< Postanak 10 >
1 A ovo su plemena sinova Nojevijeh, Sima, Hama i Jafeta, kojima se rodiše sinovi poslije potopa.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
2 Sinovi Jafetovi: Gamer i Magog i Madaj i Javan i Tovel i Meseh i Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
3 A sinovi Gamerovi: Ashanas i Rifat i Togarma.
Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
4 A sinovi Javanovi: Elisa i Tarsis, Kitim i Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
5 Od njih se razdijeliše ostrva narodna na zemljama svojim, svako po jeziku svojemu i po porodicama svojim, u narodima svojim.
Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
6 A sinovi Hamovi: Hus i Mesrain, Fud i Hanan.
Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
7 A sinovi Husovi: Sava i Evila i Savata i Regma i Savataka. A sinovi Regmini: Sava i Dadan.
Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
8 Hus rodi i Nevroda; a on prvi bi silan na zemlji;
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
9 Bješe dobar lovac pred Gospodom; zato se kaže: dobar lovac pred Gospodom kao Nevrod.
Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
10 A poèetak carstvu njegovu bješe Vavilon i Oreh i Arhad i Halani u zemlji Senaru.
Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
11 Iz te zemlje izaðe Asur, i sazida Nineviju i Rovot grad i Halah,
Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
12 I Dasem izmeðu Ninevije i Halaha; to je grad velik.
na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
13 A Mesrain rodi Ludeje i Enemeje i Laveje i Neftaleje,
Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
14 I Patroseje i Hasmeje, odakle izaðoše Filisteji i Gaftoreji.
Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
15 A Hanan rodi Sidona, prvenca svojega, i Heta,
Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
16 I Jevuseja i Amoreja i Gergeseja,
pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
17 I Eveja i Arukeja i Aseneja,
Mhivi, Mwarki, Msini,
18 I Aradeja i Samareja i Amateja. A poslije se rasijaše plemena Hananejska.
Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
19 I bjehu meðe Hananejske od Sidona iduæi na Gerar pa do Gaze, i iduæi na Sodom i Gomor i Adamu i Sevojim pa do Dasa.
Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
20 To su sinovi Hamovi po porodicama svojim i po jezicima svojim, u zemljama svojim i u narodima svojim.
Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
21 I Simu rodiše se sinovi, najstarijemu bratu Jafetovu, ocu svijeh sinova Everovijeh.
Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
22 Sinovi Simovi bjehu: Elam i Asur i Arfaksad i Lud i Aram.
Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
23 A sinovi Aramovi: Uz i Ul i Gater i Mas.
Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
24 A Arfaksad rodi Salu, a Sala rodi Evera.
Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
25 A Everu se rodiše dva sina: jednom bješe ime Falek, jer se u njegovo vrijeme razdijeli zemlja, a bratu njegovu ime Jektan.
Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
26 A Jektan rodi Elmodada i Saleta i Sarmota i Jaraha,
Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 I Odora i Evila i Deklu,
Hadoram, Uzali, Dikla,
28 I Evala i Avimaila i Savu,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 I Ufira i Evilu i Jovava; ti svi bjehu sinovi Jektanovi.
Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 I življahu od Mase, kako se ide na Safir do gora istoènijeh.
Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
31 To su sinovi Simovi po porodicama svojim i po jezicima svojim, u zemljama svojim i u narodima svojim;
Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
32 To su porodice sinova Nojevijeh po plemenima svojim, u narodima svojim; i od njih se razdijeliše narodi po zemlji poslije potopa.
Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.