< 1 Kraljevima 5 >
1 I Hiram car Tirski posla sluge svoje k Solomunu èuvši da su ga pomazali za cara na mjesto oca njegova, jer Hiram ljubljaše Davida svagda.
Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
2 A Solomun posla ka Hiramu i poruèi mu:
Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
3 Ti znaš da David otac moj nije mogao sagraditi doma imenu Gospoda Boga svojega od ratova kojima ga opkoliše, dokle ih Gospod ne položi pod noge njegove.
“Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
4 A sada Gospod Bog moj dao mi je mir otsvuda, nemam nijednoga neprijatelja ni zle smetnje.
Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
5 Zato, evo, velim da sagradim dom imenu Gospoda Boga svojega, kao što je rekao Gospod Davidu ocu mojemu govoreæi: sin tvoj, kojega æu posaditi mjesto tebe na prijesto tvoj, on æe sagraditi dom imenu mojemu.
Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
6 Zato zapovjedi sada neka mi nasijeku drva kedrovijeh na Livanu, a sluge æe moje biti sa slugama tvojim, a platu slugama tvojim daæu ti kako god reèeš; jer ti znaš da u nas nema ljudi koji umiju sjeæi drva kao Sidonci.
“Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
7 I kad Hiram èu rijeèi Solomunove, obradova se veoma i reèe: da je blagosloven Gospod danas, koji dade Davidu mudra sina nad onijem narodom velikim.
Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
8 I posla Hiram Solomunu, i poruèi: èuo sam èega radi si slao k meni; ja æu uèiniti svu volju tvoju za drva kedrova i za drva jelova.
Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
9 Moje æe sluge snijeti s Livana na more, i ja æu ih povezati u splavove i spustiti morem do mjesta koje mi kažeš, i ondje æu razvezati, pa ih nosi; a ti æeš uèiniti moju volju i dati hranu èeljadi mojoj.
Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
10 I tako davaše Hiram Solomunu drva kedrova i drva jelova, koliko mu bješe volja.
Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
11 A Solomun davaše Hiramu dvadeset tisuæa kora pšenice za hranu èeljadi njegovoj, i dvadeset kora ulja cijeðenoga; toliko davaše Solomun Hiramu svake godine.
naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
12 I Gospod dade mudrost Solomunu kako mu bješe obrekao, i bješe mir izmeðu Hirama i Solomuna, i uhvatiše vjeru meðu sobom.
Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
13 I odredi Solomun ljude iz svega Izrailja, i bi odreðenijeh trideset tisuæa ljudi.
Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
14 I slaše ih na Livan po deset tisuæa svakoga mjeseca naizmjence; jedan mjesec bijahu na Livanu, a dva mjeseca kod kuæa svojih. A Adoniram bješe nad ovijem poslenicima.
Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
15 I imaše Solomun sedamdeset tisuæa nosilaca i osamdeset tisuæa tesaèa u planini,
Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
16 Osim nastojnika Solomunovijeh, koji bijahu nad tijem poslom, tri tisuæe i trista, koji upravljahu narodom koji poslovaše taj posao.
pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
17 I zapovjedi car da snose veliko kamenje, skupocjeno kamenje za temelj domu, tesano kamenje.
Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
18 I tesahu poslenici Solomunovi i poslenici Hiramovi i Givleji, i pripravljahu drvo i kamenje da se zida dom.
Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.