< 2 Kraljevima 13 >
1 Godine dvadeset treæe carovanja Joasa sina Ohozijina nad Judom zacari se Joahaz sin Jujev nad Izrailjem u Samariji, i carova sedamnaest godina.
Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba.
2 I èinjaše što je zlo pred Gospodom, jer hoðaše za grijesima Jerovoama sina Navatova, kojima navede na grijeh Izrailja i ne otstupi od njih.
Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha.
3 Zato se razgnjevi Gospod na Izrailja i dade ih u ruke Azailu caru Sirskom i u ruke Ven-Adadu sinu Azailovu za sve ono vrijeme.
Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.
4 Ali se Joahaz pomoli Gospodu, i Gospod ga usliši, jer vidje nevolju Izrailjevu, kako ih muèi car Sirski.
Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali.
5 I dade Gospod Izrailju izbavitelja, te se oprostiše ruke Sirske, i življahu sinovi Izrailjevi u šatorima svojim kao prije.
Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali.
6 Ali ne otstupiše od grijehova doma Jerovoamova kojima na grijeh navede Izrailja, nego hodiše u njima, i sam lug još stajaše u Samariji.
Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.
7 A ne osta Joahazu naroda više od pedeset konjika i deset kola i deset tisuæa pješaka; nego ih pobi car Sirski i satr ih, te biše kao prah kad se vrše.
Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.
8 A ostala djela Joahazova i sve što je èinio, i junaštva njegova, nije li to zapisano u dnevniku careva Izrailjevijeh?
Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
9 I poèinu Joahaz kod otaca svojih, i pogreboše ga u Samariji; a na mjesto njegovo zacari se Joas sin njegov.
Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
10 Godine trideset sedme carovanja Joasova nad Judom zacari se Joas sin Joahazov nad Izrailjem u Samariji, i carova šesnaest godina.
Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita.
11 I èinjaše što je zlo pred Gospodom, ne otstupi ni od jednoga grijeha Jerovoama sina Navatova, koji navede Izrailja na grijeh, nego u njima hoðaše.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.
12 A ostala djela Joasova, i sve što je èinio, i junaštva njegova, kako je vojevao s Amasijom carem Judinijem, nije li to zapisano u dnevniku careva Izrailjevijeh?
Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
13 I poèinu Joas kod otaca svojih, a Jerovoam sjede na prijesto njegov; i pogreboše Joasa u Samariji kod careva Izrailjevijeh.
Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.
14 A Jelisije razbolje se od bolesti, od koje i umrije; i Joas car Izrailjev doðe k njemu, i plaèuæi pred njim govoraše: oèe moj, oèe moj, kola Izrailjeva i konjici njegovi!
Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”
15 A Jelisije mu reèe: uzmi luk i strijele. I on uze luk i strijele.
Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo.
16 Tada reèe caru Izrailjevu: nategni luk rukom svojom. I nateže luk rukom svojom. A Jelisije metnu ruke svoje caru na ruke.
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.
17 I reèe: otvori prozor s istoka. I otvori, a Jelisije reèe: pusti strijelu. I on pusti strijelu, a Jelisije reèe: strijela izbavljenja Gospodnjega, strijela izbavljenja od Siraca; jer æeš pobiti Sirce u Afeku, i satræeš ih.
Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.”
18 Još reèe: uzmi strijele. I uze, a on reèe caru Izrailjevu: udari u zemlju. I udari tri puta, pa stade.
Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.
19 Tada se rasrdi na nj èovjek Božji i reèe: da si udario pet puta ili šest puta, tada bi pobio Sirce sasvijem; a sada æeš ih samo tri puta razbiti.
Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”
20 Potom umrije Jelisije, i pogreboše ga. A druge godine udariše èete Moavske na zemlju.
Elisha akafa, nao wakamzika. Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli.
21 I dogodi se kad pogrebavahu nekoga èovjeka, ugledaše èetu i baciše èovjeka u grob Jelisijev; i kad èovjek pade i dotaèe se kostiju Jelisijevih, oživje i usta na noge svoje.
Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.
22 A Azailo car Sirski muèaše Izrailja svega vijeka Joahazova.
Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi.
23 Ali se Gospodu sažali za njima i smilova se na njih i pogleda na njih zavjeta radi svojega s Avramom, Isakom i Jakovom, i ne htje ih istrijebiti i ne odvrže ih od sebe do sada.
Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.
24 I umrije Azailo car Sirski, i na njegovo se mjesto zacari Ven-Adad sin njegov.
Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 A Joas sin Joahazov povrati iz ruke Ven-Adada sina Azailova gradove koje bješe Azailo uzeo ratom Joahazu ocu njegovu; tri puta ga razbi Joas, i povrati gradove Izrailjeve.
Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.