< Jezekilj 21 >

1 I doðe mi rijeè Gospodnja govoreæi:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Sine èovjeèji, okreni lice svoje prema Jerusalimu, i pokaplji prema svetijem mjestima, i prorokuj protiv zemlje Izrailjeve.
“Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
3 I reci zemlji Izrailjevoj: ovako veli Gospod: evo me na te; izvuæi æu maè svoj iz korica, i istrijebiæu iz tebe pravednoga i bezbožnoga.
uiambie: ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
4 Da istrijebim iz tebe pravednoga i bezbožnoga, zato æe izaæi maè moj iz korica svojih na svako tijelo od juga do sjevera.
Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utakuwa wazi dhidi ya kila mmoja kuanzia kusini mpaka kaskazini.
5 I poznaæe svako tijelo da sam ja Gospod izvukao maè svoj iz korica njegovijeh, neæe se više vratiti.
Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Bwana nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
6 A ti, sine èovjeèji, uzdiši kao da su ti bedra polomljena, i gorko uzdiši pred njima.
“Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
7 A kada ti reku: zašto uzdišeš? ti reci: za glas što ide, od kojega æe se rastopiti svako srce i klonuti sve ruke i svakoga æe duha nestati, i svaka æe koljena postati kao voda; evo, ide, i navršiæe se, govori Gospod Gospod.
Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatokea, asema Bwana Mwenyezi.”
8 Potom doðe mi rijeè Gospodnja govoreæi:
Neno la Bwana likanijia, kusema:
9 Sine èovjeèji, prorokuj i reci: ovako veli Gospod Gospod: reci: maè, maè je naoštren, i uglaðen je.
“Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
10 Naoštren je da kolje, uglaðen je da sijeva; hoæemo li se radovati kad prut sina mojega ne haje ni za kako drvo?
umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ungʼae kama umeme wa radi! “‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unaidharau kila fimbo ya namna hiyo.
11 Dao ga je da se ugladi da se uzme u ruku; maè je naoštren i uglaðen, da se da u ruku ubici.
“‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
12 Vièi i ridaj, sine èovjeèji; jer on ide na narod moj, na sve knezove Izrailjeve; pod maè æe biti okrenuti s narodom mojim, zato udri se po bedru.
Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
13 Kad bješe karanje, šta bi? eda li ni od pruta koji ne haje neæe biti ništa? govori Gospod Gospod.
“‘Kwa maana upanga huu umejaribiwa na kuhakikishwa, itakuwaje basi fimbo ya ufalme ya Yuda inayoudharau kama haitakuwepo tena, bali itakuwa imeondolewa kabisa? asema Bwana Mwenyezi.’
14 Ti dakle, sine èovjeèji, prorokuj i pljeskaj rukama, jer æe maè doæi i drugom i treæom, maè koji ubija, maè koji velike ubija, koji prodire u klijeti.
“Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa kuchinja, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
15 Da se rastope srca i umnoži pogibao, metnuo sam na sva vrata njihova strah od maèa; jaoh! pripravljen je da sijeva, naoštren da kolje.
Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa kuchinja kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama umeme wa radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
16 Stegni se, udri nadesno, nalijevo, kuda se god obrneš.
Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
17 Jer æu i ja pljeskati rukama, i namiriæu gnjev svoj. Ja Gospod rekoh.
Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Bwana nimesema.”
18 Još mi doðe rijeè Gospodnja govoreæi:
Neno la Bwana likanijia kusema:
19 A ti, sine èovjeèji, naèini dva puta, kuda æe doæi maè cara Vavilonskoga; iz jedne zemlje neka izlaze oba; i izberi stranu, gdje se poèinje put gradski, izberi.
“Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
20 Naèini put, kojim æe doæi maè na Ravu sinova Amonovijeh, i u Judeju na tvrdi Jerusalim.
Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
21 Jer æe car Vavilonski stati na rasputici, gdje poèinju dva puta, te æe vraèati, gladiæe strijele, pitaæe likove, gledaæe u jetru.
Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
22 Nadesno æe mu vraèanje pokazati Jerusalim da namjesti ubojne sprave, da otvori usta na klanje, da podigne glas podvikujuæi, da namjesti ubojne sprave prema vratima, da naèini opkope, da pogradi kule.
Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka vyombo vya kuvunjia boma, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka vyombo vya kuvunjia boma kwenye malango, kuweka jeshi kuzunguka na kufanya uzingiraji.
23 I uèiniæe se vraèanje zaludno zakletima, a to æe napomenuti bezakonje da se uhvate.
Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha juu ya uovu wao na kuwachukua mateka.
24 Zato ovako veli Gospod Gospod: što napominjete svoje bezakonje, te se otkriva nevjera vaša i grijesi se vaši vide u svijem djelima vašim, zato što doðoste na pamet, biæete pohvatani rukom.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: ‘Kwa sababu enyi watu mmekumbusha uovu wenu kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mfanyayo, kwa kuwa mmefanya jambo hili, mtachukuliwa mateka.
25 A ti, neèisti bezbožnièe, kneže Izrailjev, kome doðe dan kad bi na kraju bezakonje,
“‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yako imewadia, ambaye wakati wako wa adhabu umefikia kilele chake,
26 Ovako veli Gospod Gospod: skini tu kapu i svrzi taj vijenac, neæe ga biti; niskoga æu uzvisiti a visokoga æu poniziti.
hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa na aliyekwezwa atashushwa.
27 Uništiæu, uništiæu, uništiæu ga, i neæe ga biti, dokle ne doðe onaj kome pripada, i njemu æu ga dati.
Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya mpaka aje yule ambaye ndiye mwenye haki nao; yeye ndiye nitakayempa.’
28 A ti, sine èovjeèji, prorokuj i reci: ovako veli Gospod Gospod za sinove Amonove i za njihovu sramotu; reci dakle: maè, maè je izvuèen, uglaðen da kolje, da zatire, da sijeva,
“Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu Waamoni na matukano yao. “‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama umeme wa radi!
29 Dokle ti viðaju taštinu, dokle ti gataju laž, da te metnu na vratove pobijenijem bezbožnicima, kojima doðe dan kad bi kraj bezakonju.
Wakati wakitoa maono ya uongo kwa ajili yako, wanapobashiri uongo kwa ajili yako, wanakuweka wewe kwenye shingo za watu wapotovu, wale walio waovu, wale ambao siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
30 Ostavi maè u korice; na mjestu gdje si se rodio, u zemlji gdje si postao, sudiæu ti;
Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
31 I izliæu na te gnjev svoj, ognjem gnjeva svojega dunuæu na te i predaæu te u ruke žestokim ljudma, vještim u zatiranju.
Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
32 Ognju æeš biti hrana, krv æe ti biti posred zemlje, neæeš se spominjati, jer ja Gospod rekoh.
Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Bwana nimesema.’”

< Jezekilj 21 >