< Postanak 11 >
1 A bijaše na cijeloj zemlji jedan jezik i jednake rijeèi.
Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
2 A kad otidoše od istoka, naðoše ravnicu u zemlji Senarskoj, i naseliše se ondje.
Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
3 Pa rekoše meðu sobom: hajde da pravimo ploèe i da ih u vatri peèemo. I bjehu im opeke mjesto kamena i smola zemljana mjesto kreèa.
Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
4 Poslije rekoše: hajde da sazidamo grad i kulu, kojoj æe vrh biti do neba, da steèemo sebi ime, da se ne bismo rasijali po zemlji.
Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
5 A Gospod siðe da vidi grad i kulu, što zidahu sinovi èovjeèiji.
Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
6 I reèe Gospod: gle, narod jedan, i jedan jezik u svijeh, i to poèeše raditi, i neæe im smetati ništa da ne urade što su naumili.
Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
7 Hajde da siðemo, i da im pometemo jezik, da ne razumiju jedan drugoga što govore.
Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
8 Tako ih Gospod rasu odande po svoj zemlji, te ne sazidaše grada.
Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
9 Zato se prozva Vavilon, jer ondje pomete Gospod jezik cijele zemlje, i odande ih rasu Gospod po svoj zemlji.
Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
10 Ovo je pleme Simovo: bijaše Simu sto godina, kad rodi Arfaksada, druge godine poslije potopa.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
11 A rodiv Arfaksada poživje Sim pet stotina godina, raðajuæi sinove i kæeri.
Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
12 A Arfaksad poživje trideset i pet godina, i rodi Salu;
Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
13 A rodiv Salu poživje Arfaksad èetiri stotine i tri godine, raðajuæi sinove i kæeri.
Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
14 A Sala poživje trideset godina, i rodi Evera;
Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 A rodiv Evera poživje Sala èetiri stotine i tri godine, raðajuæi sinove i kæeri.
Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
16 A Ever poživje trideset i èetiri godine, i rodi Faleka;
Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 A rodiv Faleka poživje Ever èetiri stotine i trideset godina, raðajuæi sinove i kæeri.
Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
18 A Falek poživje trideset godina i rodi Ragava;
Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 A rodiv Ragava poživje Falek dvjesta i devet godina, raðajuæi sinove i kæeri.
Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
20 A Ragav poživje trideset i dvije godine i rodi Seruha;
Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
21 A rodiv Seruha poživje Ragav dvjesta i sedam godina, raðajuæi sinove i kæeri.
Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
22 A Seruh poživje trideset godina, i rodi Nahora;
Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 A rodiv Nahora poživje Seruh dvjesta godina, raðajuæi sinove i kæeri.
Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
24 A Nahor poživje dvadeset i devet godina, i rodi Taru;
Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 A rodiv Taru poživje Nahor sto i devetnaest godina, raðajuæi sinove i kæeri.
Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
26 A Tara poživje sedamdeset godina, i rodi Avrama, Nahora i Arana.
Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
27 A ovo je pleme Tarino: Tara rodi Avrama, Nahora i Arana; a Aran rodi Lota.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
28 I umrije Aran prije Tare oca svojega na postojbini svojoj, u Uru Haldejskom.
Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
29 I oženi se Avram i Nahor, i ženi Avramovoj bješe ime Sara a ženi Nahorovoj ime Melha, kæi Arama oca Melhe i Jeshe.
Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
30 A Sara bješe nerotkinja, i ne imaše poroda.
Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
31 I uze Tara sina svojega Avrama i Lota sina Aranova, unuka svojega, i Saru snahu svoju, ženu Avrama sina svojega; i poðoše zajedno iz Ura Haldejskoga da idu u zemlju Hanansku, i doðoše do Harana, i ondje se nastaniše.
Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
32 I poživje Tara svega dvjesta i pet godina; i umrije Tara u Haranu.
Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.