< 1 Samuelova 26 >
1 Opet doðoše Zifeji k Saulu u Gavaju govoreæi: ne krije li se David na brdu Eheli prema Gesimonu?
Hao Wazifu wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hakujificha katika kilima cha Hakila, kinachotazamana na Yeshimoni?”
2 A Saul se podiže i siðe u pustinju Zifsku, i s njim tri tisuæe ljudi izabranijeh iz Izrailja, da traži Davida u pustinji Zifskoj.
Hivyo Sauli akashuka kwenda katika Jangwa la Zifu, akiwa na watu wake 3,000 wa Israeli waliochaguliwa, kumsaka Daudi huko.
3 I stade Saul u oko na brdu Eheli prema Gesimonu kraj puta; a David osta u pustinji, i opazi da Saul ide za njim u pustinju.
Sauli akapiga kambi yake kando ya barabara juu ya kilima cha Hakila kinachotazamana na Yeshimoni, lakini Daudi alikuwa anaishi huko jangwani. Alipoona kuwa Sauli amemfuata huko,
4 I posla David uhode, i od njih dozna zacijelo da je došao Saul.
Daudi akatuma wapelelezi na akapata habari kwa hakika kwamba Sauli alikuwa amewasili.
5 Tada se podiže David i doðe na mjesto gdje Saul bijaše s vojskom. I David vidje mjesto gdje spavaše Saul i Avenir sin Nirov vojvoda njegov; a spavaše Saul meðu kolima a narod ležaše oko njega.
Ndipo Daudi akaondoka, akaenda hadi mahali Sauli alikuwa amepiga kambi. Akaona mahali Sauli na Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi, walipokuwa wamelala. Sauli alikuwa amelala ndani ya kambi, jeshi likiwa limemzunguka.
6 I David progovori i reèe Ahimelehu Hetejinu i Avisaju sinu Serujinu bratu Joavovu: ko æe siæi sa mnom k Saulu u oko? A Avisaj odgovori: ja æu siæi s tobom.
Basi Daudi akamuuliza Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, nduguye Yoabu, akisema, “Ni nani atakayeshuka pamoja nami kambini kwa Sauli?” Abishai akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe.”
7 I tako David i Avisaj doðoše noæu k narodu; a gle, Saul ležaše i spavaše izmeðu kola, i koplje mu bješe èelo glave pobodeno u zemlju; Avenir pak i narod ležahu oko njega.
Hivyo Daudi na Abishai wakaenda kwenye jeshi wakati wa usiku, tazama Sauli, alikuwa amelala ndani ya kambi na mkuki wake umekitwa ardhini karibu na kichwa chake. Abneri na askari walikuwa wamelala kumzunguka Sauli.
8 Tada reèe Avisaj Davidu: danas ti dade Bog neprijatelja tvojega u ruke; zato sada da ga probodem kopljem za zemlju jedanput, neæu više.
Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemtia adui yako mikononi mwako. Sasa niruhusu nimchome mpaka ardhini kwa pigo moja la mkuki wangu; sitamchoma mara mbili.”
9 A David reèe Avisaju: nemoj ga ubiti; jer ko æe podignuti ruku svoju na pomazanika Gospodnjega i biti prav?
Lakini Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize! Ni nani awezaye kutia mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana na asiwe na hatia?”
10 Još reèe David: tako živ bio Gospod, Gospod æe ga ubiti, ili æe doæi dan njegov da umre, ili æe izaæi u boj i poginuti.
Daudi akasema, “Hakika kama vile Bwana aishivyo, Bwana mwenyewe atampiga; au wakati wake utafika, naye atakufa, au atakwenda vitani na kuangamia.
11 Ne dao mi Bog da dignem ruku svoju na pomazanika Gospodnjega! Nego uzmi sada koplje što mu je èelo glave i èašu za vodu, pa da idemo.
Lakini Mungu na apishie mbali nisije nikainua mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana. Sasa chukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyo karibu na kichwa chake, tuondoke.”
12 I David uze koplje i èašu za vodu, što bješe èelo glave Saulu, i otidoše; i niko ih ne vidje ni osjeti, niti se koji probudi, nego svi spavahu; jer bješe napao na njih tvrd san od Gospoda.
Hivyo Daudi akachukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyokuwa karibu na kichwa cha Sauli, nao wakaondoka. Hakuna yeyote aliyeona au kufahamu habari hii, wala hakuna hata mmoja aliyeamka usingizini. Wote walikuwa wamelala, kwa sababu Bwana alikuwa amewatia kwenye usingizi mzito.
13 I David prešav na drugu stranu stade navrh brda izdaleka; i bješe izmeðu njih mnogo mjesta.
Kisha Daudi akavuka upande mwingine na kusimama juu ya kilima mahali palipokuwa na nafasi pana kati yao.
14 I stade David vikati narod i Avenira sina Nirova govoreæi: što se ne odzivaš, Avenire? A Avenir se odazva i reèe: koji si ti što vièeš cara?
Daudi akalipigia kelele jeshi na Abneri mwana wa Neri, akisema, “Je, Abneri, hutanijibu?” Abneri akajibu, “Nani wewe umwitaye mfalme?”
15 A David reèe Aveniru: nijesi li ti junak? i ko je kao ti u Izrailju? Zašto nijesi èuvao cara gospodara svojega? Jer je išao jedan iz naroda da ubije gospodara tvojega.
Daudi akasema, “Wewe si ni mtu shujaa? Ni nani aliye kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukumlinda mfalme bwana wako? Mtu mmoja alikuja kumwangamiza mfalme, bwana wako.
16 Nijesi dobro radio. Tako da je živ Gospod, zaslužili ste smrt što nijeste èuvali gospodara svojega, pomazanika Gospodnjega. Eto, gledaj, gdje je koplje carevo i èaša za vodu što mu bješe èelo glave?
Ulichokifanya si kizuri. Kwa hakika kama aishivyo Bwana, wewe na watu wako mnastahili kufa, kwa sababu hamkumlinda bwana wenu, mpakwa mafuta wa Bwana. Tazameni hapo mlipo. Uko wapi mkuki wa mfalme na gudulia la maji ambavyo vilikuwa karibu na kichwa chake?”
17 Tada Saul pozna glas Davidov, i reèe: je li to tvoj glas, sine Davide? A David reèe: moj je glas, care gospodaru!
Sauli akatambua sauti ya Daudi, na kusema, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Daudi akajibu, “Naam, hiyo ndiyo, bwana wangu mfalme.”
18 Još reèe: zašto gospodar moj goni slugu svojega? jer šta sam uèinio? i kako je zlo u ruci mojoj?
Pia akaongeza, “Kwa nini bwana wangu anamfuatia mtumishi wake? Nimefanya nini, nalo kosa langu ni lipi nililolifanya niwe na hatia?
19 Zato sada care gospodaru moj, poslušaj rijeèi sluge svojega. Ako te Gospod draži na mene, neka mu je ugodan prinos tvoj; ako li sinovi èovjeèiji, prokleti su pred Gospodom, jer me izagnaše danas da se ne držim našljedstva Gospodnjega, i rekoše: idi, služi tuðim bogovima.
Sasa mfalme bwana wangu na asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama Bwana amekuchochea dhidi yangu, basi yeye na aipokee sadaka yangu. Lakini hata hivyo, kama ni wanadamu waliofanya hivyo, walaaniwe mbele za Bwana! Wao sasa wamenifukuza kutoka sehemu yangu katika urithi wa Bwana wangu wakisema, ‘Nenda ukatumikie miungu mingine.’
20 Ali sada da ne padne krv moja na zemlju daleko od oèiju Gospodnjih; jer car Izrailjev izide da traži buhu jednu, kao kad ko goni jarebicu po planini.
Basi usiache damu yangu imwagike kwenye ardhi mbali na uso wa Bwana. Mfalme wa Israeli ametoka kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware katika milima.”
21 Tada reèe Saul: zgriješio sam; vrati se, sine Davide, neæu ti otsele èiniti zla, kad ti danas draga bi duša moja; evo, ludo sam radio i pogriješio sam veoma.
Ndipo Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Rudi, Daudi mwanangu. Kwa kuwa uliyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani leo, sitajaribu kukudhuru tena. Hakika nimetenda kama mpumbavu na nimekosa sana.”
22 A David odgovori i reèe: evo koplja careva; neka doðe koji od momaka i neka ga uzme.
Daudi akajibu, “Mkuki wa mfalme uko hapa. Mmoja wa vijana wako na avuke kuuchukua.
23 A Gospod æe platiti svakome po pravdi njegovoj i po vjeri njegovoj. Jer te bješe predao Gospod danas u ruke moje, ali ne htjeh dignuti ruke svoje na pomazanika Gospodnjega.
Bwana humlipa kila mtu kwa ajili ya haki yake na uaminifu wake. Bwana alikutia katika mikono yangu leo, lakini sikuinua mkono wangu juu ya mpakwa mafuta wa Bwana.
24 I zato, evo, kako je danas meni draga bila duša tvoja, tako neka bude draga moja duša pred Gospodom, i neka me izbavi iz svake nevolje.
Kwa hakika kama vile maisha yako yalivyokuwa ya thamani kwangu leo, vivyo hivyo maisha yangu na yawe na thamani kwa Bwana na kuniokoa kutoka taabu zote.”
25 A Saul reèe Davidu: da si blagosloven, sine moj Davide! izvršiæeš i nadvladaæeš. Tada David otide svojim putem, a Saul se vrati u svoje mjesto.
Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Mwanangu Daudi na ubarikiwe; utafanya mambo makubwa na hakika utashinda.” Basi Daudi akaenda zake, naye Sauli akarudi nyumbani.