< Jestira 6 >

1 Onu noæ ne mogaše car spavati, i zapovjedi te mu donesoše knjigu od znamenitijeh dogaðaja, dnevnike, te je èitaše caru.
Usiku ule mfalme hakupata usingizi, hivyo akaagiza aletewe kitabu cha kumbukumbu za matukio ya utawala wake, asomewe.
2 I naðe se zapisano kako je Mardohej prokazao za Vihtana i Teresa, dva dvoranina, koji èuvahu stražu na pragu, da gledaju da dignu ruke na cara Asvira.
Kitabu hicho kilikutwa na kumbukumbu kwamba Mordekai alikuwa amefichua jinsi Bigthana na Tereshi, waliokuwa maafisa wawili wa mfalme, walinzi wa lango walivyokuwa wamepanga hila ya kumuua Mfalme Ahasuero.
3 Tada reèe car: kaka je èast i kako je dobro uèinjeno Mardoheju za to? A momci carevi, sluge njegove, rekoše: nije mu uèinjeno ništa.
Mfalme akauliza, “Je, ni heshima na shukrani gani Mordekai alipokea kwa ajili ya jambo hili?” Watumishi wake wakajibu, “Hakuna lolote alilofanyiwa.”
4 A car reèe: ko je u trijemu? A Aman bješe došao u spoljašnji trijem dvora careva da kaže caru da se objesi Mardohej na vješala koja mu je pripravio.
Mfalme akasema, “Ni nani yuko uani?” Wakati huo huo Hamani alikuwa ameingia ua wa nje wa jumba la mfalme kusema na mfalme kuhusu kumwangika Mordekai katika mahali pa kuangikia watu alipokuwa amepajenga kwa ajili yake.
5 A momci carevi rekoše mu: gle, Aman stoji u trijemu. A car reèe: neka doðe.
Watumishi wake wakamjibu, “Hamani amesimama uani.” Mfalme akaamuru, “Mleteni ndani.”
6 I Aman doðe, a car mu reèe: šta treba uèiniti èovjeku kojega car hoæe da proslavi? A Aman reèe u sebi: koga bi car htio proslaviti ako ne mene?
Hamani alipoingia, mfalme alimuuliza, “Afanyiwe nini mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu?” Basi Hamani akawaza moyoni mwake, “Ni nani mwingine ambaye mfalme angemheshimu kuliko mimi?”
7 I reèe Aman caru: koga car hoæe da proslavi,
Kwa hiyo akamjibu mfalme, “Kwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu,
8 Treba donijeti carsko odijelo koje car nosi, i dovesti konja na kom car jaše, i metnuti mu na glavu vijenac carski;
aletewe joho la kifalme ambalo mfalme ameshalivaa na farasi ambaye mfalme alishampanda, ambaye amevikwa taji ya kifalme kichwani mwake.
9 I odijelo i konja treba dati kome izmeðu najveæih knezova carevijeh da obuku èovjeka onoga kojega car hoæe da proslavi, pa da ga provedu na konju po ulicama gradskim i vièu pred njim: ovako biva èovjeku koga car hoæe da proslavi.
Kisha joho na farasi vikabidhiwe kwa mmojawapo wa wakuu wa mfalme anayeheshimika sana. Nao wamvike mtu yule ambaye mfalme anapenda kumheshimu, na aongozwe akiwa juu ya farasi kupitia barabara za mji, wakitangaza mbele yake, ‘Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme apenda kumheshimu!’”
10 Tada reèe car Amanu: brže uzmi odijelo i konja kao što reèe, i uèini tako Mardoheju, Judejcu koji sjedi na vratima carevijem; nemoj izostaviti ništa što si rekao.
Mfalme akamwamuru Hamani, “Nenda mara moja, chukua joho na farasi na ufanye kama vile ulivyopendekeza kwa Mordekai Myahudi, akaaye langoni mwa mfalme. Usipuuze kufanya kitu chochote ulichoshauri.”
11 I uze Aman odijelo i konja, i obuèe Mardoheja i provede ga na konju po ulicama gradskim vièuæi pred njim: ovako biva èovjeku koga car hoæe da proslavi.
Hivyo Hamani akachukua joho na farasi. Akamvika Mordekai, na kumpandisha juu ya farasi akamtembeza katika barabara za mji akitangaza mbele yake, “Hivi ndivyo anavyofanyiwa mtu ambaye mfalme anapenda kumheshimu!”
12 Potom se vrati Mardohej na vrata careva, a Aman brže otide kuæi svojoj žalostan i pokrivene glave.
Baadaye Mordekai akarudi kwenye lango la mfalme. Lakini Hamani akakimbia nyumbani, akiwa amejaa huzuni,
13 I pripovjedi Aman Seresi ženi svojoj i svijem prijateljima svojim sve što mu se dogodi. Tada mu rekoše mudarci njegovi i Seresa žena njegova: kad je od Judejskoga sjemena Mardohej pred kojim si poèeo padati, neæeš mu odoljeti, nego æeš pasti pred njim.
naye akamweleza Zereshi mkewe pamoja na rafiki zake wote kila kitu ambacho kimempata. Washauri wake pamoja na Zereshi mkewe wakamwambia, “Kwa kuwa Mordekai, ambaye mbele yake umeanza kuanguka ni wa asili ya Kiyahudi, huwezi kushindana naye; kwa hakika utaanguka!”
14 I dok oni još govorahu s njim, doðoše dvorani carevi i brže odvedoše Amana na objed koji zgotovi Jestira.
Walipokuwa bado wakizungumza naye, matowashi wa mfalme wakaja na kumharakisha Hamani aende katika karamu aliyoiandaa Esta.

< Jestira 6 >