< yohana.h 1 >

1 aadau vaada aasiit sa ca vaada ii"svare. na saardhamaasiit sa vaada. h svayamii"svara eva|
Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
2 sa aadaavii"svare. na sahaasiit|
Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
3 tena sarvva. m vastu sas. rje sarvve. su s. r.s. tavastu. su kimapi vastu tenaas. r.s. ta. m naasti|
Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
4 sa jiivanasyaakaara. h, tacca jiivana. m manu. syaa. naa. m jyoti. h
Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
5 tajjyotirandhakaare pracakaa"se kintvandhakaarastanna jagraaha|
Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
6 yohan naamaka eko manuja ii"svare. na pre. sayaa ncakre|
Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
7 tadvaaraa yathaa sarvve vi"svasanti tadartha. m sa tajjyoti. si pramaa. na. m daatu. m saak. sisvaruupo bhuutvaagamat,
Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
8 sa svaya. m tajjyoti rna kintu tajjyoti. si pramaa. na. m daatumaagamat|
Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
9 jagatyaagatya ya. h sarvvamanujebhyo diipti. m dadaati tadeva satyajyoti. h|
Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
10 sa yajjagadas. rjat tanmadya eva sa aasiit kintu jagato lokaasta. m naajaanan|
Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
11 nijaadhikaara. m sa aagacchat kintu prajaasta. m naag. rhlan|
Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
12 tathaapi ye ye tamag. rhlan arthaat tasya naamni vya"svasan tebhya ii"svarasya putraa bhavitum adhikaaram adadaat|
Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
13 te. saa. m jani. h "so. nitaanna "saariirikaabhilaa. saanna maanavaanaamicchaato na kintvii"svaraadabhavat|
Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
14 sa vaado manu. syaruupe. naavatiiryya satyataanugrahaabhyaa. m paripuur. na. h san saardham asmaabhi rnyavasat tata. h pituradvitiiyaputrasya yogyo yo mahimaa ta. m mahimaana. m tasyaapa"syaama|
Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
15 tato yohanapi pracaaryya saak. syamida. m dattavaan yo mama pa"scaad aagami. syati sa matto gurutara. h; yato matpuurvva. m sa vidyamaana aasiit; yadartham aha. m saak. syamidam adaa. m sa e. sa. h|
Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
16 apara nca tasya puur. nataayaa vaya. m sarvve krama"sa. h krama"sonugraha. m praaptaa. h|
Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
17 muusaadvaaraa vyavasthaa dattaa kintvanugraha. h satyatva nca yii"sukhrii. s.tadvaaraa samupaati. s.thataa. m|
Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
18 kopi manuja ii"svara. m kadaapi naapa"syat kintu pitu. h kro. dastho. advitiiya. h putrasta. m prakaa"sayat|
Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
19 tva. m ka. h? iti vaakya. m pre. s.tu. m yadaa yihuudiiyalokaa yaajakaan levilokaa. m"sca yiruu"saalamo yohana. h samiipe pre. sayaamaasu. h,
Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
20 tadaa sa sviik. rtavaan naapahnuutavaan naaham abhi. sikta itya"ngiik. rtavaan|
Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
21 tadaa te. ap. rcchan tarhi ko bhavaan? ki. m eliya. h? sovadat na; tataste. ap. rcchan tarhi bhavaan sa bhavi. syadvaadii? sovadat naaha. m sa. h|
Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
22 tadaa te. ap. rcchan tarhi bhavaan ka. h? vaya. m gatvaa prerakaan tvayi ki. m vak. syaama. h? svasmin ki. m vadasi?
Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
23 tadaa sovadat| parame"sasya panthaana. m pari. skuruta sarvvata. h| itiida. m praantare vaakya. m vadata. h kasyacidrava. h| kathaamimaa. m yasmin yi"sayiyo bhavi. syadvaadii likhitavaan soham|
Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
24 ye pre. sitaaste phiruu"silokaa. h|
Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
25 tadaa te. ap. rcchan yadi naabhi. siktosi eliyosi na sa bhavi. syadvaadyapi naasi ca, tarhi lokaan majjayasi kuta. h?
wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
26 tato yohan pratyavocat, toye. aha. m majjayaamiiti satya. m kintu ya. m yuuya. m na jaaniitha taad. r"sa eko jano yu. smaaka. m madhya upati. s.thati|
Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
27 sa matpa"scaad aagatopi matpuurvva. m varttamaana aasiit tasya paadukaabandhana. m mocayitumapi naaha. m yogyosmi|
Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
28 yarddananadyaa. h paarasthabaithabaaraayaa. m yasminsthaane yohanamajjayat tasmina sthaane sarvvametad agha. tata|
Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
29 pare. ahani yohan svanika. tamaagacchanta. m yi"su. m vilokya praavocat jagata. h paapamocakam ii"svarasya me. sa"saavaka. m pa"syata|
Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
30 yo mama pa"scaadaagami. syati sa matto gurutara. h, yato hetormatpuurvva. m so. avarttata yasminnaha. m kathaamimaa. m kathitavaan sa evaaya. m|
Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
31 apara. m naahamena. m pratyabhij naatavaan kintu israayellokaa ena. m yathaa paricinvanti tadabhipraaye. naaha. m jale majjayitumaagaccham|
Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
32 puna"sca yohanaparameka. m pramaa. na. m datvaa kathitavaan vihaayasa. h kapotavad avatarantamaatmaanam asyoparyyavati. s.thanta. m ca d. r.s. tavaanaham|
Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
33 naahamena. m pratyabhij naatavaan iti satya. m kintu yo jale majjayitu. m maa. m prairayat sa evemaa. m kathaamakathayat yasyoparyyaatmaanam avatarantam avati. s.thanta nca drak. sayasi saeva pavitre aatmani majjayi. syati|
Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
34 avastanniriik. syaayam ii"svarasya tanaya iti pramaa. na. m dadaami|
Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
35 pare. ahani yohan dvaabhyaa. m "si. syaabhyaa. m saarddhe. m ti. s.than
Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
36 yi"su. m gacchanta. m vilokya gaditavaan, ii"svarasya me. sa"saavaka. m pa"syata. m|
Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
37 imaa. m kathaa. m "srutvaa dvau "si. syau yii"so. h pa"scaad iiyatu. h|
Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
38 tato yii"su. h paraav. rtya tau pa"scaad aagacchantau d. r.s. tvaa p. r.s. tavaan yuvaa. m ki. m gave"sayatha. h? taavap. rcchataa. m he rabbi arthaat he guro bhavaan kutra ti. s.thati?
Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
39 tata. h sovaadit etya pa"syata. m| tato divasasya t. rtiiyapraharasya gatatvaat tau taddina. m tasya sa"nge. asthaataa. m|
Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
40 yau dvau yohano vaakya. m "srutvaa yi"so. h pa"scaad aagamataa. m tayo. h "simonpitarasya bhraataa aandriya. h
Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
41 sa itvaa prathama. m nijasodara. m "simona. m saak. saatpraapya kathitavaan vaya. m khrii. s.tam arthaat abhi. siktapuru. sa. m saak. saatk. rtavanta. h|
Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
42 pa"scaat sa ta. m yi"so. h samiipam aanayat| tadaa yii"susta. m d. r.s. tvaavadat tva. m yuunasa. h putra. h "simon kintu tvannaamadheya. m kaiphaa. h vaa pitara. h arthaat prastaro bhavi. syati|
Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
43 pare. ahani yii"sau gaaliila. m gantu. m ni"scitacetasi sati philipanaamaana. m jana. m saak. saatpraapyaavocat mama pa"scaad aagaccha|
Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
44 baitsaidaanaamni yasmin graame pitaraandriyayorvaasa aasiit tasmin graame tasya philipasya vasatiraasiit|
Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
45 pa"scaat philipo nithanela. m saak. saatpraapyaavadat muusaa vyavasthaa granthe bhavi. syadvaadinaa. m granthe. su ca yasyaakhyaana. m likhitamaaste ta. m yuu. sapha. h putra. m naasaratiiya. m yii"su. m saak. saad akaar. sma vaya. m|
Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
46 tadaa nithanel kathitavaan naasarannagaraata ki. m ka"sciduttama utpantu. m "saknoti? tata. h philipo. avocat etya pa"sya|
Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
47 apara nca yii"su. h svasya samiipa. m tam aagacchanta. m d. r.s. tvaa vyaah. rtavaan, pa"syaaya. m ni. skapa. ta. h satya israayelloka. h|
Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
48 tata. h sovadad, bhavaan maa. m katha. m pratyabhijaanaati? yii"suravaadiit philipasya aahvaanaat puurvva. m yadaa tvamu. dumbarasya tarormuule. asthaastadaa tvaamadar"sam|
Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
49 nithanel acakathat, he guro bhavaan nitaantam ii"svarasya putrosi, bhavaan israayelva. m"sasya raajaa|
Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
50 tato yii"su rvyaaharat, tvaamu. dumbarasya paadapasya muule d. r.s. tavaanaaha. m mamaitasmaadvaakyaat ki. m tva. m vya"svasii. h? etasmaadapyaa"scaryyaa. ni kaaryyaa. ni drak. syasi|
Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
51 anyaccaavaadiid yu. smaanaha. m yathaartha. m vadaami, ita. h para. m mocite meghadvaare tasmaanmanujasuununaa ii"svarasya duutaga. nam avarohantamaarohanta nca drak. syatha|
Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”

< yohana.h 1 >