< 1 Kraljevima 15 >
1 A osamnaeste godine carovanja Jerovoama sina Navatova zacari se Avijam nad Judom.
Katika mwaka wa kumi na tano wa mfame Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya alianza kutawala juu yaYuda.
2 I carova tri godine u Jerusalimu. A materi mu bješe ime Maha kæi Avesalomova.
Alitawala kwa miaka mitata kule Yerusalemu. Jina la mama yake allikuwa Maaka. Alikuwa binti wa Absalomu.
3 On hoðaše u svijem grijesima oca svojega, koje je èinio pred njim, i ne bješe srce njegovo cijelo prema Gospodu Bogu njegovu kao srce Davida oca njegova.
Naye alitembea katika dhambi zote ambazo baba yake alizifanya kabla yake; moyo wake haukuwa mkalifu kwa BWANA, Mungu wake kama moyo wa Daudi, babu yake ulivyokuwa.
4 Ali radi Davida dade mu Gospod Bog njegov vidjelo u Jerusalimu podigav sina njegova nakon njega i utvrdiv Jerusalim;
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi, BWANA, Mungu wake alimpa taa Yerusalemu kwa kumwinua mwanae baada yake ili kuiimarisha Yerusalemu.
5 Jer je David èinio što je pravo pred Gospodom niti je otstupao od èega što mu je zapovjedio svega vijeka svojega osim stvari s Urijom Hetejinom.
Mungu alifanya haya kwa sababu Daudi alifanya yaliyo mema machoni pake; wakati wote wa uhai wake, hakugeuka wala hakukosa katika yote aliyomwamuru, isipokuwa tu swala la Uria Mhiti.
6 A rat bješe izmeðu Rovoama i Jerovoama do njegova vijeka.
Sasa kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Jeroboamu katika siku zote za maisha ya Abiya.
7 A ostala djela Avijamova i sve što je èinio nije li zapisano u dnevniku careva Judinijeh? A bijaše rat izmeðu Avijama i Jerovoama.
Kwa mambo mengine ya Abiya, yote aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda? Sasa kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
8 I Avijam poèinu kod otaca svojih, i pogreboše ga u gradu Davidovu, a na njegovo mjesto zacari se Asa sin njegov.
Abiya akalala na mababu zake, nao wakamzika katika mji wa Daudi. Asa mwanae akawa mfalme mahali pake.
9 Godine dvadesete carovanja Jerovoamova nad Izrailjem zacari se Asa nad Judom.
Katika mwaka wa ishirini wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akaanza kutawala Yuda.
10 Èetrdeset i jednu godinu carova u Jerusalimu. A materi mu bješe ime Maha kæi Avesalomova.
Alitawala kwa miaka arobaini na moja kule Yerusalemu. Bibi yake alikuwa Maaka, binti wa Absalomu.
11 I tvoraše Asa što je pravo pred Gospodom kao David otac mu.
Asa akafanya yaliyo mema machono mwa BWANA, kama alivyofanya Daudi, babu yake.
12 Jer istrijebi adžuvane iz zemlje i ukide sve gadne bogove koje bjehu naèinili oci njegovi.
Yeye aliwafukuza kutoka katika nchi wale makahaba wa kipagani na akaziondoa sanamu zote ambazo babu zake walikuwa wametengeneza.
13 I mater svoju Mahu svrže s vlasti, jer ona naèini idola u lugu; i Asa izlomi idola i sažeže na potoku Kedronu.
Pia alimwondoa bibi yake asiwe Malkia, kwa sababu alikuwa amefanya sanamu ya kuchukiza kwa Ashera. Asa aliikata sanamu ya kuchukiza na kuiteketeza katika Bonde la Kidroni.
14 Ali visine ne biše oborene; ali srce Asino bješe cijelo prema Gospodu svega vijeka njegova.
Lakini pale mahali pa juu hapakuchukuliwa. Hata hivyo. Moyo wa Asa ulikuwa mkamilifu mbele ya BWANA katika siku zake zote.
15 I unese u dom Gospodnji što bješe posvetio otac njegov i što on posveti, srebro i zlato i sudove.
Alivirerjesha katika nyumba ya BWANA vitu vile vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya BWANA, na vile vitu vyake vilivyokuwa vimetengezwa kwa fedha, na dhahabu na vyombo.
16 I bješe rat izmeðu Ase i Vase cara Izrailjeva svega vijeka njihova.
Basi kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli, kwa miaka yao yote.
17 Jer Vasa car Izrailjev izide na Judu i stade zidati Ramu da ne da nikome otiæi k Asi caru Judinu ni od njega doæi.
Baasha mfalme wa Israeli, akaivamia na kuijenga Rama, kiasi kwamba hakumruhusu yeyote kuondoka au kuingia katika nchi ya Asa mfalme wa Yuda.
18 Ali Asa uzev sve srebro i zlato što bješe ostalo u riznici Gospodnjoj i u riznici doma careva dade ga slugama svojim, i posla ih car Asa Ven-Adadu sinu Tavrimona sina Esionova, caru Sirskom, koji stanovaše u Damasku, i poruèi:
Kisha Asa akazichukua zile fedha na dhahabu zilizokuwa zimebaki kwenye hazina kwenye nyumba ya BWANA, na katika hazina ya ikulu ya mfalme. Akaziweka katika mikono ya watumishi wake na kuzituma kwa Beni Hadadi mwana wa Tabrimoni mwana wa Hezioni, mfalme wa Shamu ambaye alikuwa akishi Dameski. Akamwambia,
19 Vjera je izmeðu mene i tebe, izmeðu oca tvojega i oca mojega; evo šaljem ti dar, srebro i zlato; hajde, pokvari vjeru koju imaš s Vasom carem Izrailjevim, eda bi otišao od mene.
“Naomba tufanye patano kati yangu na wewe, kama ilivyokuwa kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, Nimekutumia zawadi ya fedha na dhahabu. Ili uvunje agano lako na Baasha mfalme wa Israeli, ili kwamba aniache.”
20 I posluša Ven-Adad cara Asu, i posla vojvode svoje na gradove Izrailjeve i pokori Ijon i Dan i Avel-Vetmahu i sav Hinerot i svu zemlju Neftalimovu.
Beni Hadadi akamsikiliza mfalme Asa na kutuma wakuu wa majeshi yake, nao wakaishambulia miji ya Israeli. Wakaishambulia Ijoni, Dani, Abeliya Bethi Maaka, na Kinerothi yote, pamoja na nchi yote ya Naftali.
21 A kad Vasa to èu, presta zidati Ramu, i vrati se u Tersu.
Ikawa Baasha aliposikia haya, akaacha kuijenga Rama akarudi Tirza.
22 Tada car Asa sazva sav narod Judin, nikoga ne izuzimajuæi; te odnesoše kamenje iz Rame i drva, èim zidaše Vasa, i od njega sazida car Asa Gevu Venijaminovu i Mispu.
Kisha mfalme Asa akaitangazia Yuda yote. Hakuna aliyeachwa. Wakayabeba mawe na miti ya Rama ambayo Baasha alikuwa akijengea mji. Kisha mfalme Asa akavitumia hivyo vitu kuijenga Geba ya Benjamini na Mispa.
23 A ostala sva djela Asina i sva junaštva njegova, i što je god èinio i koje je gradove sagradio, nije li sve zapisano u dnevniku careva Judinijeh? Ali u starosti svojoj bolovaše od nogu.
Mambo mengine yanyohusu utawala wa Asa, uwezo wake wote, yote aliyofanya, na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda? Lakini wakati wa uzee wake alipata ugonjwa wa miguu.
24 I Asa poèinu kod otaca svojih, i bi pogreben kod otaca svojih u gradu Davida oca svojega. A na njegovo mjesto zacari se Josafat sin njegov.
Kisha Asa akalala na mababu zake na akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Yehoshafati mwanae akawa mfalme mahali pake.
25 A Nadav sin Jerovoamov poèe carovati nad Izrailjem druge godine carovanja Asina nad Judom; i carova nad Izrailjem dvije godine.
Nadabu mwana wa Yerobiamu alianza kutawala huko Israeli wakati wa mwaka wa pili wa Asa mfalme wa Yuda; Aliitawala Israeli kwa miaka miwili.
26 I èinjaše što je zlo pred Gospodom hodeæi putem oca svojega i u grijehu njegovu, kojim navede na grijeh Izrailja.
Akafanya yaliyo maovu mbele y a macho ya BWANA naye akatembea katika njia ya baba yake, na katika dhambi yake, aliisababisha Israeli kufanya dhambi.
27 I diže bunu na nj Vasa sin Ahijin od doma Isaharova, i ubi ga Vasa kod Givetona, koji bijaše Filistejski, kad Nadav i sav Izrailj bjehu opkolili Giveton.
Baasha mwana wa Ahiya, wa familia ya Isakari, akafanya hila dhidi ya Nadabu; Baasha akamwua huko Gibethoni, ambao ulikuwa mji wa Wafilisti, kwa kuwa Nadabu na Israeli walikuwa wakiuhusuru Gibethoni.
28 I tako ga ubi Vasa treæe godine carovanja Asina nad Judom, i zacari se na njegovo mjesto.
Katika mwaka wa tatu wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha alimwua Nadabu naye akawa mfalme mahali pake.
29 A kad se zacari, pobi sav dom Jerovoamov, i ne ostavi nijedne duše od roda Jerovoamova dokle sve ne istrijebi po rijeèi Gospodnjoj, koju reèe preko sluge svojega Ahije Silomljanina,
Mara tu baad ya kuwa mfalme, Baasha aliwaua watu wote wa familia ya Yeroboamu. Hakumwacha hata mmoja wa uzao wa Yeroboamu awe hai; Kwa njia hii akawa ameuharibu ukoo wote wa kifalme, kama vile BWANA alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake Ahiya Mshilo,
30 Za grijehe Jerovoamove, kojima je griješio i kojima je na grijeh naveo Izrailja, i za draženje kojim je dražio Gospoda Boga Izrailjeva.
kwa sababu ya dhambi za Yeroboamu ambazo alifanya na akaisababishia Israeli kufanya dhambi, kwa kuwa alimkasirisha BWANA, Mungu wa Israeli.
31 A ostala djela Nadavova i sve što je èinio, nije li to zapisano u dnevniku careva Izrailjevijeh?
Mambo mengine yanayomhusu Nadabu, na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
32 I bješe rat izmeðu Ase i Vase cara Izrailjeva svega vijeka njihova.
Kisha kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli katika siku zao zote.
33 Treæe godine carovanja Asina nad Judom zacari se Vasa sin Ahijin nad svijem Izrailjem u Tersi, i carova dvadeset i èetiri godine.
Katika mwaka wa tatu wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya alianza kuitawala Israeli yote huko Tirza naye alitawala kwa miaka ishirini na nne.
34 I èinjaše što je zlo pred Gospodom hodeæi putem Jerovoamovijem i u grijehu njegovu, kojim navede na grijeh Izrailja.
Naye akafanya yaliyo mabaya katika macho ya BWANA na akatembea katika njia ya Yeroboamu na katika dhambi yake ambayo kwa hiyo aliifanya Israeli kufanya dhambi.