema, ‘Wenye madoadoa watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye madoadoa, kama alisema, ‘Wenye mistari watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye mistari.
9 Tako Bog uze stoku ocu vašemu i dade je meni;
Hivyo Mungu amechukua mifugo ya baba yenu na amenipa mimi.
10 Jer kad se upaljivaše stoka, podigoh oèi svoje i vidjeh u snu, a to ovnovi i jarci što skaèu na ovce i koze bijahu šareni, s biljegama prutastim i kolastim.
“Wakati fulani majira ya kuzaliana niliota ndoto ambayo niliinua macho na kuona kwamba wale mabeberu waliokuwa wakipanda kundi walikuwa wa mistari, madoadoa na mabakabaka.
11 A anðeo Gospodnji reèe mi u snu: Jakove! A ja odgovorih: evo me.
Malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, ‘Yakobo.’ Nikamjibu, ‘Mimi hapa.’
12 A on reèe: podigni sad oèi svoje i gledaj, ovnovi i jarci što skaèu na ovce i koze, šareni su, s biljegama prutastim i kolastim; jer vidjeh sve što ti èini Lavan.
Akasema, ‘Inua macho yako uone wale mabeberu wote wanaopanda kundi wana mistari, madoadoa au mabakabaka, kwa maana nimeona yale yote ambayo Labani amekuwa akikutendea.
13 Ja sam Bog od Vetilja, gdje si prelio kamen i uèinio mi zavjet; ustani sada i idi iz ove zemlje, i vrati se na postojbinu svoju.
Mimi ndiye Mungu wa Betheli, ulikomiminia ile nguzo mafuta na pale mahali uliponiwekea nadhiri. Sasa ondoka katika nchi hii mara moja urudi katika nchi uliyozaliwa.’”
14 Tada odgovori Rahilja i Lija, i rekoše mu: eda li još imamo kakav dio i našljedstvo u domu oca svojega?
Ndipo Raheli na Lea wakajibu, “Je bado tu tunalo fungu lolote katika urithi wa nyumba ya baba yetu?
15 Nije li nas držao kao tuðinke kad nas je prodao? pa je još i naše novce jednako jeo.
Je, yeye hatuhesabu sisi kama wageni? Sio kwamba ametuuza tu, bali ametumia hata na vile vilivyolipwa kwa ajili yetu.
16 Jer sve ovo blago što uze Gospod ocu našemu, naše je i naše djece. Zato èini sve što ti je Gospod kazao.
Hakika utajiri wote ambao Mungu ameuchukua kutoka kwa baba yetu ni mali yetu na watoto wetu. Hivyo fanya lolote lile Mungu alilokuambia.”
17 I podiže se Jakov, i metnu djecu svoju i žene svoje na kamile;
Ndipo Yakobo akawapandisha watoto wake na wake zake juu ya ngamia,
18 I odvede svu stoku svoju i sve blago što bješe stekao, stoku koju bješe stekao u Padan-Aramu, i poðe k Isaku ocu svojemu u zemlju Hanansku.
naye akawaswaga wanyama wote mbele yake pamoja na vitu vyote alivyokuwa amechuma huko Padan-Aramu kwenda kwa baba yake Isaki katika nchi ya Kanaani.
19 A Lavan bješe otišao da striže ovce svoje; i Rahilja ukrade idole ocu svojemu.
Labani alipokuwa amekwenda kukata kondoo wake manyoya, Raheli aliiba miungu ya nyumba ya baba yake.
20 I Jakov otide kradom od Lavana Sirina ne javivši mu da hoæe da ide.
Zaidi ya hayo, Yakobo alimdanganya Labani Mwaramu kwa kutokumwambia kwamba anakimbia.
21 I pobježe sa svijem blagom svojim, i podiže se te prijeðe preko vode, i uputi se ka gori Galadu.
Hivyo akakimbia pamoja na vitu vyote alivyokuwa navyo na kuvuka Mto Frati akaelekea nchi ya vilima katika Gileadi.
22 A treæi dan javiše Lavanu da je pobjegao Jakov.
Siku ya tatu Labani akaambiwa kwamba Yakobo amekimbia.
23 I uze sa sobom braæu svoju, i poðe za njim u potjeru, i za sedam dana stiže ga na gori Galadu.
Akiwachukua jamaa zake, akamfuatia Yakobo kwa siku saba na kumkuta kwenye nchi ya vilima katika Gileadi.
24 Ali Bog doðe Lavanu Sirinu noæu u snu, i reèe mu: èuvaj se da ne govoriš s Jakovom ni lijepo ni ružno.
Ndipo Mungu akamjia Labani Mwaramu katika ndoto usiku na kumwambia, “Jihadhari usiseme neno lolote kwa Yakobo, liwe zuri au baya.”
25 I stiže Lavan Jakova; a Jakov bješe razapeo šator svoj na gori, pa i Lavan takoðer razape svoj s braæom svojom na gori Galadu.
Yakobo alikuwa amepiga hema lake katika nchi ya vilima katika Gileadi wakati Labani alipomkuta, Labani na jamaa yake wakapiga kambi huko pia.
26 I Lavan reèe Jakovu: šta uèini te kradom pobježe od mene i odvede kæeri moje kao na maè otete?
Ndipo Labani akamwambia Yakobo, “Umefanya nini? Umenidanganya na umewachukua binti zangu kama mateka katika vita.
27 Zašto tajno pobježe i kradom otide od mene? niti mi reèe da te ispratim s veseljem i s pjesmama, s bubnjima i guslama?
Kwa nini ulikimbia kwa siri na kunidanganya? Kwa nini hukuniambia ili nikuage kwa furaha na nyimbo za matari na vinubi?
28 Niti mi dade da izljubim sinove svoje i kæeri svoje? ludo si radio.
Hata hukuniruhusu niwabusu wajukuu zangu na kuwaaga binti zangu. Umefanya kitu cha kipumbavu.
29 Mogao bih vam dosaditi; ali Bog oca vašega noæas mi reèe govoreæi: èuvaj se da ne govoriš s Jakovom ni lijepo ni ružno.
Nina uwezo wa kukudhuru, lakini usiku uliopita Mungu wa baba yako alisema nami, akaniambia, ‘Jihadhari, usiseme neno lolote kwa Yakobo liwe zuri au baya.’
30 Idi dakle kad si se tako uželio kuæe oca svojega; ali zašto ukrade bogove moje?
Sasa umeondoka kwa sababu umetamani kurudi nyumbani kwa baba yako. Lakini kwa nini umeiba miungu yangu?”
31 A Jakov odgovori i reèe: bojah se i mišljah: hoæeš silom oteti kæeri svoje od mene.
Yakobo akamjibu Labani, “Niliogopa, kwa sababu nilifikiri ungeweza kuninyangʼanya binti zako kwa nguvu.
32 A bogove svoje u koga naðeš, onaj neka ne živi više; pred našom braæom traži što je tvoje u mene, pa uzmi. Jer Jakov nije znao da ih je ukrala Rahilja.
Lakini kama ukimkuta yeyote aliye na miungu yako, hataishi. Mbele ya jamaa yetu, angalia mwenyewe uone kama kuna chochote chako hapa nilicho nacho, kama kipo, kichukue.” Basi Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameiba hiyo miungu.
33 I uðe Lavan u šator Jakovljev i u šator Lijin i u šator dviju robinja, i ne naðe ih; i izašav iz šatora Lijina uðe u šator Rahiljin.
Kwa hiyo Labani akaingia ndani ya hema la Yakobo na ndani ya hema la Lea na ndani ya hema la watumishi wawili wa kike, lakini hakukuta chochote. Baadaye alipotoka katika hema la Lea, akaingia hema la Raheli.
34 A Rahilja uze idole i sakri ih pod samar kamile svoje i sjede ozgo; i Lavan pipaše po cijelom šatoru, i ne naðe.
Basi Raheli ndiye alikuwa amechukua ile miungu ya nyumbani kwao na kuiweka katika matandiko ya ngamia na kukalia. Labani akatafuta kila mahali kwenye hema lakini hakupata chochote.
35 A ona reèe ocu svojemu: nemoj se srditi, gospodaru, što ti ne mogu ustati, jer mi je što u žena biva. Traživ dakle ne naðe idola svojih.
Raheli akamwambia baba yake, “Usikasirike, bwana wangu kwa kuwa siwezi kusimama ukiwepo, niko katika hedhi.” Labani akatafuta lakini hakuweza kuipata miungu ya nyumbani kwake.
36 I Jakov se rasrdi, i stade koriti Lavana, i govoreæi reèe mu: šta sam uèinio, šta sam skrivio, te si me tako žestoko tjerao?
Yakobo akakasirika na kumshutumu Labani, akisema, “Uhalifu wangu ni nini?” Akamuuliza Labani, “Ni dhambi gani niliyofanya hata unaniwinda?
37 Pipao si sav prtljag moj, pa šta si našao iz svoje kuæe? daj ovamo pred moju i svoju braæu, neka rasude izmeðu nas dvojice.
Sasa kwa kuwa umepekua vitu vyangu vyote umepata nini kilicho cha nyumbani mwako? Kiweke hapa mbele ya jamaa yako na yangu, nao waamue kati yetu sisi wawili.
38 Evo dvadeset godina bijah kod tebe: ovce tvoje i koze tvoje ne jaloviše se, a ovnova iz stada tvojega ne jedoh.
“Mpaka sasa nimekuwa pamoja nawe miaka ishirini. Kondoo wako na mbuzi wako hawajaharibu mimba, wala sijala kondoo dume kutoka makundi yako.
39 Što bi zvijerje zaklalo nijesam ti donosio, sam sam podmirivao; od mene si iskao što bi mi bilo ukradeno danju ili noæu.
Sikukuletea mfugo aliyeraruliwa na wanyama pori, nilibeba hasara mimi mwenyewe. Tena ulinidai malipo kwa chochote kilichoibwa mchana au usiku.
40 Danju me ubijaše vruæina a noæu mraz; i san mi ne padaše na oèi.
Hii ndiyo iliyokuwa hali yangu: Niliumia kwa joto la mchana na baridi usiku, pia usingizi ulinipa.
41 Tako mi je bilo dvadeset godina u tvojoj kuæi; služio sam ti èetrnaest godina za dvije kæeri tvoje i šest godina za stoku tvoju, i platu si mi mijenjao deset puta.
Ilikuwa hivi kwa miaka ile ishirini niliyokuwa nyumbani kwako. Nilikutumikia miaka ile kumi na minne kwa ajili ya binti zako wawili, miaka sita kwa ajili ya makundi yako, nawe ulibadilisha ujira wangu mara kumi.
42 Da nije Bog oca mojega, Bog Avramov, i strah Isakov bio sa mnom, bi me zacijelo otpustio prazna. Ali je Bog vidio nevolju moju i trud ruku mojih, pa te ukori noæas.
Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Abrahamu na Hofu ya Isaki, hakuwa pamoja nami, hakika ungenifukuza mikono mitupu. Lakini Mungu ameona taabu yangu na kazi ngumu ya mikono yangu, naye usiku uliopita amekukemea.”
43 A Lavan odgovori Jakovu i reèe: ove su kæeri moje kæeri, i ovi su sinovi moji sinovi, i ova stoka moja stoka, i što god vidiš sve je moje; pa šta bih uèinio danas kæerima svojim ili sinovima njihovijem koje rodiše?
Labani akamjibu Yakobo, “Wanawake hawa ni binti zangu, watoto hawa ni watoto wangu na makundi haya ni makundi yangu. Vyote unavyoviona ni vyangu. Lakini hata hivyo ninaweza kufanya nini kuhusu hawa binti zangu, au kuhusu watoto waliowazaa?
44 Nego hajde da uhvatimo vjeru, ja i ti, da bude svjedoèanstvo izmeðu mene i tebe.
Njoo sasa na tufanye agano, wewe na mimi, na liwe kama shahidi kati yetu.”
45 I Jakov uze kamen i utvrdi ga za spomen.
Hivyo Yakobo akachukua jiwe, akalisimamisha kama nguzo.
46 I reèe Jakov braæi svojoj: nakupite kamenja. I nakupiše kamenja i složiše na gomilu, i jedoše na gomili.
Akawaambia jamaa yake, “Kusanyeni mawe.” Hivyo wakachukua mawe na kuyakusanya yakawa lundo, wakala chakula hapo karibu na hilo lundo.
47 I Lavan ga nazva Jegar-Sahadut, a Jakov ga nazva Galed.
Labani akaliita Yegar-Sahadutha na Yakobo akaliita Galeedi.
48 I reèe Lavan: ova gomila neka bude svjedok izmeðu mene i tebe danas. Zato se prozva Galed.
Labani akasema, “Lundo hili ni shahidi kati yako na mimi leo.” Ndiyo maana likaitwa Galeedi.
49 A prozva se i Mispa, jer reèe Lavan: neka Gospod gleda izmeðu mene i tebe, kad ne uzmožemo vidjeti jedan drugoga.
Pia liliitwa Mispa, kwa sababu alisema, “Bwana na aweke ulinzi kati yako na mimi wakati kila mmoja akiwa mbali na mwingine.
50 Ako ucvijeliš kæeri moje i ako uzmeš žene preko mojih kæeri, neæe èovjek biti izmeðu nas, nego gle Bog svjedok izmeðu mene i tebe.
Kama ukiwatenda mabaya binti zangu au ukioa wake wengine zaidi ya binti zangu, hata ingawa hakuna hata mmoja aliye pamoja nasi, kumbuka kwamba Mungu ni shahidi kati yako na mimi.”
51 I još reèe Lavan Jakovu: gledaj ovu gomilu i gledaj ovaj spomenik, koji podigoh izmeðu sebe i tebe.
Pia Labani akamwambia Yakobo, “Hili ndilo lundo, na hii ndiyo nguzo niliyoisimamisha kati yako na mimi.
52 Svjedok je ova gomila i svjedok je ovaj spomenik: da ni ja neæu prijeæi preko ove gomile k tebi ni ti k meni da neæeš prijeæi preko ove gomile i spomenika ovoga na zlo.
Lundo hili ni shahidi na nguzo hii ni shahidi, kwamba sitavuka lundo hili kuja upande wako kukudhuru, nawe kwamba hutavuka lundo hili na nguzo hii kuja upande wangu kunidhuru.
53 Bog Avramov i bogovi Nahorovi, bogovi oca njihova, neka sude meðu nama. A Jakov se zakle strahom oca svojega Isaka.
Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Nahori, Mungu wa baba zao, aamue kati yetu.” Hivyo Yakobo akaapa kwa jina la Hofu ya baba yake Isaki.
54 I Jakov prinese žrtvu na gori, i sazva braæu svoju na veèeru; i jedoše pa noæiše na gori.
Yakobo akatoa dhabihu juu ya kilima na akawaalika jamaa zake kula chakula. Baada ya kula, wakalala huko.
55 A ujutru rano usta Lavan, i izljubi svoju unuèad i kæeri svoje, i blagoslovi ih, pa otide i vrati se u svoje mjesto.
Kesho yake asubuhi na mapema, Labani akawabusu wajukuu zake, binti zake na kuwabariki. Kisha akaondoka, akarudi nyumbani.

< Postanak 31 >