< Postanak 21 >
1 I Gospod pohodi Saru, kao što bješe rekao, i uèini Gospod Sari kao što bješe kazao.
Yahwe akamsikiliza Sara kwa umakini kama alivyo kuwa amemwambia, Yahwe akamfanyia Sara kama alivyo kuwa amemwahidi.
2 Jer zatrudnje i rodi Sara Avramu sina u starosti njegovoj u isto vrijeme kad kaza Gospod.
Sara akachukua mimba na akamzalia Abraham mtoto wa kiume katika uzee wake, katika muda ule ule ambao Mungu alikuwa amemwambia.
3 I Avram nadjede ime sinu koji mu se rodi, kojega mu rodi Sara, Isak.
Abraham akamwita jina mwanawe, ambaye alizaliwa kwake, na Sara, Isaka.
4 I obreza Avram sina svojega Isaka kad bi od osam dana, kao što mu zapovjedi Bog.
Abraham akamtahiri mwanawe Isaka alipofikisha siku nane, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza.
5 A Avramu bješe sto godina kad mu se rodi sin Isak.
Abraham alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwanawe Isaka anazaliwa kwake.
6 A Sara reèe: Bog mi uèini smijeh; ko god èuje, smijaæe mi se.
Sara akasema, “Mungu amenifanya nicheke; kila mtu atakaye sikia atacheka pamoja na nami.”
7 I reèe: ko bi rekao Avramu da æe Sara dojiti djecu? ipak mu rodih sina u starosti njegovoj.
Pia akasema, “Nani angesema kwa Abraham kwamba Sara atalea mtoto, na sasa kweli nimemzalia mtoto wakiume katika uzee wake!”
8 A kad dijete doraste da se odbije od sise, uèini Avram veliku gozbu onaj dan kad odbiše Isaka od sise.
Mtoto akakua na akaachishwa kunyonya, na Abraham akafanya sherehe kubwa katika siku ambayo Isaka aliachishwa.
9 I Sara vidje sina Agare Misirke, koja ga rodi Avramu, gdje se potsmijeva;
Sara akamwona mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alikuwa amezaliwa kwa Abraham, akidhihaki.
10 Pa reèe Avramu: otjeraj ovu robinju sa sinom njezinijem, jer sin ove robinje neæe biti našljednik s mojim sinom, s Isakom.
Kwa hiyo akamwambia Abraham, “Mfukuze huyu mwanamke huyu mtumwa pamoja na mtoto wake: kwa kuwa mtoto huyu wa mwanamke mtumwa hawezi kuwa mrithi pamoja na mwanangu Isaka.”
11 A to Avramu bi vrlo krivo radi sina njegova.
Jambo hili likamuhuzunisha sana Abraham kwa sababu ya mwanawe.
12 Ali Bog reèe Avramu: nemoj da ti je krivo radi djeteta i radi robinje tvoje. Što ti je god kazala Sara, poslušaj; jer æe ti se u Isaku sjeme prozvati.
Lakini Mungu akamwambia Abraham, “Usihuzunike kwa sababu ya kijana huyu, na kwa sababu ya mwanamke huyu mtumwa wako. Sikiliza maneno asemayo Sara juu ya jambo hili, kwa sababu itakuwa kupitia Isaka kwamba uzao wako utaitwa.
13 Ali æu i od sina robinjina uèiniti narod, jer je tvoje sjeme.
Nitamfanya pia mtoto wa mjakazi kuwa taifa, kwa sababu ni uzao wako.”
14 I Avram ustav ujutru rano, uze hljeba i mješinu vode, i dade Agari metnuvši joj na leða, i dijete, i otpusti je. A ona otišavši lutaše po pustinji Virsavskoj.
Abraham akaamka asubuhi na mapema, akachukua mkate na kiriba cha maji, akampatia Hajiri, akiweka juu ya bega lake. Akamtoa kijana akampatia Hajiri na akawaondoa. Hajiri akaondoka akapotea katika jangwa la Beerisheba.
15 A kad nesta vode u mješini, ona baci dijete pod jedno drvo,
Maji yalipokwisha kwenye kiriba akamtelekeza kijana katika moja ya vichaka.
16 Pa otide koliko se može strijelom dobaciti, i sjede prema njemu; jer govoraše: da ne gledam kako æe umrijeti dijete. I sjedeæi prema njemu stade iza glasa plakati.
Kisha akaondoka, na akakaa umbali kidogo na yule kijana, umbali kama wa kutupa mshale, kwa vile alisema, “Na nisitazame kifo cha mtoto.” Alipokuwa amekaa kumkabili, akapaza sauti yake akalia.
17 A Bog èu glas djetinji, i anðeo Božji viknu s neba Agaru, i reèe joj: što ti je, Agaro? ne boj se, jer Bog èu glas djetinji odande gdje je.
Mungu akasikia kilio cha kijana, na malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, “Nini kinakusumbua? Usiogope, kwa kuwa Mungu amesikia kilio cha kijana mahali alipo.
18 Ustani, digni dijete i uzmi ga u naruèje; jer æu od njega uèiniti velik narod.
Inuka msimamishe mtoto, na umtie moyo; kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
19 I Bog joj otvori oèi, te ugleda studenac; i otišavši napuni mješinu vode, i napoji dijete.
Kisha Mungu akayafunua macho ya Hajiri, natazama akaona kisima cha maji. Akaenda akajaza kiriba maji, na akampatia kijana akanywa.
20 I Bog bijaše s djetetom, te odraste, i življaše u pustinji, i posta strijelac.
Mungu akawa pamoja na kijana, na akakua. Akaishi jangwani akawa mwindaji.
21 A življaše u pustinji Faranu. I mati ga oženi iz zemlje Misirske.
Akaishi katka jangwa la Parani, na mama yake akampatia mke kutoka Misri.
22 U to vrijeme reèe Avimeleh i Fihol vojvoda njegov Avramu govoreæi: Bog je s tobom u svemu što radiš.
Ikawa kwamba katika wakati ule Abimeleki na Fikoli kamanda wa jeshi lake akamwambia Abraham, akisema, “Mungu yuko pamoja na wewe katika yote uyatendayo.
23 Zakuni mi se sada Bogom da neæeš prevariti mene ni sina mojega ni unuka mojega, nego da æeš dobro onako kako sam ja tebi èinio i ti èiniti meni i zemlji u kojoj si došljak.
Sasa niapie kwa Mungu kwamba hutanifanyia baya, wala mwanangu, wala uzao wangu. Onesha kwangu na kwa nchi ambayo umekuwa ukikaa agano lile lile la uaminifu ambalo nimekuonesha wewe.”
24 A Avram reèe: hoæu se zakleti.
Abraham akasema, “Nina apa.”
25 Ali Avram prekori Avimeleha za studenac, koji uzeše na silu sluge Avimelehove.
Abraham pia akamlalamikia Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki wamekinyang'anya.
26 A Avimeleh reèe: ne znam ko je to uèinio; niti mi ti kaza, niti èuh do danas.
Abimeleki akasema, “Sijui ni nani amefanya jambo hili. Hukuniambia mapema; na sijalisikia ila leo hii.”
27 Tada Avram uze ovaca i goveda, i dade Avimelehu, i uhvatiše vjeru meðu sobom.
Kwa hiyo Abraham akachukua kondoo na ng'ombe maksai akampatia Abimeleki, na wawili hawa wakafanya agano.
28 I Avram odluèi sedam jaganjaca iz stada.
Kisha Abraham akatenga wanakondoo wa kike saba pekeyao.
29 A Avimeleh reèe Avramu: šta æe ono sedam jaganjaca što si odluèio?
Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini maana ya hawa wanakondoo wa kike saba ambao umewatenga pekeyao?”
30 A on odgovori: da primiš iz moje ruke ono sedam jaganjaca, da mi bude svjedoèanstvo da sam ja iskopao ovaj studenac.
Akajibu, “Hawa wanakondoo wa kike saba utawapokea kutoka mkonono mwangu, ili kwamba uwe ushahidi kwangu, kuwa nichimba kisima hiki.”
31 Otuda se prozva ono mjesto Vir-Saveja, jer se ondje zakleše obojica.
Kwa hiyo akaita mahali pale Beerisheba, kwa sababu mahali pale wote wawili wali apa kiapo.
32 Tako uhvatiše vjeru na Virsaveji. Tada se diže Avimeleh i Fihol vojvoda njegov, i vratiše se u zemlju Filistejsku.
Walifanya agano hapo Bersheba, kisha Abimeleki na Fikoli, amiri wa jeshi, wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
33 A Avram posadi lug na Virsaveji, i ondje prizva ime Gospoda Boga vjeènoga.
Abraham akapanda mti wa mkwaju katika Beerisheba. Na pale akamwabudu Yahwe, Mungu wa milele.
34 I Avram življaše kao došljak u zemlji Filistejskoj mnogo vremena.
Abraham akasalia kuwa mgeni katika nchi ya Wafilisti kwa siku nyingi.